Kimenuka: Lady jay Dee afunguka, Atoa wosia wake siku akifa

Malalamiko na tuhuma anazotoa Jay Dee(Anaconda) si mpya kwani zilishazungumzwa sana, zimeimbwa na kitabu zikatungiwa. Kama unataka ushahidi upo kwenye maandishi. Katafute FROM STREET TO PARLIAMENT.


Ebana elewa kuwa hakuna anaepinga hizo harakati.
Ila binafsi mishipa inanisimama kupinga unafiki aliouonesha huyo Bibi.
 
Matusi JF si angekuwa ashapigwa BAN?
Twendeni kwenye meza na tupeane majibu ya hili sakata.
Kwa kuanza basi Ruttashobolwa hebu eleza ni kitu gani unachompinga Putin?

Ndugu nafikiri kama una fatilia anavyo jibu hoja zake utagundua kuwa zimejaa matusi, kejeli, dharau japo si sehemu ya mada, kuhusu kupigwa ban ukumbuke kuwa si kila anaye tukana au kukejeli ana pigwa ban maana mods hawaoni kila kitu ndio maana kuna kitufe pale na mi sikutaka nikitumie kile maana tuna uwezo wa kurekebishana na kurudi kwenye mistari bila maneno ya maudhi, na bado na muhitaji kwenye mjadala huu.

Back to topic
hakuna anayempinga jyde hapa hata mmoja ambaye ameweza kuthibitisha jyde ana sema uongo au uzushi, ninachoona ni kuwa ni mtindo wa kujibu tuhuma kwa tuhuma hakuna lingine. wengi wanasema jyde ni mnafiki kuwa alikuwa wapi nami nawauliza kwa kuwa hakusema basi akisema ni uongo na uzushi.

Ndugu yake ameshindwa kuthibitisha jyde ana wasingizia au ni muongo zaidi naona na yeye ana toa tuhuma kwa jyde.
 
MTAZAMO WANGUi:-

*Namfananisha Jide na Muumini Mwinjuma...Kwa aina ya nyimbo wanazoimba...kwa sehemu kubwa zinabeba ujumbe wa kuonyesha wao ni wa kuonewa siku zote. Na hata anapotoka bendi moja Muumini lazima ataanza kutusi kule alipotoka. Ni aina ya watu wanaopenda kupata huruma muda wote. Inawezekana kuna tofauti kati ya Jide na uongozi wa clouds lakini kwa mtu wa sampuli ya Jide na Muumini utarajie Mayowe ili dunia nzima isikie. Hakuna "malaika" anayeweza kuridhisha wote, na hata unapojaribu kuridhisha kundi fulani lazima hawa wengine wataona kwa nini wale na sio sisi. Na watalalamika tu. Kwa hiyo pia lazima na sisi tujiulize ni kwa nini wao (wananufaika) na sio wale.

*Pia tukumbuke Jide kwa sasa anafight kimaisha (kibiashara n.k) kwa vyovyote lazima atakuwa "sensitive" kwa matukio yoyote hata kama ni ya kawaida tu haswa kama mambo yake (kibiashara) hayaendi kama anavyotarajia, Ni sawa na mtoto anayeishi na mama wa kambo akishajenga hisia za kuonewa hata ufanye nini ni vigumu kumridhisha.

*Hata Michael Jackon aliwahi kumshutumu mtu waliyetoka naye mbali TOMMY MATTOLA kwa vile tu albam ya INVINCIBLE haikufanya vizuri.

*Rai yangu kwa wasanii wote, wafanye kazi kwa kuangalia mustakabali wao, Bidii, ubunifu na kujituma ndio iwe kauli mbiu yako, yule anayekushika mkono kwa njia yoyote basi umpe heshima yake pale inapobidi. Na binadamu yeyote hapaswi kuishi kwa kutarajia mambo yatakuwa tambarare daima.

*Na kwa wanaclouds kama kuna mapungufu myafanyie kazi na msikate tamaa kuwasaidia wale ambao wapo tayari, na sisi wadau tupo nje tunaangalia..Wapo wasanii wanaofanya vizuri wakiwa sambamba na clouds sihitaji ushahidi mwingine zaidi ya huu, Ingawa nao pia wanaweza kuja kuwalaumu hapo baadae.

*Nakumbuka hata Dogojanja alimlaumu sana Madee, Na ni vigumu kwa mimi mwanainchi wa kawaida kujua ukweli haswa ni upi kati yao kila mmoja anajitetea kivyake, Maamuzi yanabaki kwa msikilizaji.
 
Hivi Unaweza Ongelea background ya mtu Humjui? Jibu hoja co kumtetea huyo BIBI.
Out of topic, hivi Jide ana umri gani? nimekuwa nikilisikia sana hili swala la umri ningependa kujuwa kama una taarifa sahihi za umri wake au watu aliosoma nao Primary au Secondary wana umri gani? niko interested sana kulijuwa hili don't ask me why!!
 
