Kingunge: JK ameitosa CCM - Katiba mpya

Kingunge: JK ameitosa CCM - Katiba mpya

Ileje

JF-Expert Member
Joined
Dec 20, 2011
Posts
9,524
Reaction score
13,682
Katika kipindi cha "Je tutafika" cha channel ten, Kingunge ameonyesha masikitiko yake kwa kitendo cha JK kuridhia kuanzishwa kwa mchakato wa kuandikwa kwa katiba mpya kwa sababu CCM haikuwa imejiandaa kwa mabadiliko ya katiba! Kingunge amedai kuwa CCM iliandaa sera za masafa marefu za 2000 - 2010 na 2010 - 2020 ambazo hakuna hata moja ilikuwa na mpango wa kuandika katiba mpya!

Aidha Kingunge ameishangaa Tume kupendekeza serikali tatu katika katiba mpya kwa kuwa haikuwa sehemu ya hadidu za rejea walizopewa Tume ya Warioba!

Kingunge amesema kitendo cha JK kuridhia kuanzishwa kwa mchakato wa kuandika katiba mpya ni surprise kwa CCM kwa kuwa haikuwahi kujadiliwa katika kikao cho chote cha CCM!

Naye Vuai Naibu katibu mkuu wa CCM (Zanzibar) aliyeshiriki katika kipindi hicho amesema kuanzishwa kwa serikali tatu ni pigo kwa Wazanzibari kwa kuwa kwa kiwango kikubwa Wazanzibari wamekuwa wanategemea Tanzania Bara kwa elimu, uchumi na shughuli za kijamii!! Amesema katika muundo wa sasa wa muungano Wazanzibari wamekuwa huru kufanya shughuli zao Tanzania bara bila bugudha zo zote!

Aidha Vuai amelaani slogan ya CUF huko Zanzibar inayosema "Tunataka nchi yetu"

Kingunge na Vuai wote wanadhani kitendo cha Warioba kupendekeza serikali tatu ni kuvunja muungano!

Tutafakari upya hoja zetu za serikali tatu au nne zinazopendekezwa wa Wapemba!!
 
Nampongeza mh Rais Kikwete kwa kuona kuwa maslahi ya Tz ni zaidi ya chama chake.

Kusema kweli amelielewa lileandiko linalo sema waache wafu wazikane wenyewe.Sera za masafa marefu mpaka 2020 kuna watu walikuwa hawaoni umuhimu wa katiba mpya!!!!!!

Nani kasema serikali tatu ni hoja ya Wapemba peke yao, kama hawajui wajue kuwa Watanganyika wako wengi tu wanaounga mkono hii hoja.
 
Katika kipindi cha "Je tutafika" cha channel ten, Kingunge ameonyesha masikitiko yake kwa kitendo cha JK kuridhia kuanzishwa kwa mchakato wa kuandikwa kwa katiba mpya kwa sababu CCM haikuwa imejiandaa kwa mabadiliko ya katiba! Kingunge amedai kuwa CCM iliandaa sera za masafa marefu za 2000 - 2010 na 2010 - 2020 ambazo hakuna hata moja ilikuwa na mpango wa kuandika katiba mpya!

Aidha Kingunge ameishangaa Tume kupendekeza serikali tatu katika katiba mpya kwa kuwa haikuwa sehemu ya hadidu za rejea walizopewa Tume ya Warioba!

Kingunge amesema kitendo cha JK kuridhia kuanzishwa kwa mchakato wa kuandika katiba mpya ni surprise kwa CCM kwa kuwa haikuwahi kujadiliwa katika kikao cho chote cha CCM!

Naye Vuai Naibu katibu mkuu wa CCM (Zanzibar) aliyeshiriki katika kipindi hicho amesema kuanzishwa kwa serikali tatu ni pigo kwa Wazanzibari kwa kuwa kwa kiwango kikubwa Wazanzibari wamekuwa wanategemea Tanzania Bara kwa elimu, uchumi na shughuli za kijamii!! Amesema katika muundo wa sasa wa muungano Wazanzibari wamekuwa huru kufanya shughuli zao Tanzania bara bila bugudha zo zote!

Aidha Vuai amelaani slogan ya CUF huko Zanzibar inayosema "Tunataka nchi yetu"

Kingunge na Vuai wote wanadhani kitendo cha Warioba kupendekeza serikali tatu ni kuvunja muungano!

Tutafakari upya hoja zetu za serikali tatu au nne zinazopendekezwa wa Wapemba!!

