Kina nani hawakupinga misaada ya kigeni kabla ili kutaka kujitegemea?

Kina nani hawakupinga misaada ya kigeni kabla ili kutaka kujitegemea?

mkuu tuelewane kdg..hata mimi napenda tanzania tuache habar ya misaada ili tujenge msingi mzuri wa kujitegemea na kuondo foreign influence kwe mambo yetu..ila mi nashangaa watu wanataka kuficha sababu ya sisi kusitishiwa misaada ni nini badala yake wanadandia ooh inabidi tujitegemee misaada haina maana..kabla hatujafika huko kwanza tumezikosa hz pesa kwasababu ya mambo yaliotajwa.......tuache misaada sawa ila sio tusitishiwe misaada kwa vikashfa flan tutofautishe hapo mkuu..haijalishi rais ni nani..lets say yalitokea lets say tusitishiwe misaada kisa yalitokea mauaji ya halaiki halafu c tujisifu eti hatutaki kuwa tegemezi noo...km tumeamua kutopokea hapo sawa ila sio tusipokee kisa tumepiga blanda flani
Hizo unazoziita kashfa zimejadiliwa sana humu na zimetolewa sana ufafanuzi lakini sababu ya mihemko ya mahaba ya kivyama hakuna anayekubaliana na mawazo ya mwenzie.
Sababu ya kwanza ni kunyimwa msaada huu ni kutoridhishwa ni jinsi ulivyoshughulikiwa mgogoro wa uchaguzi wa Zanzibar na kurudiwa kwa uchaguzi huo ambao haukuwa shirikishi. Mtanzania gani leo ni kipofu wa juhudi zilizofanywa kushughulikia mgogoro huu? Yale mazungumzo ya kutafuta muafaka haikuwa juhudi ya kushughulikia tatizo? aliyekwamisha mazungumzo yale alikuwa nani aliyeenda Serena Hotel na kutangaza hana shida ya maridhiano? Kurudiwa kwa uchaguzi ni matokeo ya mtu kudanganywa ajitoe katika mazungumzo kuna mataifa yatakuunga mkono huo ni utumwa wa kifikra katika siasa za Kiafrika. Marekani wenyewe waliwahi kufuta matokeo ya Jimbo zima la Texas sababu ya utata wa utoboaji wa karatasi za kupigia kura yaliyoelekea kumpa ushindi mmoja wa wagombea katika uchaguzi uliokuwa huru na wa haki.

Madai mengine ya kijinga ni ya uchaguzi kutokuwa shirikishi. Ushirikishi kwa wenzetu hawa ni kulazimisha wale walioamua kwa hiari yao kutoshiriki washiriki. leo hawaamini mtu kuamua kushiriki au kutoshiriki mchakato wa uchaguzi nayo ni Demokrasia. Na wanaoshangilia uamuzi huu wa MCC ni wale waliokuwa wakilalamika wasilazimishwe kushiriki kitu ambacho wao hawakitaki. sijui walitaka nchi ikae bila Rais kwa muda gani mpaka hapo wanaotaka kubembelezwa kushiriki wajisikie sasa wanataka kushiriki.

Suala la Cyber crime law ni la taratibu na sheria za kibunge zaidi, Serikali ilishatoa maelezo kama kuna mapungufu katika sheria ile mapendekezo ya marekebisho yanatakiwa kupitia katika taratibu za kawaida za kibunge. Sasa mtu utashangaa walitaka uchaguzi uahirishwe mpaka marekebisho hayo yafanyike? na yangefanywa na chombo gani hali kuwa muda wa wawakilishi wetu umeisha? Hivi tufikirie kana Watanzania mswada ule ungalikuwa haujapitishwa, uchaguzi wa 2015 ungalikuwaje ukizingatia uhuni na uchochezi uliokuwa ukifanywa kupitia mtandao? kama ilifikia waharifu wa mtandao kuaminisha kuwa sasa nchi haina mkuu wa majeshi ati amekufa, lengo lilikuwa nini? Ukizingatia na wageni walioletwa kusaidia baadhi ya vyama kitekinologia kujaribu kuharibu matokeo Ni lazima tukubali hii sheria imesaidia sana uchaguzi huu kuwa wa Amani kama si hivyo kungalitokea machafuko makubwa.
 
