Kinyozi atupwa jela miaka 30 kwa kumpa mimba mwanafunzi

Mahakama ya Wilaya ya Iringa imemuhukumu kifungo cha miaka 30 Batista Ngwale (27) kwa kukutwa na hatia ya kumpa mimba Mwanafunzi mwenye umri wa miaka 18 ambaye alikuwa akisoma kidato cha nne katika Shule ya Sekondari ya Kibena iliyopo Iringa vijijini.

Batista alikuwa akijishughulisha na kazi ya kinyozi ambapo ameiomba Mahakama kumpunguzia adhabu kwasababu ana Ndugu watatu na Mtoto mmoja ambaye anasoma Shule ya awali ambao wote wanamtegemea, maelezo ya Mahakama yanaeleza kuwa Kijana na Binti walifanya mapenzi mara mbili vichakani huku Kijana akijua dhahiri kwamba Binti huyo ni Mwanafunzi.

Kesi hiyo ilikuwa na Mashahidi sita akiwemo Daktari wa kituo cha afya cha Ifunda ambapo Binti alipelekwa kufanyiwa uchunguzi na kugundulika ana ujauzito wa wiki nne, Shahidi wa tatu ni Binti ambaye ameiambia Mahakama kuwa walianza mahusiano na Batista Mwezi May na walijamiana Mwezi June na baada ya mwezi mmoja alijihisi mjamzito na alimtaarifu Mhusika na akamshauri watoe lakini Binti hakutaka kutoa mimba hiyo na siku alipofika Mahakamani kutoa ushahidi alikuwa ni mjamzito.

Kesi hiyo imesimamiwa na Mawakili wa Serikali Radhia Njovu,Simon Nashon pamoja na Reuben Lubango ambapo waliomba mahakama kutoa adhabu kali kwa sababu kitendo hicho cha kufanya mapenzi vichakani kinamfedhehesha Mwanamke, akisoma hukumu hiyo Hakimu Mkazi Mkuu Said Ally Mkasiwa amesema kwa kuzingatia athari za kukatisha masomo ya Binti huyo na kumpa ujauzito,Mahakama imemkuta na hatia na imempa kifungo cha miaka 30 huku akipewa nafasi ya kukata rufaa.
#MillardAyoMAHAKAMANI
 
Ngoja arudi akiwa na miaka 57 mbususu imemponza shenzi zake.
 
binti naye 18yrs ameshabalehe tayari, haja zake anatimiziwa na nani?.

Kinyozi angeozeshwa pamoja na kutoachana milele, siku akitoa talaka anakwenda jela, binti aendelee na shule akitokea kwa mme wake.

Wazazi tujitahidi vijana wasome na umri mdogo, hiyo 18yrs ni 2nd year chuo kikuu.
 
Sheria ya kikatili sana hii. Sijui bunge letu lilikuwa linawaza nini
 
Hii haijakaa sawa.

Kushiriki mapenzi kwa hiari na mwanamke mwenye umri wa miaka 18 ni kubaka!

Hii akipata wanasheria wazuri anatemwa.
 
Jela wanahesabu usiku na mchana siku mbili.

Atarudi na 27 + 15 = 42 years.

Hawahesabu usiku na mchana
Wanahesabu zao mtu anapunguziwa 1/3 ya kifungo chake maana yake anafungwa 2/3.

Kwa mantiki hiyo 1/3 ya miaka 30 ni miaka 10 maana yake atafungwa miaka 20

Ongeza umri wake atatoka ana miaka 47
 
Wanaharakati walisema hii adhabu ni ndogo, wanataka mwanaume akibaka na ikathibitika, basi ahasiwe ili asirudie kosa.
 
Nikwel mkuu vip hot balaa mm kuna kimoja nilianza kukichakata tokea kipo form two mpaka saiz kipo form4 yan kipo moto nihtr akijawai poa me nakimezesha p2
We mmezeshe p2 ila kumbuka akienda kwa boda boda hammezeshi p2 mzigo utakuja kwako unadhani una faidi tunda mwenyewe.
 
We mmezeshe p2 ila kumbuka akienda kwa boda boda hammezeshi p2 mzigo utakuja kwako unadhani una faidi tunda mwenyewe.
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ Ajal kazin mm mwenyew nibodaboda
 
Kubaka
Kuiba
Kuua

Haya mambo ni ya hovyo kabisa.

huyo hajabaka, Ila anaonewa tu. Inakuaje watu watongozane na wafanye mapenzi kwa ridhaa zao halafu uambiwe kabaka? Sheria za kipuuzi kabisa
 
Kubaka
Kuiba
Kuua

Haya mambo ni ya hovyo kabisa.
Kesi sio ya ubakaji bana ni kumpa mimba mwanafunzi. Kuna tofauti hapo.

Mtu wa miaka 18 kisheri sio minor so huwezi kusema alibakwa. The age of consent to sexual activity in Tanzania is 18 years.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…