Kimbisa na Lukuvi; Mnasubiri Wafadhili na Wahisani au Amri Kutoka Ikulu?

Rev.Kishoka,

..dawa ni kuanzisha redio inayopigia kelele uongozi mbovu wa CCM mpaka wananchi waelewe somo.

..vilevile watafutwe wajanja wa kutengeneza political ads. nadhani kuna statements nyingi sana wanazotoa unaweza kuzitumia against them.
 
Rev.Kishoka,

..dawa ni kuanzisha redio inayopigia kelele uongozi mbovu wa CCM mpaka wananchi waelewe somo.

..vilevile watafutwe wajanja wa kutengeneza political ads. nadhani kuna statements nyingi sana wanazotoa unaweza kuzitumia against them.

Halafu vijana wanaograduate masomo ya media na arts watakwambia kazi hamna wakati sehemu kibao za kuwa innovative zipo.Kila mtu anataka kuajiriwa.
 

Samahani mkuu kama nitakuwa nakutukana. Lakini mambo ya kusema kuwa huku Rwanda Kagame anafanya hivi au vile ni UPUUZI MTUPU.

Rwanda ni kubwa kuliko Kagame. Hivyo Kagame kuna siku ataiacha Rwanda. Je ni nani atakayefanya kazi ya kuangalia ufanisi?

Usafi ni kwa faida yako. Kwanini president aje kuhimiza usafi?

Kuna vitu vya collective responsibility, na umefika wakati tuanze kuchukua majukumu yetu.
 
Halafu vijana wanaograduate masomo ya media na arts watakwambia kazi hamna wakati sehemu kibao za kuwa innovative zipo.Kila mtu anataka kuajiriwa.

Ni vigumu mtu kuona matatizo yake. Uwezekano mkubwa ni hao vijana kuwa wachafu.
 
Rev.Kishoka,

..dawa ni kuanzisha redio inayopigia kelele uongozi mbovu wa CCM mpaka wananchi waelewe somo.

..vilevile watafutwe wajanja wa kutengeneza political ads. nadhani kuna statements nyingi sana wanazotoa unaweza kuzitumia against them.

Ahahahahahahaaa...Joka...bongo siyo Marekani..lol. Mambo ya "I voted for it before I voted against it" katika siasa za bongo bado hayajashika nafasi. Unahitaji a 24hr news cycle kwa vitu kama hvyo kuwa effective. Sasa bongo watu wangapi wana access za media outlet kama Nyamwezi?
 

Julius,

..Iran walikuwa na mahubiri ya Ayatollah aliyekuwa exiled in France kwenye audio tapes.

..Sumaye naye alikuwa blitz kwenye magazeti kwa kila upuuzi aliousema. effect yake ni kwamba leo hii anaonekana ni fisadi kuliko Mkapa.

..Tanzania kila weekend wananchi wanaangali English premium league, why not run a political ad now and then. walioko vijijini kule kusikukuwa na access ya hivi vitu watasimuliwa.
 

Never underestimate us bwana, tunajua first eleven na reserves wa timu zote za premier leugue, la liga, serie A, bundesliga lakini hatujui hata diwani wetu na mbunge ni nani na anatakiwa kufanya nini kwetu, bongo tambarare bwana. Kuonyesha ligi hizo ni kurekebisha maisha kiingilio 500 bobs half time wanaweka vitu vya ajabu, weka siasa utakufa njaa na dish lako utashindwa hata kulipia DSTV.
 
Wakuu zangu binafsi nadhani hatuna haja ya kulalamikia Madiwani na viongozi wadogo wa halmashauri. Binafsi naamini mfumo mzima wa Utawala nchini ni MBAYA. Mfumo mzima wa Utawala unatakiwa kutazamwa upya.

Tumeanzisha halmashauri za miji lakini bado kila kitu kipo centralized kiasi kwamba halmashauri hizi zinategemea panga toka serikali kuu badala ya Halmashauri kujiendesha zenyewe kwa mtaji unatolewa na serikali.
Mwalimu Nyerere kawaachia rasilimali nyingi sana kutokana na Ujamaa wake. Alijenga nyumba za NHC kibao, akataifisha nyumba nyingine nyingi tu kiasi kwamba serikali ilikuwa na nyumba nyingi pengine kuliko hata watu binafsi kwa hesabu. Leo hii hatupo tena katika Ujamaa. Hizi nyumba zilitakiwa zichujukuliwe na Halmashauri wazipangishe wao at market rate, hizo Bustani, Parking lot, michezo na maonyesho asilimia fulani ingekuwa ni mapato ya halamashuari hizi kila siku..Lakini unakuta Ukiritimba ambao mkuu wa wilaya (mwakilishi wa rais) ndiye hakimu wa mambo mengi ya kimaendeleo na sii ajabu kabisa ukaambiwa mkuu wa mkoa ama wilaya ndiye mwezeshaji wa mabadiliko ya mazingira na sii halmashauri ya miji..