Mkuu Mwanakijiji, don't be disingenuous please! Unafahamu fika (unless you have been infected with the "CCM" disease) kwamba kinachowasukuma Watanzania wengi kufurahia huu uamuzi wa MCC siyo suala la sisi kunyimwa huo msaada. In fact, nadiriki kusema Watanzania wengi wana chuki dhidi ya dhana ya sisi kutegemea misaada - wanachama wa CCM na hata Wapinzani wengi tu. Issue hapa ni sababu za sisi kunyimwa misaada. Be truthful and tell us if you truly believe CCM didn't commit foul in the Zanzibar election saga, and deserve MCC's rulling. Tell us if you really think the Cyber Security law passed by CCM is not undemocratic, to say the least. Come on Brother! You used to be my model!

Mbona nimeshajieleza huko nyuma; suala la Cybercrime Law ni jambo la aibu hata kufikiria; hivi ni kuulize hii sheria ilipitishwa lini? Na kwanini Wamarekani hawakuipinga kivile; wakati mimi nilikuwa mtu wa kwanza kutoa angalizo dhidi ya ujio wa sheria hii na madhara yake miaka mitatu kabla hata haijapitishwa na wengine kudandia kuanza kuipinga? Zanzibar ilichezwa faulu bila ya shaka, tatizo ni kuwa wengi wanaamini waliocheza faulo hiyo walikuwa CCM peke yake.
 
Kwani hao bibi na babu yako wameanza kuishi kijijini mwaka huu? Miaka yote umewafikiria kwa misaada what happened?
Process za misaada zilikuwa in progress. Ila sasa misaada imeshazuiwa so kufikiwa ni vigumu sana
 
1. Ni nani anayelalamika kuhusu kurugwa kwa uchaguzi?
2. Je, ni kweli Jecha alichukuliwa na 'vyombo' au si kweli?
3. Je, kuna kumbu kumbu za kikao cha tume kuhusu kufutwa uchaguzi?
4. Je, ni dai au madai gani yaliyoelezwa na tume a.k.a Jecha?
5. Sheria gani ya ZNZ inayosema tume inaweza kufuta uchaguzi wote?
6. Ni sharia gani ya ZNZ inayoeleza kuhusu uchaguzi wa marudio?

Hapa hatuongeleI CUF, CCM au UKAWA. Tunaongelea tu taratibu ziliztumika

Mimi jibu langu - na haya ni mawazo yangu tu:

Kilichotokea Zanzibar kilikuwa kitu kinachosimamiwa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar. Ni mambo yanayohusiana na Zanzibar na kama baadhi yetu tulivyoonesha wakati ule kuwa ni suala la Zanzibar na tume yao wala halihusiana na Tume ya Uchaguzi ya Taifa wala matokeo ya Uchaguzi wa taifa.

Tarehe ile ya 28 Oktoba mimi niliandika mada hii kuelezea mawazo yangu siku ile. Baadhi ya maswali yako yanajibika mle. Nitajinukuu kidogo tu na naamini hatuko mbali kifikra katika hili.

Juu ya Jecha na kufuta uchaguzi:

the only grave issue here is the authority of NEC or its chairman to nullify the whole election based on some irregularities that could have been dealt with otherwise. As I read Chairman Jecha?s letter to announce his decision I found nowhere in it where the chairman argued a point of law to defend his decision. He didn?t mention a single law to show that indeed he has the power to nullify the law. This does not mean he doesn?t or that NEC doesn?t have that authority. This means then that this question cannot be settled by politicians who would benefit either way with the decision. This issue should be sorted and settled in a court of law immediately. Everything else stands or falls on this point.

