Kinda mpya wa Simba queens (Victoria Masele)

Nilitazama mpira jana "live" kupitia Global TV lakini mbona kama mtupu sana uwanjani kwani hata mpira wa kurusha tu ulimshinda. Kwa jinsi nilivyomuona jana nahisi usajili wake Simba kuna ujanja ujanja fulani kwani hana uwezo wa kuchezea Simba Queen. Labda waseme tu ameomba kuja kufanya mazoezi apate uzoefu.
 
Yes Hata mm nilishangaa alishindwaje kurusha Ule Mpira, Hana Uwezo Wa Kucheza Hapo Simba Princess Kwa Mda Mrefu, Then siamini Kwamba Kweli ana Miaka 13 Huyo Binti, Huyu Namuona Atakuja Kuwa Kama Chikwende Tu.
 
Huyo siyo mchezaji aliyesajiliwa rasmi na Simba Queens, Ni mwanafunzi ambaye anaishi Marekani na wazazi wake watanzania lakini wapo Tanzania kwa mapumziko tu.

Anaipenda Simba ndiyo maana alichagua kucheza ili kujipa mazoezi tu.
 
Huyo siyo mchezaji aliyesajiliwa rasmi na Simba Queens, Ni mwanafunzi ambaye anaishi Marekani na wazazi wake watanzania lakini wapo Tanzania kwa mapumziko tu.

Anaipenda Simba ndiyo maana alichagua kucheza ili kujipa mazoezi tu.
Mkuu ahsante sana kwa ufafanuzi maana daa nilishangaa sana jana kwa promo zote zile hata mpira wa kurusha tu ulimshinda na tukio lingine alipiga hewa badala ya mpira nikajua tayari Simba wameshapigwa za uso mchana kweupe.
 
Huyo siyo mchezaji aliyesajiliwa rasmi na Simba Queens, Ni mwanafunzi ambaye anaishi Marekani na wazazi wake watanzania lakini wapo Tanzania kwa mapumziko tu.

Anaipenda Simba ndiyo maana alichagua kucheza ili kujipa mazoezi tu.
Daha kweli kabisa muonekano wake tu na jinsi alivyo anaonekana kabisa anamwili wa supermarket.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…