Kinacholitesa Taifa kwa sasa ni watu kuwekeza kwa mtu na sio kuwekeza kwa Taifa

polokwane

JF-Expert Member
Joined
Dec 16, 2018
Posts
3,361
Reaction score
5,842
Hiki ndicho kinacho litesa sana taifa kwa sasa na itachukua muda kidogo kwa taifa kuondokana na tatizo hili na kuzifuta element hizi.

Hii haikuwa legacy nzuri ambayo JPM ameliachia taifa na ndicho kinacho leta shida kwa sasa kwa wananchi hata sasa bungeni.

Kuna haja kama taifa kutengeza mfumo ambao Rais atakuwa anawajibika kama taasisi na si kuwajibika kama mtu binafsi ili kuondokana na watu kuwa na uzalendo kwa mtu badala ya taifa.
 
Na angetawala milele, haki ya nani baadhi ya sisi raia wenye akili timamu, tungeishi maisha magumu sana! Ilifikia wakati kila kitu kikifanyika hata kama ni cha kawaida kiasi gani, pongezi zote zilienda kwa Mheshimiwa Rais Dokta John Pombe Joseph Magufuli!

Mungu Mkubwa aisee!!
 
Exactly

Huko ndoko tulikokuwa tunaenda kama Taifa, kuwa na The Life President ndani ya nchi yetu na kinyume kabisa na Katiba yetu ya nchi
 
Hivi jaffo yupo?Mzee wa kila mradi unapewa jina magufuli
 
Kwakweli MAGUFULI alitengeneza legacy ya hovyo sana sana na mama samia ana kaxi kubwa sana kuondosha huu ujinga kwanza

Maana watu wameaminishwa kwamba hakuna Rais apaswaye kuambudiwa isipokuwa magufuli
 
Kinacholitesa Taifa letu ni kutokuwa na chaguzi huru na za haki. Na cha kuondoa mateso haya ni Katiba mpya ya rasimu ya Warioba na Tume huru ya uchaguzi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…