Elections 2010 Kinana aomba wasilaumiwe sana - "Tusiwachanganye wananchi"

Elections 2010 Kinana aomba wasilaumiwe sana - "Tusiwachanganye wananchi"

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Leo nimejikuta nacheka sanaaa.. Mwenyekiti wa Kampeni ya Urais ya Kikwete Bw. Kinana akihojiwa mapema leo asubuhi na ITV amevisihi vyama vingine visiwaeleze sana mambo mabaya na yenye kubebesha lawama serikali ya Kikwete kwani kwa kufanya hivyo wanawachanganya wananchi. "Tuna matatizo mengi ya afya, elimu, maji, miundombinu hivyo tuzungumzie sera zaidi tutafanya nini" amesema Kinana.

Je vyama vingine vitamsikiliza na kuacha kuzungumzia mambo ya kashfa au ubovu na kuanza kueneza sera tu? Je kuna umuhimu wa kuwajulisha wananchi mambo yaliyokwenda kombo miaka mitano iliyopita?
 
If you want to say nothing, at least say it in a style...
 
CCM wametuchanganya wao, kweli sera wanazo nzuri tu, ni kitu gani sasa kiliwashinda kuzitekeleza? Hicho ndio wananchi wanapaswa waeleweshwe, na wenyewe wananchi waamue ajira yenu iendelee au ikome.
 
Leo nimejikuta nacheka sanaaa.. Mwenyekiti wa Kampeni ya Urais ya Kikwete Bw. Kinana akihojiwa mapema leo asubuhi na ITV amevisihi vyama vingine visiwaeleze sana mambo mabaya na yenye kubebesha lawama serikali ya Kikwete kwani kwa kufanya hivyo wanawachanganya wananchi. "Tuna matatizo mengi ya afya, elimu, maji, miundombinu hivyo tuzungumzie sera zaidi tutafanya nini" amesema Kinana.

Je vyama vingine vitamsikiliza na kuacha kuzungumzia mambo ya kashfa au ubovu na kuanza kueneza sera tu? Je kuna umuhimu wa kuwajulisha wananchi mambo yaliyokwenda kombo miaka mitano iliyopita?

Japo siungani na msomali moja kwa moja, lakini hoja ya msingi ina mantiki tuu tusibakie kulaumu, kulalamika na kulalama tuu, bali kampeni ziseme tutafanya nini.
Yaani zisibakie kampeni za fault finding mission, bali trend setting mission, hayo mabaya ya nyjuma/CCM yatumike kama sababu, cause ya kutufikisha hapa tulipo, na isiwe ndio the only finger pointing CCM, CCM, tunawapa free publicity hawa CCM kwenye kampeni zetu.
 
Wananchi wana haki ya kujua uovu wa serikali ya CCM ili wafanye uchagizi uliokwenda shule. Ukweli utabakia kuwa ukweli, Kinana anatakiwa kulifahamu hilo!
 
Hayo sio Maji ya Shingo hayo ni MAJI YA PUA hawawezi kupumua.... nabado watajikanyagakanyaga weeeeeeeeee huku wakiwatengenezia njia UPINZANI.
Bado yule Mbwatukaji wao nae haja likoroga..... wataanza mmoja badaa ya mwingine kama jana Kigoda alivyo mnadi Mkapa badala ya Kikwete yaani hii sinema sijui tuipe jina gani kwa kweli lol! :becky::becky::becky::becky:
 
Wananchi walishanganywa siku nyingi?

Sasa hapa wanachanganyikiwa wao ndiyo maana wanaamua kutafuta namna ya kutuliza mzuka kwani wanaogopa wasizidi kuchanganyikiwa zaidi. Unajua wiki-ZAIDI hawataweza hata kufanya kampeni.
 
Nini? Wanataka wizi wao na hujuma kubwa waliofanya dhidi ya wananchi usizungumzwe jukwaani? Wao wana-control kodi zinazokusanywa kwa hivyo wana advantage ya kueleza "mafanikio" waliyoleta. Na upinzani wana haki ya kusema "mafanikio" hayo ni upuuzi kwani mnaiba hela nyingi zingine. Iko mbaya gani hapa?

Hata hivyo Dr Slaa anafanya yote mawili -- anawaponda CCM kwa ufisadi wao na hapo hapo anaeneza atafanya nini akiingia madarakani.