Mzee Kingunge hivi hajui kwamba wakati ni ukuta? Hivi mzee Kingunge hajui kusoma alama za nyakati? Inawezekana mawazo yake yamezeeka kama mwili wake.Akumbuke kwamba macho ya binadamu yana kikomo cha kuona na wanadamu waloanzisha muumgano huu hawakujua itakavyokuwa leo.Kikwete ameona mbali sana na maamuzi yake ni sahihi kabisa.
Namshangaa sana huyu mtu anayeitwa Vuai.kwa nini anailaumu Cuf wakati chama chake na serikali yake mwaka 2010 katika kuihuisha katiba yao walisema Zanzibar ni nchi? Au Vuai hajui maana ya nchi?
Mtu apende asipende,kwa wakati huu serikali tatu haizuiliki.
 
Hawa wote wawili ni MADEBE matupu na vichwani kuna TOPE badala ya Ubongo hasa Huyu Vuai wa Zanzibar anasema Zanzibar inaitegemea Bara kila kitu hata elimu. Ama kweli wana U-Pinda wote wawili
 
Weken serikal 2 lakin punguzen mambo ya Muungano tu, mukiweka 3 Itabid muweke 4 pia.
Hawa Kina Warioba wanajichanganya tu,
Mambo ya Muungano yawe 3 tu. Serikal ziwe 2. Kuepusha nchi moja kuwa na marais 6.5 nadhan tuwe makini sana.....

Lau kama mnatengezeana Ulaji tujue mapema tu.
 
Nampongeza mh Rais Kikwete kwa kuona kuwa maslahi ya Tz ni zaidi ya chama chake.

Kusema kweli amelielewa lileandiko linalo sema waache wafu wazikane wenyewe.Sera za masafa marefu mpaka 2020 kuna watu walikuwa hawaoni umuhimu wa katiba mpya!!!!!!

Nani kasema serikali tatu ni hoja ya Wapemba peke yao, kama hawajui wajue kuwa Watanganyika wako wengi tu wanaounga mkono hii hoja.

Mkuu unajua kunawatu mi nashangaa sana mara nyingi huwa niliamini kwamba Uzee ni hazina na kwamba kdri umri unavyoonge zeka ndivyo busara na uwezo wa mtu kupima jambo na kufanya uamuzi makini unaongezeka ila ninawasiwasi kwamba kuna wazee inawezekana wakawa wanazeeka vibaya.

Katika hili la katiba nadhani Mh.Rais Kikwete,Mzee Butiku,Mzee Warioba wamedhihirisha kwamba wanazeeka vizuri tatizo liko kwenye wahafidhina wachama hicho ambao kwanza hawataki kukubali kwamba wamezeeka na pia wameshindwa kusoma alama za nyakati
 
Hoja za Kingunge na Vuai kwa sasa hazina mshiko

MABADILIKO NI NDANI YA MABADILIKO J.K NYERERE
 
Hiv bado mnamsikiliza huyo Mzee Kingunge, ambaye anaamini hakuna Mungu, anajiona kuwa amejiumba mwenyewe.
 
Hiv bado mnamsikiliza huyo Mzee Kingunge, ambaye anaamini hakuna Mungu, anajiona kuwa amejiumba mwenyewe.

CCM watu wa ajabu sana, wanapenda sana matumizi ya makapi, ndiyo maana mambo yao vululuvululu tu. Fikiri ingekuwaje mzee kama huyu awe na final say kwenye jambo fulani nyeti, nchi inaweza kugeuka 'somalia'.

Historia haiishiwi wino.
 
Tusisahau kuwa wengi waliokuwepo Enzi za Mwalimu Nyerere walikua ni vichwa vitupu - akili ya kufukiri hakuna. Lakini kwa sababu za akili na uadilifu wa Mwalimu aliweza kulifunika hilo na kuwaaminisha watanzania kuwa mambo ni shwari. Angalia baada ya kifo cha Mwalimu. Ikawa ni wizi mtupu hadi leo. Kwa hakika rushwa wanayoiendekeza ndiyo itakayowamaliza.
 
Huyu Kingunge naona pesa za Parking System anazopata bure zimeaanza kumchanganya kibak huyu atuondoshee mauza uza yake silipendi sana hili... toto lake linabebesha watu madawa lenyewe limepewa pesa za jiji za parking mijini bado halilidhiki au anadhania sie tunafurahi? maegesho hata sehemu zisizo stahili yeye anatoza pesa.... huyu ni wa Motoni tu... kumdiskasi ni kama kosa kwetu...
 
unategemea nini kutoka kwa mtu asiyeamini mungu. totaly nothing. huyu anatakiwa kupumzika tu kule pugu ale upepo mambo ya politic awaachie kina lukuvi ambavyo ndo vichwa vilivyobaki ccm.
 
Back
Top Bottom