King Kiba atupia lawama tena kwa vituo ya radio na Tv

kedrick

JF-Expert Member
Joined
Apr 25, 2015
Posts
5,080
Reaction score
4,914
Alikiba amesema tatizo lililopo kwenye muziki wa Tanzania, ni baadhi ya nyimbo nzuri kutopewa nafasi ya kusikika kama zinavyostahili.

Ametoa kauli hiyo wakati akihojiwa kwenye kipindi cha Daladala Beat cha Magic FM wakati alipokuwa kwenye ziara ya kupromote wimbo wake na Ommy Dimpoz, Kajiandae.

“Kuna watu wanaweza wakawa wanajua kabisa huu ni muziki mzuri, kuna watu hawatotaka ukae kwa muda mrefu, hii inatucost sana,” alisema.
“Kuna muziki mzuri, wasanii wanaimba nyimbo nzuri lakini kuna watu wengine hawataki hii haifai hatuwezi kuendelea,” alisisitiza. “Hili suala siwezi kulinyamazia kimya.”

Source Bongo 5
 
atuliage nae sio kila siku lawama, kazi ya kuskiliza tuachie wasikilizaji,
We dondosha ngoma kali hayo mengine achana nayo bhana,
Unamaneno maneno utadhani mwimbaji wa singeli bhana, ah
Mbn maneno mengi sana kuna mini ndg
 

Huyu nae kila siku ni kulalamika hakuna kitu anaweza sifu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…