Kifupi Halamashauri zetu hazina fedha na bahati mbaya bado halmashauri hizi zinajiendesha kisiasa zaidi ya kutoa huduma kwani waajira ktk kila halamashauri ni kubwa kuliko kazi walizokuwa nazo.. ule ule mpango wa Kijamaa, pato kubwa la halamashauri hizi linaishia kulipa mishahara ya wafanyakazi wake ambao hawafanyi kazi..
Eeeeeh! ni Tanzania tu ndo utakuta kuna waajiriwa Wafanyakazi ambao Hawafanyikazi!
 
Mhe. Jaji Warioba wakati akiwa Mhe. Waziri wa Serikali za Mitaa, aliwahi kutamka kwamba "HIVI KILA KITU MNASUBILI MFANYIWE NA SERIKALI ZA MITAA? HATA UCHAFU ULI MBELE YA NYUMBA YAKO HATA MAJANI YALIYOOTA MBELE YA NYUMBA YAKO UNATAKA KIMBISA AU LUKUVI WAJE KUZOA AU KUPALIA AU KUFYEKA?"

Unajua huwa napata shida sana kuona sisi Watanzania tunapenda sana UCHAFU na wala hatuna UOGA na uchafu.

Utakuta mtu anamenya viazi anatoka nje anatupa maganda mlangoni, ukiuliza LUKUVI NA KIMBISA watakuja kuzoa eti?

Nenda kwenye Maduka ya Kariakoo, utacheka mtu anafungua mzigo wake wa nguo au viatu, kisha anatupa makasha hovyo tu barax2ni na hakuna hata mtu anayemuona akamuambia HEBU NDUGU ACHA UCHAFU.

Nenda kwenye vyoo vyetu majumbani kila siku utasikia watu wanaanguka bafuni kwa sababu watu hawataki kupiga deki na hata vyoo vinatoa harufu ambayo hata mende hawezi kuishi lakini sisi hatuna wasix2, mtu ataingia ****** na kukaa humo nusu saa. akitoka kwanza apigwe upepo maana utafikir kinyesi kimemjaa mwilini. Hili nalo TUNAWASUBILI KIMBISA NA LUKUVI waje.

Mtu anakula ndizi, chungwa n.k anaamua kutupa barax2ni kisa Serikali za Mitaa zitakuja kuzoa eti?

Unajua kila mara huwa KICHWA kinaniuma sana unakuta KONDAKTA wa DALAX2 shati hana na kwapani kumejaa ndevu jasho la DSM linamtoka ananuka lakini hakuna wa kumueleza TUNASUBILI LUKUVI NA KIMBISA.

Mie jamani napata shiiiiiiida. Ona hata Mfano huu, kwa ajili ya usalama watu tunaambiwa tufunge mikanda ya gari, lakini uatakuta Mtu anasema trafiki huyo funga mkanda tusije pigwa faini. Na siyo afunge Mkanda kwa ajili ya usalama wake bali asitozwe faini.

Utacheka sana. Kula kwenye maghorofa tunawajuwa kabisa watu wanaojisaidia kwenye mifuko na kutupa uchafu wao chini, Lakini hutaki kwenye kusema kwenye vyombo husika AU MUANDAMANE BASI
 
Wasegesege,

Mkuu haya maneno ya Warioba yalikuwa hayana ukweli kabisa.. nyumba nyingi Dar es Salaam husafishwa na wenye nyumba isipokuwa uchafu toka ktk nyumba zao ndio huu tunaoonyeshwa katika picha hizi.
Sijui kama umejiuliza wewe mwenyewe ya kwamba, kama wananchi watasafisha uchafu wa nyumba zao huo uchafu waupeleke wapi?..
Ebu wewe nambie ukisha safisha nyumba yako utatupa wapi hizo taka zako..Nina hakika wazo litakalo kuja ni kuchoma hizo taka..Fikiria hilo moshi linalotoka hapo kwa afya ya hao hao mnaowalaumu..
Tatizo hakuna utamaduni wa usafi hata kidogo, kwa waliosoma na kina sisi mbumbumbu.. Ujenzi wa miji yetu hadi leo ni sawa na maisha ya mswahili.. Tunajenga vyoo kuhifadhi kinyesi na ni jukumu la mwenye nyumba kumwagilia chunvi kila baada ya muda kupunguza ujazo.. Hivyo uchafu wa vyoo unahifadhiwa utafikiri tunatengeneza mbolea fulani, wakati mji mzima umejengwa pasipo mifereji na maji machafu.
 
