Si ajabu hata uchaguzi wa mitaa TU mnaandikisha watoto. Punguzeni ujinga uliopitiliza.
Wewe ndio mpubavu na mavi kabisa.
Mtaani wetu wanafahamiana mnashinda kudhibiti uhuni mnakuja kulia lia Yutube .Mamaammaeee.
Mfano mna vijana mia mtaani na mnajua kabisa nyie ndio wengi kanatokea kamama Kamoja kanafanya uhuni mnakajua kwenye ofisi ya umma au ya kijiji au ya familia za vijana wa Frelimo mnakaangalia na kulia lia mtegemee huruma ya nani ?
Yaani tulipokuwa tunasema kuwa Mbowe ameshindwa chama siku nyingi akili yake imegota kabisa hamuani.?
Nani anayependa nyumba yake uchomwe moto ,nani anapenda ofisi yao ichomwe moto?
Nani atajitolea kupambania chama kama pesa zote zinaishia mikononi mwa Mbowe na marafiki zake?
Unamkumbuka yule mama wa Bawacha alidhalilishwa na kutukanwa kwenye mitandao kuwa ni malaya ?
Mama wa watu alisema kuwa ametekwa na kupigwa lakini hakuna kiongozi wa chama aliyehangaika kumtafutia wakili wala kufuatilia ishu yake kisa eti amefumaniwa! Kwani fumanizi kwenye nchi hii ni kosa linaloshughulikiwa kwa kujichukulia sheria mikononi?
Vijana wengi wanausezo wa kujitoa mhanga kudhibiti uhuni wote kokote hata katikati ya Vifaru vya kivita alimradi waone haki inatendeka na familia zao zinabaki salama lakini bado Mbowe anashindwa kutumia nguvu ya umma kwa kupeleka fedha kwenye mikono ya umma badala ya kukaa nazo yeye kama bepari.
Bepari kamwe haliwezi kuleta mabadiliko kwa wanyonge zaidi ya kuangalia maslahi ya kibepari.
Kwa Taarifa yako kati ya Samia na Lisu aliyetishio kwa Mabepari akiwemo Mbowe ni Lisu hivyo usitegemee mabadiliko kwa kumtegemea Mbowe. Sahau kabisa.
Kauli ya Askofu Shoo ni kauli pendwa ya Mbowe sio kauli ya bahati mbaya.
Mabepari siku zote fursa yao ni wanyonge kuteseka watauza mpaka maiti. Mabepari kila tatizo kwao ni fursa. Yaani watu wakiugua sana watauza sana dawa na kufungua maduka ya dawa. Watu wakifa sana watasafrisha sana maiti na majeneza na watajenga mochwari za kulipia .
Mafuta yakipanda bei na watu wakashindwa kununua mafuta wao watanunua mabasi kwa ajili ya kusafirisha abiria.
Bandari ikiuzwa watainunua.
Mtaji mkubwa wa Mabepari akiwemo Mbowe ni utawala legelege na wa kifisadi usioweza kudhibiti rushwa kubwa na matumizi ya serikali .
Kwa Afrika bado sana huwezi kuondoa ufisadi kwa kurembua . Ukitumia sheria kali kulinda mali za umma lazima Mabepari akiwemo Mbowe watalia kwa sauti ya mbwa koko.
Tuliwaambia mnasema eti tuna roho mbaya na wivu ila matokeo ya uovu wa Mabepari kufifisha maendeleo endelevu na demokrasi ya kweli.
Haiwezekani kujenga chama cha siasa kwa kumtegemea mtu mmoja mwenye pesa badala ya kujenga mfumo unaopatikana kwa nguvu ya umma wenyewe .
Tuliwaambia miaka mingi kuwa pesa za Ruzuku mjenge ofisi za chama kuanzia ngazi za msingi ,mkamwamini Mbowe na stori zake kuwa anajenga falsafa kwenye mioyo ya watu bila kujua kuwa wanachama wengi wa Chadema walitokea NCCR mageuzi na CCM na waliondoka kwa sababu moja tu ya Rushwa na ufisadi ndani ya serikali ya CCM. Sasa Mtu asiye na nia thabiti ya kupinga ufisadi kamwe hawezi kuingia kwenye mioyo ya watanganyika. Ndio maana Dr. SLAA alikua anaitisha maandamano na watu wanakwenda Mbele bila kuogopa risasi hata kuawa. Leo wetu ni waoga hata kutoka na kukimbia hawawezi ,wewe unaona ni jambo la kawaida eti watanzania ni waoga .!!!
Hakuna mtu muoga ,wafu wangekua waoga ufisadi usingekuwepo ?
Watu wanauana na kutoana makafara kwa sababu ya kutafuta pesa ,chama kisicho na mfumo wa kupeleka pesa kwa umma kamwe hakiwezi kuingia madarakani kwa nguvu ya umma.
Umma kuchoka utajitenga na siasa na sio kujitoa kuandamana kwa ajili ya wanasiasa wabinafsi.
Umma unaangalia nia thabiti ya kiongozi na walioko juu kisha unakua tayari kwa lolote.
Kama unabisha fuatilia uone jinsi watu wanavyoipenda yanga kwa sasa ,wako tayari hata kupoteza maisha alimradi timu yao isihujumiwe. Timu ikifanya vibaya hakuna mtu anajitoa kwa ajili ya timu hiyo . Kwa hiyo kama Chadema na viongozi wake wangekua wanarudisha nguvu ya chama kwa umma na kufanya kama umma unavyotaka kupambana na ufisadi leo huo huu ujinga wa watu wa dogo kabisa kuvuruga uchaguzi wa serikali za mitaa usingekuwepo.
Mbowe alipaswa Aachie ngazi mara tu baada ya Lowasa kukosa urais lakini badala yake amekua aliwatumia vijana wake kumtukana Dr.Slaa na Wale waliokimbilia CCM .
Mbowe akishupaza shingo basi chama kitapoteza kabisa kwa sababu wananchi hawana imani na Chadema chini ya Mbowe na Serikali ya CCM chini ya Dr.Samia.
Huisheni chama kwa kuweka sura mpya kabla ya uchaguzi mkuu . Mnasema Mbowe atawavusha wakati mnapoteza kwa figisu kila kukicha na hamna watu wa kupambana na wizi na figisu mpaka seikali za mitaa. Sasa huo ukubwa wa chama uko wapi ?
Tulitegemea magereza yote yajae vijana wa Chadema kwa Malaki lakini Wanaovuruga uchaguzi wawe wametiwa adabu . Na baada ya uchaguzi CCM wangeomba poo na 2025 uchaguzi ungekua wa huru zaidi na nuru ingekua inaanza kuonekana.
Hivi magereza yanaweza kuwatosha vijana mil. moja kwa muda mfupi?
Wakati huo huo CCM ingekua inaelekezwa kibla kabla ya 2025 hivyo hata wangekua na kesi ngapi wangetoka miaka michache ijayo na Chadema ingekua madarakani na familia nyingi kulipwa fidia na waliosababisha mateso wangekwenda gerezani.
Nani anafifisha harakati za kweli za Chadema kushika dola kama sio mbowe kwa kupenda umaarufu peke yake . Lisu alianza vizuri na Msigwa kufanya mikutano ,Genge la Mbowe likaona wivu kuwa hawa wawili wanaagenda ya kuchukua kiti ,matokeo yake Lisu akazuiwa kuendelea na mikutano . Msigwa kwa hasira akakimbila CCM.