Nikaeleza tena kidogo kuwa:

What most people probably missed in Jecha?s reasoning for the cancellation of the Presidential results is the inference on who is responsible for meddling with the election process. If we were to believe his points of irregularities the whole mess started in Pemba. Point 2, 3, 4, 7 and 9 in his letter clearly accuse (not by mentioning names) that CUF which has an overwhelming presence in Pemba for interfering with the process. This was capped up with Seif declaring himself a winner and thus putting ZEC in crossfire. There was no way out for ZEC; declare Seif the winner and thus ignore those issues raised in points 2, 3, 4, 7 and 9 in his letter to the wrath of the ruling party or declare Shein the winner and ignore Seif?s allegations. To be between the rock and the hard place would have been a better than this position. He chose the way out ? nullify the whole process to the anger of probably both.

Nikatoa wito kuwa:

As I have said above the issue of ZEC power to nullify election is the fundamental one to be dealt here and as a matter of fact urgently.

Sasa, sijui kwanini unaweza kudhania kuwa sijajali sana hoja hii nzito ya masuala hayo. Lakini niliamini wakati ule na nikatoa neno la hekima tu kuwa:


Last note is that this issue is a Tanzanian issue and I believe with all the deficiencies we have in our legal system we still are capable of addressing them. Foreign entities should not be allowed to put undue pressure on the country. This is a very delicate time and we should expect our friends to refrain from inflaming the wounded sentiments of our people. They should be wise to let the Tanzanian people sort these things on their own.
 
Nimegundua watanzania tunahitaji maombi maalumu kama hamtaki misaada mbona msaada Wa japani juzi mmepokea
Kwani umesikia Serikali ya Tanzania imesema haitaki misaada? au una changanya kauli ya mtu wa kawaida kama mimi kuwa ni msimamo rasmi wa serikali. Serikali yetu bado ni ombaomba na inategemea misaada. Haijawahi kukataa misaada - kama principle.
 
WanaCCM tumeshaeleza wazi kuwa hatuna shida na vijimisaada vyenye masharti. Hili hata mstaafu Kikwete alilizungumza na sasa rais Dkt Magufuli anazidi kulikazia.

HAMY D, please nakuomba uache kuingiza ukada katika mambo serious!
Fallacy of generalization, hicho ndio unachokifanya, kwa kujua au kutokujua hilo unafahamu wewe, HII NCHI SI YA WANACCM PEKEE, kuwa makini na kauli zako ndugu, hili jambo ebu litazame kwa upana zaidi, kama hauwezi acha wenye weredi wachangie, please!
 
Kwani MCC ilianzishwa mwaka gani?
Hata hivyo CCM ipo kwenye position nzuri sana kujibu hilo swali lako la msingi.... kwamba kwa miaka 55 tumeshindwa kujitegemea, leo kwa kunyimwa misaada kwa ulafi wa madaraka mnakuja na drama za uzalendo na blabla...kujitegemea bila viwanda, umeme wa uhakika na uzalishaji wa kibiashara umeona wapi mkuu
CCM wapuuzi kweli ,siku zote nchi ikiingia kwenye crisis ndio inacheza karata ya uzalendo . Tunasema hivi tunashukuru wahisani kuzuia misaada na tunaomba waliosalia nao wazuie misaada. Tupo tayari kuvumilia machungu ya muda mfupi kuikuza tamaduni ya demokrasia nchini.
 
Kwa upeo wangu mdogo nadhani kuna baadhi ya mambo huwa yanaflowa kwa kutegemeana always!!
Binafsi nadhani kujitegemea katika nyanja za kiuchumi na kijamii lazima kuendane na uwepo wa utawala bora, hii ni pamoja na kuheshimu demokrasia pamoja na uhuru wa vyombo vya habari.
Hatuwezi kuwa na maendeleo yenye tija kama hatuna demokrasia, mfano ni yanayoendelea sasa Zanzibar, shughuli za uzalishaji na biashara zimedolola, tunaendelea vipa katika mazingira kama haya?! Watu hawafanyi kazi kwa hofu ya majeshi na polisi kutanda mitaani, watu hawafanyi kazi kwasababu hata general happiness ya watu imeshuka mno (kumbuka video ya wale watu wanaolia ndani ya nyumba ya ibada ambayo imezagaa kwenye mitandao) people produce more when they are happy!!

