Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,468
- 911,184
Mara nyingi kuwa macho na mgema unaposifiwa......
Mara nyingi ni kuwa mnywaji anakujengea hoja ya siri....
Mara nyingi mgema huvimba kichwa na kudhani mambo shwari
Mara nyingi mambo huwa siyo shwari hata chembe ila hadaa..
Hivi kileleni feki utakitambuaje?
Mpenzio huweza kujifanya mjuaji kwa ghiliba kibao
Na kujitia karidhishwa na dhoruba ulizomletea!
Kumbe wote ni usanii wake wa kufupisha karaha zako..........
Kwa vile kaboreka huhitaji basi yaishe naye apumzike
Hivi kileleni feki utakitambuaje?
Dalili nyingi hukuachia lakini wewe hukupofusha na misifa!
Siri ya kung'amua utapeli huu ni kumjua mjenga hoja...
Hukusubiri ukikaribia kileleni naye kuanza vioja!
Lengo ni kukuharakisha kwa ukelele na mauno balaa..
Hivi kileleni feki utakitambuaje?
Huku hadaa yake ni kuwa naye umemfikisha alikotaka!
Yawaje kila mechi twende sote kileleni kama siyo gheresha zake?
Ukidhani mpo wote basi nawe kulainika na kujiachia!
Kumbe sasa umekuwa teja wa mbinu zake hadaa..
Hivi kileleni feki utakitambuaje?
Ukiona naye kakomesha vimbwanga vyake baada ya wewe..
Basi jua amekuchora na tafuta mbinu mpya ya kumkabili.......
Hakiki pumzi yake kama nayo imekatika ghafla...
Ukiona kanywea na akushurutisha ubanduke basi jua umeliwa.......
Hivi kileleni feki utakitambuaje?
Mara nyingi ni kuwa mnywaji anakujengea hoja ya siri....
Mara nyingi mgema huvimba kichwa na kudhani mambo shwari
Mara nyingi mambo huwa siyo shwari hata chembe ila hadaa..
Hivi kileleni feki utakitambuaje?
Mpenzio huweza kujifanya mjuaji kwa ghiliba kibao
Na kujitia karidhishwa na dhoruba ulizomletea!
Kumbe wote ni usanii wake wa kufupisha karaha zako..........
Kwa vile kaboreka huhitaji basi yaishe naye apumzike
Hivi kileleni feki utakitambuaje?
Dalili nyingi hukuachia lakini wewe hukupofusha na misifa!
Siri ya kung'amua utapeli huu ni kumjua mjenga hoja...
Hukusubiri ukikaribia kileleni naye kuanza vioja!
Lengo ni kukuharakisha kwa ukelele na mauno balaa..
Hivi kileleni feki utakitambuaje?
Huku hadaa yake ni kuwa naye umemfikisha alikotaka!
Yawaje kila mechi twende sote kileleni kama siyo gheresha zake?
Ukidhani mpo wote basi nawe kulainika na kujiachia!
Kumbe sasa umekuwa teja wa mbinu zake hadaa..
Hivi kileleni feki utakitambuaje?
Ukiona naye kakomesha vimbwanga vyake baada ya wewe..
Basi jua amekuchora na tafuta mbinu mpya ya kumkabili.......
Hakiki pumzi yake kama nayo imekatika ghafla...
Ukiona kanywea na akushurutisha ubanduke basi jua umeliwa.......
Hivi kileleni feki utakitambuaje?