Kinana: Serikali tatu ni hatari, itasababisha machafuko

Mi nashangaa Kikwete kwa unafiki kawatoa 'warwanda' kawaacha wasomali! Aziz Ally wana mtaa wao, hadi mkaa wanauza!
 
Hivu muungano unalinda vipi amani? . Na hivi TZ kuna Amani kwa sasa?
Yapasa kuheshimu haki ya wengine kutoa maoni huku ukielewa kuwa hapo ndipo uelewa wake unaishia na hataki kufikiri!
 
unaweza ku prove mkuu au ndio viroba asubuhi

Fuatilia vizuri thread hii toka mwanzo pamoja na michango ya wengine utajikuta peke yako ndo upo tofauti. Inawezekana hujaelewa au unataka malumbano tu. Unataka kuprove nini? Kwamba kinana na CCM wana msimamo waserikali mbili au?
 
CCM na Amani:

Tukiruhusu vyama vingi itatokea fujo.
Mkichagua upinzani itatokea machafuko.
Na Sasa Serikali tatu italeta machafuko.

Hivi CCM wamekosa kabisa Sera zaidi ya hiii ya Amani na Mshikamano ambao tayari haupo?
 
Mods kwa nini mmetoa uzi huu wakati umzingatia itifaki zote za jf? Halafu haieleweki mmeunganisha na uzi gani! Naomba mrudishe tafadhali, tunajadili mustakabali wa taifa letu.
 
Mh Kinana hajui hata maana ya Muungano unaotakiwa na watanzania wa leo. Yeye anafikiri ni wa mke na mume kama ule wa awali? Maana katika muungano mwaka 1964, Tanganyika ilipoteza uasili wake. Ni kama iliolewa na Zanzibar, maana Zanzibar ilibaki na serikali yake. Kama tunafikiria Muungano wa "Federation" hakuna nchi inayopaswa kupoteza uasili wake. Wakati Tanganyika inaungana na Zanzibar maono ya watu wake yalikuwa duni ukilinganisha na watanzania wa wakati huu. Sasa hii hofu ya CCM na viongozi wake inatoka wapi wakati wananchi wana upeo mkubwa wa kuelewa ukilinganisha na mwaka 1964? Hata jina la serikali ya Muungano liliyotajwa kwenye "Articles of Union"ya wakati ule ilitaja kabisa jina litakuwa "The united Republic of Tanganyika and Zanzibar." Jina laTANZANIA liliasisiwa baadaye kuondoa mlolongo wa kutamka majina ya nchi mbili. Kwa sababu za uandishi wa historia kupotoshwa makusudi na watawala wetu, ni watu wachache sana wanaofahamu, au kukumbuka mambo yalivyokuwa. Hawa viongozi wote wa CCM walio madarakani ni wale waliolishwa historia iliyopotoshwa, ndio maana wanahubiri hofu walizonazo. MH. KINANA NA VIONGOZI WA CCM WAACHIE WATANZANIA WAPATE FURSA YA KUTENGENEZA NCHI WANAYOTAKA BILA YA KUTIWA HOFU. Hata hivyo katiba sii BIBLIA wala QURAN ambazo yaliyoandikwa yalishaandikwa!! Ni kitu kinachojadilika na kurekebishwa muda wowote inapohitajika. Wamarekani pamoja na kuwa makini na katiba yao, wameshaifanyia marekebisho mara 27!! SISI NI KWA NINI TUIONE KATIBA KAMA KITU KITEULE KISICHOWEZA KUBADILISHWA HAJA INAPOKUWEPO? WANANCHI TUAMKE TUSILEMAZWE NA HAWA WANAOTAKA KUTUTAWALA KIFIKRA.
 
Kinana hana hoja.

ccm ndio inayoingilia mchakato wa katiba mpya.
Na ndio itakayoleta vurugu nchini.maana ni mambo mazuri yaliyoandikwa kwenye rasmu ya awali ndio maoni ya watanzania na yeyote anayeyapinga huyo sio mtanzania bali ni msaliti na mroho wa madaraka.

cha msingi ni kuiboresha hiyo rasimu na ccm kujiandaa kisaikolojia kuongozwa na serikali ya cdm bara na zanzibar cuf.

hofu ya ccm sio serikali 3 wala gharama za uedeshaji maana kama ni gharama wasingeongeza mikoa ,wilaya n.k bali hofu yao ni zanzibar kuongozwa na cuf.

tayari tuna marais kibao,kuna rais wa TFF,n.k
Hoja rais wa nchi atakuwa mmoja wengine watakuwa mawaziri wakuu.
 