Hivyo basi tunapozungumzia kujitegemea tulizungumzie na hili la demokrasia.

Binafsi nadhani tukifaulu hapa basi njia ni nyeupe kuyafikia maendeleo endelevu, siasa za ushindani wa kweli na haki ni chachu ya maendeleo.
 
Mirisho umeongea neno la maana, umemuuliza mwanakijiji maswali ya maana, Ngoja na mie nimuulize swali langu, hapa tatizo sio msaada tatizo hata ile miradi waliotusaidia tumeshindwa kuiendeleza au kuitunza, mfano mdogo tuu ni hii barabara ya mwendo kasi imejengwa kwa ghaarama kubwa tena kwa pesa za mkopo leo barabara imegeuka kuwa dampo la takataka, kuanzia manzese tiptop mpaka mwembe chai nje ya ofisi za finka, sie waafrika tuna bahati mbaya sana na haya mambo sana sana yanatokea tanzania tuu, tuna vyanzo vya kila aina vya kutufanya tuwe nchii tajiri, kuanzia ardhi,mito,maziwa,madini ,gas na hali ya hewa nzuri ila mpaka leo kuna sehemu ya tanzania watu wanakula mizizi, la msingi mcc wamesema hawajaridhika na marudio ya uchaguzi zanzibar na sheria ya mtandao na haya waliyazungumzia before ila nashangaa mwanakijiji anazungumzia tiba kuliko kuzuia au kuondoa sababu ambazo wakubwa wetu wamezitaja hata kama utapenda neno wakubwa ila ukweli ndio huo wale jamaa wakubwa mno na wewe unajua hilo, kumbe mnapita huko vijijini kuahidi maji na umeme kumbe na nyie wenyewe uwezo hamna mnategemea kwenda kuomba aibu ilioje.
 
CCM wapuuzi kweli ,siku zote nchi ikiingia kwenye crisis ndio inacheza karata ya uzalendo . Tunasema hivi tunashukuru wahisani kuzuia misaada na tunaomba waliosalia nao wazuie misaada. Tupo tayari kuvumilia machungu ya muda mfupi kuikuza tamaduni ya demokrasia nchini.

Yaani neno UZALENDO nadhani wanasiasa wanalitumia vibaya mno! Kiukweli sijawai ona uzalendo kwa mwanasiasa yoyote yule. Ni neno lao pendwa sana inapokuja katika swala kuhalisha uovu flani.
 
Kwa upeo wangu mdogo nadhani kuna baadhi ya mambo huwa yanaflowa kwa kutegemeana always!!
Binafsi nadhani kujitegemea katika nyanja za kiuchumi na kijamii lazima kuendane na uwepo wa utawala bora, hii ni pamoja na kuheshimu demokrasia pamoja na uhuru wa vyombo vya habari.
Hatuwezi kuwa na maendeleo yenye tija kama hatuna demokrasia, mfano ni yanayoendelea sasa Zanzibar, shughuli za uzalishaji na biashara zimedolola, tunaendelea vipa katika mazingira kama haya?! Watu hawafanyi kazi kwa hofu ya majeshi na polisi kutanda mitaani, watu hawafanyi kazi kwasababu hata general happiness ya watu imeshuka mno (kumbuka video ya wale watu wanaolia ndani ya nyumba ya ibada ambayo imezagaa kwenye mitandao) people produce more when they are happy!!

Hivyo basi tunapozungumzia kujitegemea tulizungumzie na hili la demokrasia.

Binafsi nadhani tukifaulu hapa basi njia ni nyeupe kuyafikia maendeleo endelevu, siasa za ushindani wa kweli na haki ni chachu ya maendeleo.
Tatizo ni sisi Watanzania Bara kujifanya tunajua sana yanayotokea Zanzibar kuliko Wa Zanzibari wenyewe, Atii shughuli za uzalishaji zimesimama, mara zimedorola, kwa taarifa taarifa Zanzibar ilisimama pale Seif alipojitangazia ushindi, hofu ilitanda kote na watu kujifungia ndani. Jecha alinusuri hali ile baada ya kufuta matokeo watu wakarejea mitaani.