Solution ya hili swala ni simple. Wananchi mkae chini, mgeuzi ishu iwe run privately. Mkikaa na kusubiri sijui serikali, mtasubiri mpaka kufa. Gaweni ajira hizo. Serikali ikiwanyima, ongeeni na mbunge wenu, andikeni magazetini, fanyeni maandamano, fungeni barabara. Dont wait for change...be the catalyst for change. That shld be the new motto, na tuanze hapa ndani JF. Pia naombeni badala ya kuvunjana moyo, tuweni watu wa kutoa suggestions zaidi ya kuzungumzia matatizo. Ama sivyo JF itabaki pale pale.
 
Jamani wa TZ tutakuwa tumerogwa,Hivi wewe umemenya viazi vyako vya chipsi,unavizia usiku unaenda kutupa takataka Barabarani,Halafu unasubiri Rais/serikali ije ikuzolee taka au uhimizwe uzoe kwa viboko!?? Hizi ni akili au matope?
Mungu wangu tutabaki kulalamika kila siku hata kwa mambo yasiyostahili.
 
Walitakiwa wakatupe wapi?..ndio swali nalotaka kujua mimi..
 
Walitakiwa wakatupe wapi?..ndio swali nalotaka kujua mimi..
Mimi ninapokaa tuna mifuko maalumu tunakusanya Taka mara nyingi kwa wiki.Then wanakuja wale wenye ajira zao na mikokoteni na kuzichukua na tunalipia huduma hiyo,na wao wanazipeleka kwenye dampo.Sehemu nyingine nimeona magari huwa yanapita kukusanya.Wale wanatupa barabarani wanakwepa kulipia hiyo 500/= je unadhani hii ni sawa?
 
Hivi ktk fikra zako uchafu huo unaouona hapo ktk picha umefanywa na watu binafsi wenye nyumba zao jirani?.. Hao unaowapa uchafu wenye mikokoteni ndio hao wanaotupa taka hizo barabarani kwa sababu hizo unaziita ajira hazilipi..Hakuna utaratibu maalumwa kutpa taka na wala huyo mwenye mkokoteni hafuatwi.

Mkuu wangu, kuna Mshikaji wangu kaleta hayo mapipa ya taka unayoyaona mjini haswa wilaya ya Ilala na Kinondoni..mapipa ya kileo na imemgharimu kiasi kikubwa sana. Ka invest fedha yake binafsi na kachukua mikopo kutuwezesha tuwe na utaratibu wa taka..Jamaa kufika Bongo siasa zikaanza, kafunga mapipa ya taka halipwi fedha yoyote ati serikali wanategemea yeye ajitangaze na atafute tender za matangazo iwe ndio malipo yake. Kapewa kazi nyingine na kaa hataki aondowe mapipa yake, hiyo baada ya kuyaleta.

Haya wanaokuja chukua uchafu ilikuwa tender nyingine watu wakagombea baada ya mapipa kuwepo..Yaleyale ya Songos atuletee gas lakini mabomba ya kusafirishwa Mwanza apewe Richmond wakati ahadi ya mwanzo ilikuwa Songos wajenge wao mabomba hayo.

Hivi mkuu unakumbuka wakati wa mwalimu mji wetu pamoja na uchovu wake ulivyokuwa msafi?..Je, Unakumbuka wakati PWD, Comworks hadi idara ya ujenzi kama sikosei barabara zikisafishwa na mifereji kuondolewa michanga! Kama iliwezekana enzi za Ukoloni na Ujamaa, wakati watu ni hao hao iweje leo tushindwe wakati serikali ina uwezo mkubwa zaidi kifedha. nakumbuka enzi zetu kule chini harbourfront ya Posta ya zamani kulikuwa na taa na bustani nzuri tu watu wakipumzika wakati wakisubiri usafiri wa UDA...
Lakini nambie siku hizi nasikia ndio crib ya majambazi watu hawapandi tena daladala Posta ya zamani.. Kifupi Dar leo hii usiku wa saa tatu kila mtu kituoni huwezi kuona biashara yoyote mjini.Kwanza kiza halafu mji umekufa kabisa...Sasa Ujambazi ukianza mjini mtasema wananchi ndio tabia yao! wapi umeona mji hauna taa kabisa za barabarani na biashara zote zimefungwa baada ya saa 12 jioni..Wapi?
 


Mkuu,

Wakati mwingine hata maelekezo ya Rais hayafuatwi na watendaji wake and nobody cares. Rais alitoa amri barabara ya Mabibo-Kigogo ijengwe kwa kiwango cha lami lakini hivi ninavyoandika barabara hiyo ni maandaki ambayo ukiwa na gari dogo huwezi kupita au mvua ikinyesha hata magari makubwa hayawezi kupita. Diwani anakaa mitaa ile lakini anachojali yeye ni sitting allowance na sio maendeleo kwenye eneo lake.

Wanatia aibu.

Tiba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…