.ENYI WANACCM Mnaoamini kuwa serikali tatu ni kuvunja muungano ningewaelewa sana mngekuja na wazo la kuwa na serikali moja ya Tanzania, kama Tanganika ilipoungana na Zanzibar ikazaliwa Tanzania ,why Zanzibar ilibaki mpaka leo?...Wakti mwingine nafikiri ILIKUWA NI KUBADILI JINA LA NCHI NA KUISAIDIA zanziba kiuchumi.
 
Ama kweli ukistaajabu ya Musa utayaona ya filauni.Muungano wa nchi mbili umetusumbua kwa muda mrefu na tumekaa vikao vingi sana tukisema tunatatua kero ndogondogo za Muungano ambazo mpaka leo zimeshindwa kutatulika.Kwa akili ya kawaida isiyohitaji elimu ya juu embu tujiulize mambo yafuatayo: 1) Ikiwa leo hii katika hali ya muungano tulionao tukasambaratika na kugawanyika,mustakabali wa nchi yetu upo vipi?.2)Vijana wengi walio na umri chini ya miaka 35 wengi hawahitaji aina hii ya muungano,si kwa Zanzibar wala Tanzania bara,je tunatengeneza mazingira yapi ya baadae kwa kizazi hicho.Tuache ushabiki wa kisiasa na tuangalie mustakabali wa nchi yetu.Gharama za Serikali ya tatu zitachangiwa na nchi zote mbili na kila nchi itatambua rasilimali ilizo nazo na namna ya kendesha nchi bila ya kuingiliwa na upande mwingine.Wakati umefika wa kufikiria nje ya box.
 
Propaganda ndivyo ilivyo. Zua jambo, lipambe lipambike, watu watakuamini tu. Kinana anasema Serekali 3 zitauvunja muungano, ati serekali moja ikiamua kwenda vitani nyingine inaweza kukataa. Saa hii tunavyo danganywa na Kinana, kule Zenji, wao wana bunge lao, bajeti yao, Rais wao, Bendera yao, wimbo wao wa Taifa. Hao Kinana anadhani akitaka kwenda vitani tayari watafuatana naye. Pole Kinana, yeye mwenyewe akitaka kwenda Zenji lazima aonyeshe pass ya kuingia Zenji, sasa huo ndo Muungano??? Ama kweli, Zidumu fikra sahihi za M/Kiti wa CCM.
Kuwe na serekali 10 au ishirini, Muungano wako Kinana upo kwenye mushkeli mpaka sasa. Tupe serekali 3, tujadili aina ya muungano. Nasema; "TUUJADILI" Yaani "Shirikisho". BAAAAAASI. Vingine, muungano utakufia mkononi Kinana.
Tanganyika ni lazima. Kama unautaka muungano uwepo siku mbili tatu hivi.
Ati serekali 3 zitaleta machafuko; kakuambia nani? Kwani hizo serekali 3 zitaundwa na watu kutoka sayari nyingine au ni sisi! Kama umekosa cha kupingia kubali yaishe. Ukikubali haitakuwa aibu ati kwa sababu Dr. Slaa amekubali. CCM kazi yao ni kupinga kila kitu ambacho upinzani umekisema.
 
Kinana sisi hatuna tabu na ww sisi shida yetu ni Tanganyika yetu sasa kama mtaifuta zanzibar then Tanganyika ndo ibaki nchi xawa 2.
 
Mbona hawaongelei Serikali moja, endapo tatu ni mzigo?
 
Serikali tatu si kwa ajili ya Chadema au CUF au NCCR. Si kwa ajili ya Wahaya, wanyakyusa , wachaga,wasukumuma,wazaramo, wasambau n.k . Ni kwa ajili ya Watanzania wote na ni maoni kutoka kwa Watanzania walio wengi sasa huyu katibu asituleetee maoni yake! Tanganyika kwanza Vyama vyetu baadaye.
 
Maccm yanajua yakiruhusu Tanganyika itakuwa ngumu kuiba kura kwenye sanduku la rais wa muungano, Tanganyika na Zanzibar wakati uchaguzi,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…