M-mbabe
JF-Expert Member
- Oct 29, 2009
- 13,203
- 23,027
Huu ndiyo ukweli wenyewe.
Wapinzani wakichukua nchi watatumia fimbo ile ile ambayo sisi CCM tumekuwa tukiitumia dhidi ya tusiowapenda, wakiwemo wa vyama vya upinzani.
Na tusijidanganye kuwa CCM tutakaa madarakani milele. Dalili zilizopo zinaonyesha tutaondolewa madarakani muda si mrefu.
Kitakachotokea upinzani ukiingia ikulu ni hiki:
Bila kujali ni kinyume cha katiba au la, kwa nyakati tofauti (say kwa interval ya miezi sita sita) serekali chini ya upinzani itawasweka Segerea viongozi wastaafu kwa mashitaka yasiyodhaminika kwa staili ile ile inayotumika sasa. Wanaweza kukaa selo hata kwa miaka 15 kwa kisingizio cha kutokamilika kwa upelelezi. Yatakuwa ni majuto makubwa sana kwao na kwa wanaowategemea.
Nitoe wito kwa watu wenye ushawishi ndani ya chama chetu CCM waendelee kuwashauri sana viongozi walio madarakani sasa kuzingatia kutenda haki kwa wote ili wasiwape kisingizio wahasimu wao kuja kulipa visasi huko mbeleni.
What goes around comes around!
Wapinzani wakichukua nchi watatumia fimbo ile ile ambayo sisi CCM tumekuwa tukiitumia dhidi ya tusiowapenda, wakiwemo wa vyama vya upinzani.
Na tusijidanganye kuwa CCM tutakaa madarakani milele. Dalili zilizopo zinaonyesha tutaondolewa madarakani muda si mrefu.
Kitakachotokea upinzani ukiingia ikulu ni hiki:
Bila kujali ni kinyume cha katiba au la, kwa nyakati tofauti (say kwa interval ya miezi sita sita) serekali chini ya upinzani itawasweka Segerea viongozi wastaafu kwa mashitaka yasiyodhaminika kwa staili ile ile inayotumika sasa. Wanaweza kukaa selo hata kwa miaka 15 kwa kisingizio cha kutokamilika kwa upelelezi. Yatakuwa ni majuto makubwa sana kwao na kwa wanaowategemea.
Nitoe wito kwa watu wenye ushawishi ndani ya chama chetu CCM waendelee kuwashauri sana viongozi walio madarakani sasa kuzingatia kutenda haki kwa wote ili wasiwape kisingizio wahasimu wao kuja kulipa visasi huko mbeleni.
What goes around comes around!