Kimenuka Instagram: Zari vs Wema Sepetu (Madam Range)

Nifah

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2014
Posts
34,020
Reaction score
79,098
Ni muendelezo wa vita ya maneno isiyoisha kati ya anayejiita Zari The Bosslady na wa kuitwa Tanzanians sweetheart Wema Sepetu.

Vita hiyo imeendelea leo kwa Zari kuanza kumtupia mafumbo mwenzie Wema,wapambe wa Wema wakacharuka na kumuita boss wao Wema ambaye alitaharuki na kuuliza kipi kinachoendelea?

Ndipo mpambe wake anayejiita wemareplies alipomuwekea screen shot ya aliyoyasema Zari.

Wema nae akajibu huku akisisitiza hana muda na Zari wala kaka (Diamond)

Kama haitoshi akapost picha huku akiweka caption ya kuwa kafunzwa na mamie kugombana na watu wazima (Zari) ni kukosa adabu.

Ndipo Zari nae akamjibu kuwa yuko busy na kazi,asijisumbue.

Nimeatach na screen shots za matukio yote.....

 
Nifah we mbeya hhhhhh
 
Basi tu nna mudi nzuri leo, ila ningekutukana.
 
Mtaa huu uko vizuri Nifah
 
Huyu zari naye kakosa adabu,kwa umri wake wema ni kama mwanae,anaanzaje kurushiana vijembe na mwanae?
Katika hili nimemdharau sana Zari.
Wema ameshamuachia huyo Diamond,anamfuata tena na vijembe vya nini?
Anaonekana ana stress sana baada ya kusikia Wema ana mimba.
Na sikutegemea Zari yule anayejidai mzungu kufanya uswahili wa namna hii.
Ni wazi Wema anamuumiza sana.
 
Ni kina nani hao!? Ngoja nimpigie simu babu yangu aliye kijijini..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…