flyn rider
JF-Expert Member
- Sep 24, 2013
- 456
- 78
mkuu samahani kutoka nje ya mada, nilitaka kufahamu ukimaliza kozi za agriculture engineering na irrigation and water resources engineering unapangiwa kazi na serikali au unatafuta mwenyewe?????
Kujituma ni suala binafsi kati ya mtu na mtu,mfano wafanyakazi wawili waliosoma UDSM mmoja akajituma na wa pili akawa hajitumi na ni kozi moja wamesoma.Nachofahamu ubora wa chuo ni pamoja na products zinazotoka. Wanafunzi wengi wa SUA, ni bora na wanajituma sana wakiwa makazini ukilinganisha na kutoka vyuo vingine.
Hii inatokana na ubora wa elimu inayotolewa katika chuo kile. Mwanafunzi GOIGOI akienda pale hata Semester moja hamalizi.
Najua siwezi pata shida kuwashawishi watu kwamba UDSM ni bora kuliko Mzumbe; lakini naweza hata kutupiwa mawe kujaribu kuwaambia wadau kwamba SUA ni bora kuliko Mzumbe! Kwavile ni ngumu kuwashawishi watu (sio wana JF pekee; bali hata wale walio nje ya JF) kuamini kwamba SUA ni bora kuliko Mzumbe lakini ni rahisi kuwashawishi watu kwamba UDSM ni bora kuliko Mzumbe; basi ni bora nikaijadili Mzumbe na SUA!
Nilijaribu kutafakari uwepo wa idadi kubwa maradufu ya wahadhiri wenye PhD ukilinganisha na wale wenye Masters! Kwa mtizamo wangu, nimeona mambo mawili yamechangia SUA kuwa na PhD holders wengi. Kwanza, kuna kila dalili kwamba wale waliokuwa wanasoma shahada zao za kwanza (ambazo nyingi zake enzi hizo ni za Kilimo) walikuwa hawataki kufanya kazi zinazoendana na fani yao! Kama si hivyo, basi inawezekana kabisa hata hizo ajira zenyewe kwao kupata ilikuwa shida kwavile hatukuwa na kilimo cha ku-accomodate graduates! Kwahiyo si ajabu, wengi wao walikuwa wana-opt kurudi tena darasani na kuchukua Masters na PhD! Sababu nyingine ni kwamba, I guess wafadhili wengi walipendelea zaidi kuisaidia TZ kwenye suala zima la maendeleo ya kilimo, hivyo hii iliwapatia graduates wa SUA kupata scholarship kirahisi kwenda nje ya nchi kusoma!
Likewise, SUA wana some monopoly power kutokana na kuwa the sole agricultural university in TZ! Hivyo basi, msomi yeyote wa kilimo na forestry anaye-opt kuwa lecturer atakuwa hana option(otherwise, ata-enjoy limited option) zaidi ya kwenda SUA! Hii nayo ina-play kama comparative advantage kwa SUA kuweza kuhodhi idadi kubwa ya wasomi wa aina yake tofauti na wasomi wa fani zingine!
Kwanini Mzumbe ni maarufu mno kuliko SUA?! Jibu lake ni jepesi mno! Program za asili pale Mzumbe ni za wapiga domo(Wanasiasa)! Wengi wao ni wale waliosomea masomo ya arts ambao kwa asili ni wapiga domo! Na ndio maana hadi leo hii endapo watu tutaulizwa ni wasomi gani wanatoka UDSM, basi wengi wetu tutawataja wale wanaotoka departments za History, Political Science na Law kwavile ndio pekee wanaopenda kuuza sura kwenye TV na vyombo vingine vya habari! Ni nani anaweza kututajia wasomi toka Faculty of Engineering ya UDSM? Kuna ma-PhD holders kibao lakini hawafahamiki! Ni nani anaweza kututajia wasomi wa Muhimbili University? Ni nani anaweza kututajia wasomi wa Ardhi University? Ni wa-TZ wangapi wanafahamu juu ya kuwepo kwa Muhimbili na Ardhi ya University? Nature ya taaluma zao si za kupiga domo! Leo hii Ikulu ikilipuliwa, Profesa Baregu au Profesa Xavery watakaa chonjo kusubiria mwaliko wa vyombo vya habari ili wahojiwe na wao kutoa maoni yao jambo ambalo halitatokea kwa ma-profesa wa ama SUA, Ardhi au Muhimbili!