Kweli maji shingoni hawa!!!!
Strategy yao hii ni ya kipuuzi kabisa!!!! Songa mbele Dr Slaa -- yamebakia mabomu mangapi vile? Na ninaona umeanza na yale mepesi mepesi -- yaani rasha rasha tu.
 
Jamaa anaona ni wachafu ndo maana anakimbilia kwenye kusema sera ndo zisemwe. Maana anajua CCM ni wazuri kwenye sera zisizotekeleza. Mkwele sasa hivi ameahidi bajaji kwa kinamama wajawazito, neti 2 kwa kila kaya, kila aakiona ziwa au mto anaahidi meli na bado ataahidi kujenga bandali Singida. Harafu
 
Lakini nimejiuliza nilipomsikiliza mbona lugha ilikuwa imepowa na sauti ilikuwa ya kiuungwana ,sio ile tena ya kuonyesha kwamba tayari wamekata nchi iwe isiwe,nimejiuliza mengi nikasema nini wanachokiona mbele yao,msomali wa watu amekazana pia kuonyesha kwamba wao sio wanaotumia lugha za matusi,ukweli wananchi wanaujua nani mwenye matusi na ngebe
 
Leo nimejikuta nacheka sanaaa.. Mwenyekiti wa Kampeni ya Urais ya Kikwete Bw. Kinana akihojiwa mapema leo asubuhi na ITV amevisihi vyama vingine visiwaeleze sana mambo mabaya na yenye kubebesha lawama serikali ya Kikwete kwani kwa kufanya hivyo wanawachanganya wananchi. "Tuna matatizo mengi ya afya, elimu, maji, miundombinu hivyo tuzungumzie sera zaidi tutafanya nini" amesema Kinana.

Je vyama vingine vitamsikiliza na kuacha kuzungumzia mambo ya kashfa au ubovu na kuanza kueneza sera tu? Je kuna umuhimu wa kuwajulisha wananchi mambo yaliyokwenda kombo miaka mitano iliyopita?

teh teh MKJJ,

Kweli matatizo yako mengi sana ambayo serikali ya JK inapambana nayo na mafanikio yake kweli yanakuwa hafifu na twashindwa jua kama kweli twaenda mbele au twarudi nyumaaa?

Na dhani ni kweli kuna haja ya kujua wapi serikali walienda kombo katika miaka mitano na ndio itakuwa msingi bora wa utawala bora na viongozi kujituma kufanya kazi za wananchi wao na kutokalia kutupa porojo na siasa zaidi kuliko maendeleo.

Na ndio maana napendekeza katiba ya nchi kupanguliwa na kupangwa upya na haya yote yatakuwa reveal na nchi ita kuwa na Mustakabali unaoeleweka na tutapiga maendeleo kwa kasi kabisa

 
Nini? Wanataka wizi wao na hujuma kubwa waliofanya dhidi ya wananchi usizungumzwe jukwaani? Wao wana-control kodi zinazokusanywa kwa hivyo wana advantage ya kueleza "mafanikio" waliyoleta. Na upinzani wana haki ya kusema "mafanikio" hayo ni upuuzi kwani mnaiba hela nyingi zingine. Iko mbaya gani hapa?

Hata hivyo Dr Slaa anafanya yote mawili CCM -- anawaponda CCM kwa ufisadi wao na hapo hapo anaeneza atafanya nini akiingia madarakani.

Kweli maji shingoni hawa!!!!
Strategy yao hii ni ya kipuuzi kabisa!!!! Songa mbele Dr Slaa -- yamebakia mabomu mangapi vile? Na ninaona umeanza na yale mepesi mepesi -- yaani rasha rasha tu.

Kabisa Slaa anafanya yote, anaeleza udwanzi wao na kumwaga sera!!! sasa kazi kwao nyambafu!!!
 
Mfa maji haachi kutapatapa..............tutabanana hivihivi mpaka ukweli ujulikane na mpaka kieleweke lazima watz wajue jinsi nchi yao inavyohujumiwa na hawa wadokozi wakubwa wana ccm wakijua then wataamua namna ya kuihukumu ccm kwa kuwasababishia watz maisha waliyonayo ambayo kikwete anayaita maisha bora kwa kila mtz
 
Leo nimejikuta nacheka sanaaa.. Mwenyekiti wa Kampeni ya Urais ya Kikwete Bw. Kinana akihojiwa mapema leo asubuhi na ITV amevisihi vyama vingine visiwaeleze sana mambo mabaya na yenye kubebesha lawama serikali ya Kikwete kwani kwa kufanya hivyo wanawachanganya wananchi. "Tuna matatizo mengi ya afya, elimu, maji, miundombinu hivyo tuzungumzie sera zaidi tutafanya nini" amesema Kinana.

