SI KWELI Kinachosababisha mlevi kuyumba ni kasi ya mzunguko wa damu kuongezeka

SI KWELI Kinachosababisha mlevi kuyumba ni kasi ya mzunguko wa damu kuongezeka

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Kuna mahala nimesikia kuwa mlevi huyumba yumba kwa kuwa kasi ya mzunguko wa damu yake huwa kubwa. Hii ni kwa sababu pombe hiyo husababisha mabadiliko hayo

istockphoto-464784920-612x612.jpg

Je, ni kweli kuwa hali ya mlevi kuyumba yumba husababishwa na ongezeko la kasi ya msukumo wa damu? Na sio pombe kuathiri mishipa ya fahamu?
 
Tunachokijua
Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), pombe huathiri saikolojia na kuzalisha tabia za utegemezi. Ni kinywaji kinachotajwa na fasihi za kale kuwa kimeanza kutumika tangu zamani sana.

Hutengenezwa kwa kusindika aina fulani za fangasi, sukari au aina fulani ya wanga unaojulikana kama Starch.

Unywaji wa pombe uliopindukia husabisha zaidi ya magonjwa 200 mwilini, lakini inapotumika kwa kiasi kidogo huhusishwa na kupunguza nafasi ya kuugua magonjwa ya moyo, kiharusi na kisukari.

Kwa mujibu wa Taasisi ya Mayoclinic, unywaji mdogo wa pombe hutambulika kama;
  • Mililita 350 za bia kwa wanawake na mililita 700 kwa wanaume.
  • Mililita 148 za divai kwa wanawake na mililita 296 kwa wanaume.
  • Mililita 44 za spirit kwa wanawake na mililita 88 kwa wanaume.
Hii humaanisha kuwa kiasi tajwa cha pombe kinafaa kutumiwa ndani ya saa 24, yaani siku 1.

Kuongezeka kwa msukumo wa damu ndio sababu ya kuyumba kwa mlevi wa pombe?
JamiiForums imefuatilia madai haya kutoka vyanzo mbalimbali pamoja na kuzungumza na wataalam kadhaa wa afya.

Katika ufuatiliaji huu tumebaini mambo yafuatayo;
  1. Sio kweli kuwa kuyumba kwa mlevi husababishwa na ongezeko la msukumo wa damu kama mtoa hoja anavyodai.
  2. Kwa mujibu wa Taasisi ya Vestibular Disorders Association, pombe huharibu uwiano na ujazo wa vimiminika vinavyopatikana kwenye sikio la kati hivyo kumfanya mlevi ayumbe.
  3. Sehemu ya ubongo inayohusika na kutunza usawa wa mwili na mijongeo ya misuli hasa sehemu ya mikono na miguu maarufu kama cerebellum hupoteza udhibiti wa kazi hiyo hivyo kumfanya mtu atembee kwa kuyumba.
Pia, JamiiForums inatambua kuwa, matumizi ya baadhi ya dawa hasa zile zinazoathiri uwezo wa akili na kuleta uraibu au utegemezi, maambukizi makubwa ya sikio la kati pamoja na ajali kubwa inayohusisha sehemu ya kichwa ni baadhi ya mambo mengine yanayoweza kupoteza balansi ya mwili na kumfanya mhusika apoteze udhibiti wa mijongeo ya misuli ya mwili wake.

Hivyo, kwa kuzingatia rejea hizi, madai ya mlevi wa pombe kuyumba kwa sababu ya kuongezeka kwa msukumo wa damu yanathibitika kuwa ni uzushi usio na hoja zilizojengwa kwenye taarifa sahihi za kisayansi.
Yaani mlevi damu yake inaenda kasi kushinda mtu aliyepo uwanjani anaupiga mpira ama mwanariadha anaekimbia marathoni masaa mawili yupo njiani anaenda kwa speed ya 10+km/hr
🤔🤔

Nijuacho ni kwamba alcohol inasumbua(neno sahihi nakosa) celebrum ambayo inahusika na cordination ya misuli. Wataalam wa baiolojia wataiweka sawa hii.
 
Si kweli, sababu ni hii

Cerebellum: The cerebellum coordinates muscle movement, balance, equilibrium and muscle tone. Alcohol can affect the cerebellum by throwing off your balance, causing you to stagger and fall.
 
Si kweli. Mtu anayumba kwa sababu ubongo unashindwa kuchakata taarifa kutoka kwenye mazingira yake. Balance ya mtu inafanywa na masikio na kwa sehemu macho(Ndiyo maana mtu akifumba macho halafu umwambie atembee utaona anapepesuka--hawezi enda kwa kunyooka). Vyote hivi hupeleka taarifa kwenye ubongo ili nao uiamuru misuli iweke mwili kwenye balansi. Sasa kwa vile ubongo haufanyi kazi sawasawa, basi unashindwa kuongoza vizuri swala la balansi.
 
Kuna mahala nimesikia kuwa mlevi huyumba yumba kwa kuwa kasi ya mzunguko wa damu yake huwa kubwa. Hii ni kwa sababu pombe hiyo husababisha mabadiliko hayo


Je, ni kweli kuwa hali ya mlevi kuyumba yumba husababishwa na ongezeko la kasi ya msukumo wa damu? Na sio pombe kuathiri mishipa ya fahamu?
[/QUOTE
Mkuu vipi mtu anayezunguka halafu akisimama anahisi kizunguzungu hii nayo ni sehemu ya sikio? Nilishawahi kuusikia ILA sikuelewA?
 
Si kweli. Mtu anayumba kwa sababu ubongo unashindwa kuchakata taarifa kutoka kwenye mazingira yake. Balance ya mtu inafanywa na masikio na kwa sehemu macho(Ndiyo maana mtu akifumba macho halafu umwambie atembee utaona anapepesuka--hawezi enda kwa kunyooka). Vyote hivi hupeleka taarifa kwenye ubongo ili nao uiamuru misuli iweke mwili kwenye balansi. Sasa kwa vile ubongo haufanyi kazi sawasawa, basi unashindwa kuongoza vizuri swala la balansi.
Fact
 
pombe inafyonza maji na oxygen kwenye ubongo hio inapelekea ubongo kukosa maelewano ndo kulewa kwenyewe. ndio maana mtu akilewa anapewa maji taratibu anarudi kwenye hali yake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom