Kinachoniuma mimi Mwananchi ni jasho langu kuwatajirisha wanasiasa

Kinachoniuma mimi Mwananchi ni jasho langu kuwatajirisha wanasiasa

BestOfMyKind

JF-Expert Member
Joined
Apr 26, 2012
Posts
1,350
Reaction score
1,464
Kinachoniuma mimi ni hela za jasho langu ndizo zinazowapa utajiri wanasiasa.

Yaani mavazi ya raisi, safari za nje za raisi, magari ya wabunge na mishahara ya wabunge vyote ni jasho la wananchi.

Lakini kama hiyo haitoshi, tumeongezewa kodi na tozo nyingine ambazo nazo zitaliwa na wanasiasa.

Wanasiasa hamuoni aibu kula jasho la wananchi masikini?

Magufuli alijua sisi ni masikini na ndio maana alipunguza tozo na kutumia rasilimali za taifa kupata hela.

Kwanini mnaogopa kutumia rasilimali zetu kupata hela?

Yaani misaada yote inayokuja nchini hakuna hata mmoja unaoenda kulipa mishahara mikubwa ya wanasiasa, gharama zote hizo za mishahara ya wabunge zaidi ya 270 inalipwa na kodi za wananchi.

Bado hamtosheki mnaona hamjatukamua vizuri.

Kama una kula hela ya mwananchi kuwa na ujasiri wa kupambana na makampuni makubwa yanayotunyonya kwenye mikataba ya madini.

Uoga wa viongozi wetu ni hatari kwa usalama wa taifa letu.

Mtaondolewa madarakani kwa mapinduzi, kila uvumilivu una kikomo chake.
 
KAMA TAIFA TULIKOSEA SEHEMU MKUU NA KUREKEBISHA HILO BILA ELIMU YA KUTOSHA NA JASHO LA DAMU HAWA WATAWALA HAWATAELEWA
 
Inauma sana, miaka ya mwanzoni mwa 2000 Serikali iliondoa kodi zenye kero kama vile kodi ya kichwa, kodi ya baiskeli na kodi ya mifugo. Sasa zimeanza kurudi tena kwa jina jipya la "Tozo", Tozo zenye kero.
 
Awamu iliyopita ilikua ya maskini kujidai. Sasa awamu hii acha na matajiri nao wajidai[emoji23][emoji23]
 
tumerudi kwenye zama za matajiri kutolipa kodi.
 
Kama haupo tayari kufa kwa ajili ya wananchi bora usigombee kabisa uongozi.
 
😁😁😁
MAElFFr.jpg
 
Mwanamke hafai kuwa kiongozi hiyo ndo nature ilivyo Kama unabisha muachie mke wako aendeshe mambo hapo nyumban uone matatzo
 
Kinacho nikera mimi ni kauli za walafi wawapo majukwaani kua watanzania wahalipi kodi, ikiwa kila huduma nayo inunua VAT iko ndani yake.

Au wao walipa kodi ni wale tuu walio sajiliwa na TRA?.ki msingi hiii kauli hua inanitesa sanaaa sanaa, sielewi tatizo la kunyanyapaliwa nini nini?.
 
achana na suala langu binafsi, watanzania wote tunalipa VAT (hata watoto wa miaka 2) hizi ndo pesa za jasho ambazo zinaenda kulipa mishahara. Mimi binafsi nalipa PAYE (siweki ushahidi), nina ninalipa kodi ya makadirio kwa biashara yangu binafsi (TIN kwa ajili ya biashara), nimelipia kodi gari, nina tozo juu ya mafuta (pamoja na kodi zote hizo, ninalipa REA ambayo haijawahi kunisaidia mimi binafsi, tozo ya miamala). N.K
weka slip za malipo yako ya KOdi TRA, huu uzi unatakiwa kuenda na ushahidi
 
Kinachoniuma mimi ni hela za jasho langu ndizo zinazowapa utajiri wanasiasa.

Yaani mavazi ya raisi, safari za nje za raisi, magari ya wabunge na mishahara ya wabunge vyote ni jasho la wananchi.

Lakini kama hiyo haitoshi, tumeongezewa kodi na tozo nyingine ambazo nazo zitaliwa na wanasiasa.

Wanasiasa hamuoni aibu kula jasho la wananchi masikini?

Magufuli alijua sisi ni masikini na ndio maana alipunguza tozo na kutumia rasilimali za taifa kupata hela.

Kwanini mnaogopa kutumia rasilimali zetu kupata hela?

Yaani misaada yote inayokuja nchini hakuna hata mmoja unaoenda kulipa mishahara mikubwa ya wanasiasa, gharama zote hizo za mishahara ya wabunge zaidi ya 270 inalipwa na kodi za wananchi.

Bado hamtosheki mnaona hamjatukamua vizuri.

Kama una kula hela ya mwananchi kuwa na ujasiri wa kupambana na makampuni makubwa yanayotunyonya kwenye mikataba ya madini.

Uoga wa viongozi wetu ni hatari kwa usalama wa taifa letu.

Mtaondolewa madarakani kwa mapinduzi, kila uvumilivu una kikomo chake.
Pole Sana ndugu ndo Mana hawataki katiba mpya hawataki kuwajibika kwa Wananchi.Juwa mcumilivu kufkia 2025 Nchi hii itakua nzur Sana kwa Sababu tutakua tumepata katiba mpya na tutakua viongozi wenye maono makubwa .
 
Back
Top Bottom