Ebana elewa kuwa hakuna anaepinga hizo harakati.
Ila binafsi mishipa inanisimama kupinga unafiki aliouonesha huyo Bibi.

Sawa hata kama anaonekana mnafiki kwa mtazamo wako, hilo haliwezi kubadili ukwel anaozungumza kuwa uwongo. Ukwel utabaki kuwa ukweli bila kujali nani anauzungumza.
 
....mkuu unajua kupigwa vita au unachukulia poa !.........unajua kuwa hawa wana studio iliyofadhiliwa na serikali ?
unaikumbuka vita ya vinega ambayo ilizimwa na Nchimbi kwa kuwapatanisha Sugu na Ruge?

Kwa hio unaunga mkono huyu dada ndio abebe kero za woooote, ndio aweke moyoni mwake HADI SIKU YA KUFA KWAKE?
jamani inabidi atafute kinywaji bariidi apooze machungu, fans tupo tu, tunambeba asonge mbele
Ila asisahau fadhila japo ni za zamani
 
Go JIDE! Lazima sanaa ifate direction sahii.Huu si wakati wa kuwaunga mkono wanyonyaji kupitia madhaifu ya JD kipindi cha nyuma.
Kama tulivyosimama na Sugu hapa JF sasa tunasimama na JIDE!
 
Go JIDE! Lazima sanaa ifate direction sahii.Huu si wakati wa kuwaunga mkono wanyonyaji kupitia madhaifu ya JD kipindi cha nyuma.
Kama tulivyosimama na Sugu hapa JF sasa tunasimama na JIDE!


mtazamo hebu nioneshe sehemu niliounga mkono wanyonyaji...
Hebu nionyese sehemu niliyowatetea Clouds...
Kisha ukimaliza utagundua niko upande gani ila tu tunatofautiana vitu vichache mi na wewe...
 
Hivi Unaweza Ongelea background ya mtu Humjui? Jibu hoja co kumtetea huyo BIBI.

Kumbe jide ni nyanya yako?sasa mbona haumpi sapoti mama ya mama yako.mi najua siku zote mtoto anapakatwa na viganja vya bibi ila wewe unavivunja sio vizuri utapata laana bure.
 
.....sijui bana... isije tu tukawa tunasahau tulikotoka...

Jidde ukifulia mie simo... wa leo wa kesho
 
Hawa Barnaba na Linah wamehama kwa Ruge?


Linah na Barnaba wameiambia Bongo5 kuwa hawatakuwepo kwenye show ya miaka 13 ya muziki ya Lady Jaydee itakayofanyika May 31, kwa kile walichodai ni kutoafikiana kwenye malipo.

Wamesema licha ya kuendelea kuwepo kwa majina yao kwenye poster ya show hiyo, hawatotumbuiza siku hiyo.
“Dada yetu alituita, akatuambia kwamba ana kazi yake ya kutumiza miaka 13 kwahiyo akawa anasema anahitaji wasanii ambao watamsupport kwaajili ya kufanya show,” amesema Linah. “Sisi tulifuata protocol zote kwasababu kama wasanii tuna viongozi, tukafuata protocol zote kuweza kukubaliana naye mpaka tukafikia hatua kwenye masuala ya biashara, yaani malipo. Kwenye upande huo kidogo tukawa tumepishana, kwenye upande wa masuala ya maslahi. Lakini sasa tunashangaa yeye kuanza kuweka posters.”
Kwa upande wake Barnaba amesema hawajashindwana na Lady Jaydee lakini wao kama wasanii wana menejementi na matakwa ya ofisi zao na hivyo muafaka ulishindwa kufikiwa na pia walikuwa na booking zingine.
Hata hivyo Barnaba amesema hakuna ugomvi wowote baina yao na Lady Jaydee. “Tuko safi tu na dada, mbona tuliafikiana vizuri tu na tuko kwenye maongezi mazuri tu, tulishaongea na hili suala liko vizuri,” amesema Barnaba.
 
mkuu unajishusha sana kutetea redio inayoshabikia na watangazaji wake kujiusisha moja kwa moja na mapenzi ya jinsia moja...


Matumbo ntake radhi mkuu...
Hebu nioneshe mahali ambapo nineisifia Clouds au mahali nimemtetea Ruge na Kusaga...
mimi siisikilizi redio Clouds, mimi nina chuki za wazi kwa Kusaga na Ruge.

Lakini naomba ieleweke kuwa siwezi kuzidisha chuki kwa ishu isiokuwa na uthibitisho.
 


hivi ndo navyotaka mimi.
Mbivu na mbichi tuzijue na si kutoa mipovu na kushutumu watu huku mmesikiliza malalamiko ya upande mmoja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…