Mapicha na video za mitandaoni qmbqao ni propaganda za kugushi haiwezi kuwa kigezo cha kudai kuwa Zanzibar hakuna Amani, na hapa niseme ndiyo umuhimu Cybercrime Law inatakiwa ifanye kazi kweli, Bahati yao wawekao picha nq video hizo, JF wamefungua kesi Mahakama kuu kupinga kutii amri ya serikali ya kutoa taarifa ya vyanzo vya taarifa kwenye mtanzano wake. Lakini ni ukweli matukio ya eneo jingine yanawekwa ili kuonyesha ni hali ilivyo sasa Zanzibar moja ni hiyo video unayo zungumzia ambayo ni tukio la Tanzania Bara la vurugu miaka ya nyuma Waumini walioijifungia pale msikiti wa Mwembechai wakiamini askari hawataingia.
 
Tatizo ni sisi Watanzania Bara kujifanya tunajua sana yanayotokea Zanzibar kuliko Wa Zanzibari wenyewe, Atii shughuli za uzalishaji zimesimama, mara zimedorola, kwa taarifa taarifa Zanzibar ilisimama pale Seif alipojitangazia ushindi, hofu ilitanda kote na watu kujifungia ndani. Jecha alinusuri hali ile baada ya kufuta matokeo watu wakarejea mitaani.

Mapicha na video za mitandaoni qmbqao ni propaganda za kugushi haiwezi kuwa kigezo cha kudai kuwa Zanzibar hakuna Amani, na hapa niseme ndiyo umuhimu Cybercrime Law inatakiwa ifanye kazi kweli, Bahati yao wawekao picha nq video hizo, JF wamefungua kesi Mahakama kuu kupinga kutii amri ya serikali ya kutoa taarifa ya vyanzo vya taarifa kwenye mtanzano wake. Lakini ni ukweli matukio ya eneo jingine yanawekwa ili kuonyesha ni hali ilivyo sasa Zanzibar moja ni hiyo video unayo zungumzia ambayo ni tukio la Tanzania Bara la vurugu miaka ya nyuma Waumini walioijifungia pale msikiti wa Mwembechai wakiamini askari hawataingia.

Niko kibandamaiti hapa!! Nakijua ninachoongea.
 
Jamani hakuna waombaji humu?
Huyu mtu anahitaji kuombewa!

Itabidi tuwaombe Moderator wamsaidie kumrudishia account yake ile heshima aliyojiwekea humu na heshima ya Jf kupitia kwake Mzee Mwanakijiji irudi maana hakuna namna huyu si yeye naanza kuamini ni mshumbushi kama alivyoharibu account ya Dr kwa kutupia mipasho!
 
Sintashangaa ukiwa miongoni mwa wale sababu account yako yenyewe ya march, 2016 sijui hii ni ya ngapi umefungua kwa kazi hiyo.

Maniac!!! Sibishani na watu wasiokuwa na akili! Niko jf kitambo sana, acc yangu ya kwanza nimeiacha baada ya kupoteza device! Amini unachotaka kuamini empty head.
 
Sintashangaa ukiwa miongoni mwa wale sababu account yako yenyewe ya march, 2016 sijui hii ni ya ngapi umefungua kwa kazi hiyo.

Kama umeshindwa kuiona logic ya ninachokizungumzia basi wewe sio size yangu katika marumbano ya aina yoyote ile, wewe ni bure kabisa kichwani!
 
Kama umeshindwa kuiona logic ya ninachokizungumzia basi wewe sio size yangu katika marumbano ya aina yoyote ile, wewe ni bure kabisa kichwani!
Na mimi nisingependa kubishana na wewe, sababu nisije kuonekana kama wewe.
 
Tangu nimezaliwa ndio leo nasikia Device kupotea na account ya mtu, when a devil is exposed you will see on how he react.
 
Back
Top Bottom