Kinyozi atupwa jela miaka 30 kwa kumpa mimba mwanafunzi

Kinyozi atupwa jela miaka 30 kwa kumpa mimba mwanafunzi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607

Mahakama ya Wilaya ya Iringa, imemhukumu kinyozi, Batista Ngwale (27) kifungo cha miaka 30 jela baada ya kumtia hatiani kwa kumpa mimba mwanafunzi mwenye umri wa miaka 18.

Binti huyo alikuwa akisoma kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya Kibena iliyopo Iringa Vijijini.

Binti aliiambia Mahakama kuwa alianza uhusiano na Batista, Mei 2021, alipopata ujauzito mtuhumiwa akamwambia atoe lakini binti huyo hakufanya hivyo.

Mashahidi 6 waliohusika katika kesi hiyo akiwemo Daktari wa Kituo cha Afya cha Ifunda.

Video: Azam TV
 
Hii mechanism ya Utoaji wa MVUA 30 kisha mtoto anaachiwa mtoto ili amlee peke yake tena katika umri mdogo pamoja na kukosa elimu na PESA naona imekaa vibaya.

Ushauri wangu ni huu:

Ukikutwa na uhusiano na Mwanafunzi,Upigwe mvua chache kidogo kisha uwekwe katika orodha ya sex Offenders n.k.Miaka 30 iachwe kwa FORCED RAPE.Ikishatokea MIMBA na Interest za muathirika zitazamwa au ikishindikana basi Kuwe na OPTION ya kufanya Abortion kwa BINTI na Mwamba akikaa JELA miaka 30 asimwachie mwenzake STRESS.

Binti mwenyewe wa miaka 18 anaoneka Ngubare
 
Hii mechanism ya Utoaji wa MVUA 30 kisha mtoto anaachiwa mtoto ili amlee peke yake tena katika umri mdogo pamoja na kukosa elimu na PESA naona imekaa vibaya.

Ushauri wangu ni huu:

Ukikutwa na uhusiano na Mwanafunzi,Upigwe mvua chache kidogo kisha uwekwe katika orodha ya sex Offenders n.k.Miaka 30 iachwe kwa FORCED RAPE.Ikishatokea MIMBA na Interest za muathirika zitazamwa au ikishindikana basi Kuwe na OPTION ya kufanya Abortion kwa BINTI na Mwamba akikaa JELA miaka 30 asimwachie mwenzake STRESS.

Binti mwenyewe wa miaka 18 anaoneka Ngubare

Sheria hii imekaa kukomoa bila kutoa suluhu kwa mtoto anayezaliwa wala mahitaji kwa aliyetiwa mimba.

Ni kweli kumpa mwanafunzi mimba ni jambo la kishenzi sana lakini mtoto anayezaliwa future yake inakuwaje? Serikali imejipangaje kwenye hili maana watoto wa mitaani na vibaka wanazidi kuongezeka
 
Sheria hii imekaa kukomoa bila kutoa suluhu kwa mtoto anayezaliwa wala mahitaji kwa aliyetiwa mimba.

Ni kweli kumpa mwanafunzi mimba ni jambo la kishenzi sana lakini mtoto anayezaliwa future yake inakuwaje? Serikali imejipangaje kwenye hili maana watoto wa mitaani na vibaka wanazidi kuongezeka
Uonevu tuu hii sheria kwani mwanamke kabakwa ata kama ni mwanafunzi, hajabakwa bana.

Na pia mbona mzazi wa mtoto hachukuliwi hatua? Na kama ulivyosema mtoto anayezaliwa mnamnyima malezi ya baba. Hii sheria waiangalie upya.
 
Back
Top Bottom