Je vyama vingine vitamsikiliza na kuacha kuzungumzia mambo ya kashfa au ubovu na kuanza kueneza sera tu? Je kuna umuhimu wa kuwajulisha wananchi mambo yaliyokwenda kombo miaka mitano iliyopita?

Mkuu,

Sikuiona hiyo lakini inachekesha sana!! Kinana anashindwa kuelewa ili wananchi waone tofauti ni lazima kuonyesha mapungufu yao, na wapi walikosea ili kuwashsawishi wananchi wafanya uchaguzi vizuri.

Naunga mkono kampeni za kutumia uozo wa CCM kama weak point kuelezea wapi mambo yatarekebishika. Hii ni dalili kuwa hata wao wenyewe wangundua kuwa hawana jipya. Ukiangalia ilani ya 2005 v/s ya 2010; utacheka, maana kuna sehemu nyingine wamehamisha kama yalivyo!!! Wnajua ni wachache sana wanaosoma ilani kabla ya kupiga kura!!!
 
Leo nimejikuta nacheka sanaaa.. Mwenyekiti wa Kampeni ya Urais ya Kikwete Bw. Kinana akihojiwa mapema leo asubuhi na ITV amevisihi vyama vingine visiwaeleze sana mambo mabaya na yenye kubebesha lawama serikali ya Kikwete kwani kwa kufanya hivyo wanawachanganya wananchi. "Tuna matatizo mengi ya afya, elimu, maji, miundombinu hivyo tuzungumzie sera zaidi tutafanya nini" amesema Kinana.

Ni mwenye akili-taka tu ambaye hawezi kuhusisha 'matatizo mengi ya afya, elimu, maji, miundombinu' na ukosefu wa fedha na ukosefu wa fedha umesababishwa na mafisadi ccm. Kwa taarifa yako Kinana haiwezekani kuzungumzia suluhisho la matatizo bila kujua chanzo cha matatizo hayo. Huko ni sawa na kuzuia moshi usitoke nje ya nyumba wakati ndani unaendelea kukoka moto. Ukitaka moshi usitoke nje zima moto kwanza. tunaondoa kwanza ufisadi ili fedha zipatikane ili tutatue hayo matatizo.
 
Alikuwa anaongea kwa uoga sana, naona ile meli imemmaliza nguvu kabisa yaani y uko chali na timu yake anaogopa hata kutaja ratiba ya kampeni ya JK anataja kwa kigugumizi; DR chanja mbuga mwezi wa mwisho watashindwa hata kupanda majukwaani hapo ndio wataona watanzania wanavyoichukua nchi yao
 
Waeneze sera tu? kwani si misera yao mibovu iliyotuweka hapa hadi leo? Yes, wapinzani lazima wasemelee kwa wananchi mauoza yaliyoyanywa na sisiemu hadi kutufikisha hapa tulipo leo.....!
 
Chadema na wagombea wote wa chadema wajitahidi kutia msisitizo kwenye kampeni kuwa tuna maswala muhimu mawili ambayo tunataka kuwafahamisha wananchi mosi, udhaifu wa serikali ya CCM na athari ilizosababisha ktk ujenzi wa taifa imara na pili chadema tutafanya nini pindi mtakapotuchagua(sera). hiyo inaweza kukata ngebe za CCM kuwa CHADEMA hawaongelei sera hivyo wanapata talking point, so ni muhimu kutanabaisha wazi kuwa tunataka hawa watanzania wenzetu wa CCM watuelewe kuwa lazima to wa expose kwa wananchi ili watanzania wajue ukweli uliofichwa kuhusu ubovu wa chama cha mapinduzi na then tutawaeleza sisi chadema tutafanya vipi tofauti , hapo ndipo mtasikia sera zetu, huwezi kutatua matatizo ya watanzania kama chama cha upinzani kama huoni kasora na matatizo yalioufanya taifa letu kuwa maskini, sasa wenzetu wa CCM hawataki mabaya yao kuanikwa hadharani ili wananchi wasifanye informed decision, which is very wrong.
 
Back
Top Bottom