Mjomba Fujo
JF-Expert Member
- Oct 27, 2012
- 2,438
- 6,313
Kwa Miongo kadhaa Tanzania kama nchi inayojitegemea, inapiga hatua kwa mwendo wa kobe.
Kuna mambo ukiangalia ni aibu sana, yani mpaka leo hii tunahangaika na mashimo ya choo, madawati, na vitu vingine ambavyo ni aibu hata kuvitaja.
Kama Taifa naona tuna changamoto hizi kubwa:
1. Ufisadi
2. Rushwa
3. Namba 1 na 2 zinazalisha uvujaji wa kodi na mapato.
Tanzania sio ya kukusanya Trillion 2 mbili kwa mwezi, kuna chenga nyingi, kuna wizi mwingi, kuna rushwa nyingi, na hizi zote zinapelekea ukusanyaji hafifu wa mapato ya serikali.
Tanzania hii kodi zikikusanywa vizuri kwa East Africa tunapiku nchi zote.
Nieleweke ninaposema zikikusanywa vizuri simaanishi wakamue watu kwenye tozo la hasha, hapa nazungumzia zile zinakwepwa.
Wanaosumbuliwa na kodi ni wafanyabiashara wadogo, wafanya biashara wakubwa wanapeta tu, kodi ya milioni 400 inakwepwa kwa ofisa kupewa rushwa ya million 10 tu, zigo mtaangushiwa nyinyi wa chini.
Mbaya zaidi wanaotakiwa kusimamia hizi sera ndio hao hao panya wa mezani nao wanakula na kusaza.
Yote haya yanachangia kuzorota kwa maendeleo ya taifa kwa nyanja zote kama uchumi, elimu, afya, miundo mbinu nk.
Nini kifanyike?
Kiuhalisia cha kufanyika hamna maana hata akija mtu msafi mmoja atakumbana na wachafu 1000, sasa 1 vs 1000 hapo moja lazima ishindwe mana itapigwa vita vibaya mno.
Kuna baadhi ya taasisi kama wewe ni mcha Mungu, mtu msafi, huwezi kudumu ni aidha utahamishwa kazini au duniani.
Wizi na ufisadi upo ngazi zote za juu mpaka kwenye shina kule, hata wewe unaeandika risiti feki ya tax ambayo hujapanda ili ukarejeshewe pesa ofisini kwako bado upo kwenye mjumuisho huu.
Hitimisho
Tanzania ni taifa lenye uwezo mkubwa kiuchumi, ila uwezo wa waendeshaji wa taifa umejikita kwenye wizi na ubinafsi.
Nakubaliana na wazungu tuna IQ ndogo, zingalikua kubwa tungetumia fursa na uwezo wetu kupiga hatua 10 zaidi, ila kwakua tunataka kuiba iba basi ngoja tubaki kusindikiza dunia.
Facts check
Leo ukimwangalia mbunge awe ndugu yako au mtu yeyote yule, jicho unalomwangalia nalo sio lile la kibunge la uwakilishi wa wananchi bali utaona ni mtu aliepatia maisha anapiga pesa tu, sasa hili jicho hata yeye mbunge huliona hivyohivyo wakati anagombea kiti, sio kwamba ana uchungu na wananchi ila ni fursa kubwa kiuchumi kwake, biashara zake na familia yake, hivyohivyo kwa mawaziri, na wengineo.
Taifa la wezi.
Kuna mambo ukiangalia ni aibu sana, yani mpaka leo hii tunahangaika na mashimo ya choo, madawati, na vitu vingine ambavyo ni aibu hata kuvitaja.
Kama Taifa naona tuna changamoto hizi kubwa:
1. Ufisadi
2. Rushwa
3. Namba 1 na 2 zinazalisha uvujaji wa kodi na mapato.
Tanzania sio ya kukusanya Trillion 2 mbili kwa mwezi, kuna chenga nyingi, kuna wizi mwingi, kuna rushwa nyingi, na hizi zote zinapelekea ukusanyaji hafifu wa mapato ya serikali.
Tanzania hii kodi zikikusanywa vizuri kwa East Africa tunapiku nchi zote.
Nieleweke ninaposema zikikusanywa vizuri simaanishi wakamue watu kwenye tozo la hasha, hapa nazungumzia zile zinakwepwa.
Wanaosumbuliwa na kodi ni wafanyabiashara wadogo, wafanya biashara wakubwa wanapeta tu, kodi ya milioni 400 inakwepwa kwa ofisa kupewa rushwa ya million 10 tu, zigo mtaangushiwa nyinyi wa chini.
Mbaya zaidi wanaotakiwa kusimamia hizi sera ndio hao hao panya wa mezani nao wanakula na kusaza.
Yote haya yanachangia kuzorota kwa maendeleo ya taifa kwa nyanja zote kama uchumi, elimu, afya, miundo mbinu nk.
Nini kifanyike?
Kiuhalisia cha kufanyika hamna maana hata akija mtu msafi mmoja atakumbana na wachafu 1000, sasa 1 vs 1000 hapo moja lazima ishindwe mana itapigwa vita vibaya mno.
Kuna baadhi ya taasisi kama wewe ni mcha Mungu, mtu msafi, huwezi kudumu ni aidha utahamishwa kazini au duniani.
Wizi na ufisadi upo ngazi zote za juu mpaka kwenye shina kule, hata wewe unaeandika risiti feki ya tax ambayo hujapanda ili ukarejeshewe pesa ofisini kwako bado upo kwenye mjumuisho huu.
Hitimisho
Tanzania ni taifa lenye uwezo mkubwa kiuchumi, ila uwezo wa waendeshaji wa taifa umejikita kwenye wizi na ubinafsi.
Nakubaliana na wazungu tuna IQ ndogo, zingalikua kubwa tungetumia fursa na uwezo wetu kupiga hatua 10 zaidi, ila kwakua tunataka kuiba iba basi ngoja tubaki kusindikiza dunia.
Facts check
Leo ukimwangalia mbunge awe ndugu yako au mtu yeyote yule, jicho unalomwangalia nalo sio lile la kibunge la uwakilishi wa wananchi bali utaona ni mtu aliepatia maisha anapiga pesa tu, sasa hili jicho hata yeye mbunge huliona hivyohivyo wakati anagombea kiti, sio kwamba ana uchungu na wananchi ila ni fursa kubwa kiuchumi kwake, biashara zake na familia yake, hivyohivyo kwa mawaziri, na wengineo.
Taifa la wezi.