BestOfMyKind
JF-Expert Member
- Apr 26, 2012
- 1,350
- 1,464
Kinachoniuma mimi ni hela za jasho langu ndizo zinazowapa utajiri wanasiasa.
Yaani mavazi ya raisi, safari za nje za raisi, magari ya wabunge na mishahara ya wabunge vyote ni jasho la wananchi.
Lakini kama hiyo haitoshi, tumeongezewa kodi na tozo nyingine ambazo nazo zitaliwa na wanasiasa.
Wanasiasa hamuoni aibu kula jasho la wananchi masikini?
Magufuli alijua sisi ni masikini na ndio maana alipunguza tozo na kutumia rasilimali za taifa kupata hela.
Kwanini mnaogopa kutumia rasilimali zetu kupata hela?
Yaani misaada yote inayokuja nchini hakuna hata mmoja unaoenda kulipa mishahara mikubwa ya wanasiasa, gharama zote hizo za mishahara ya wabunge zaidi ya 270 inalipwa na kodi za wananchi.
Bado hamtosheki mnaona hamjatukamua vizuri.
Kama una kula hela ya mwananchi kuwa na ujasiri wa kupambana na makampuni makubwa yanayotunyonya kwenye mikataba ya madini.
Uoga wa viongozi wetu ni hatari kwa usalama wa taifa letu.
Mtaondolewa madarakani kwa mapinduzi, kila uvumilivu una kikomo chake.
Yaani mavazi ya raisi, safari za nje za raisi, magari ya wabunge na mishahara ya wabunge vyote ni jasho la wananchi.
Lakini kama hiyo haitoshi, tumeongezewa kodi na tozo nyingine ambazo nazo zitaliwa na wanasiasa.
Wanasiasa hamuoni aibu kula jasho la wananchi masikini?
Magufuli alijua sisi ni masikini na ndio maana alipunguza tozo na kutumia rasilimali za taifa kupata hela.
Kwanini mnaogopa kutumia rasilimali zetu kupata hela?
Yaani misaada yote inayokuja nchini hakuna hata mmoja unaoenda kulipa mishahara mikubwa ya wanasiasa, gharama zote hizo za mishahara ya wabunge zaidi ya 270 inalipwa na kodi za wananchi.
Bado hamtosheki mnaona hamjatukamua vizuri.
Kama una kula hela ya mwananchi kuwa na ujasiri wa kupambana na makampuni makubwa yanayotunyonya kwenye mikataba ya madini.
Uoga wa viongozi wetu ni hatari kwa usalama wa taifa letu.
Mtaondolewa madarakani kwa mapinduzi, kila uvumilivu una kikomo chake.