Kinachosumbua DRC ni ukabila, wizi, kukosa uzalendo na umoja wa kitaifa

Kinachosumbua DRC ni ukabila, wizi, kukosa uzalendo na umoja wa kitaifa

ZALEMDA

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2017
Posts
1,956
Reaction score
2,225
Kinachosumbua DRC ni ukabila wizi kukosa uzalendo na umoja wa kitaifa.

1. Ukabila: Pale DRC Kuna kabila la wanyamulenge.Hawa ni watusi asili Yao kutoka Rwanda, Uganda na Burundi. Kwa asili watusi hawapendi kutawaliwa, kwahiyo wamekuwa wakitafuta msaada kutoka kwa ndugu zao wa Rwanda na Uganda kutaka kuwepo madarakani kwa vyovyote vile.

Machafuko yangeweza kufikia kiwango cha vita kama ya Burundi na Rwanda hata Uganda lakini nafikiri watusi wa DRC ni wachache na kwa sababu DRC ni nchi kubwa sana hawawezi kumudu vita ya muda mrefu.

Ukitaka amani ya kudumu mashariki mwa DRC, ongea na P Kagame na Museveni waache kuwa sappoti ndugu zao Wanyamulenge.Yani vita ya eastern DRC ni kama vita Kati ya Ukraine na Russia (kutetea ndugu tunapoona wanaonewa) wanachokitafuta wanyamulenge (watusi wa DRC Congo) ni kutaka nchi igawanywe ili wapate nchi Yao ambayo wataiongoza wenyewe kutimiza malengo ya Tutsi empire (Rwanda, Burundi, Uganda and some other eastern Africa countries ambazo sizitaji hapa kumbuka kwamba mtoto wa Museveni alisema anaitaka Nairobi)

2. Wizi wa rasimali za DRC: Nchi ni kubwa mno. Imejaa kila Aina ya madini, dhahabu, cobalt, nk. Nchi na magharibi zimekuwa zikisapoti machafuko nchini DRC kwa lengo la kuibia nchi. Hata Rwanda inafanya biasha hii.

3. Kukosa uzalendo na umoja wa kitaifa: DRC ni nchi kubwa mno na single administration from Kinshasa for a politically weak government ni shida sana.nafikiri waje wajifunze kwa Tanzania. You need a strong local government ambayo inawajibika kwa strong national government. Ndiyo maana utawala wa majimbo naupinga sana kwa nchi yetu maana litakuwa ni Jambo jipya kuli control itawa taabu.Utawala wa majimbo ulitakiwa uanze na mwanzo wa taifa kama USA.

Kwa leo niishie hapa
 
Tanzania ipo safarini kuelekea huko waliko DRC. Bado kilometers chache sana! Na hivi WanyaRwanda na Warundi washajipenyeza miongoni mwetu... Tutawahi sana!

Kama unabisha fuatilia gepu kati ya Watendaji serikalini, wanasiasa na common wananchi. Angalia PT na wapigaji wengine serikali ni walivoshtukia dili!

Yaani kuna ka uhusiano kama wa ngombe hasiyepewa matunzo lakini ni lazima atoe maziwa mengi! Bajeti ya matunzo ipo au inakopwa lakini inaingia matumizi mengine ya hanasa!

Shortcut ya utajiri wa haraka na kufura mashavu kwa sasa si biashara, taaluma wala elimu Bali ni uchawa na siasa za kitapeli!

Wapo wajinga wanamsifia JPM bila kujua hata yeye alijaribu kuwainua na kuwatengeneza wezi wapya kwa kuwashusha waliokuwepo!

Safari yetu rasmi kuingia kwenye mkwamo wa DRC inakaribia ukomo!

Labda TPDF waliingilie kati!

Tragedy!!
 
Back
Top Bottom