LAZIMA NISEME
JF-Expert Member
- Apr 5, 2015
- 240
- 267
Kama alivyosema Mwanafalsafa Prof. PLO LUMUMBA kwamba Mnenguaji mzuri lazima ajue ni wakati gani wa kushuka kwenye Jukwaa ("A good Dancer must know when to leave a stage") imekuwa tofauti kwa Mwanasiasa Tundu Lissu ndani ya CHADEMA.
Akihojiwa na moja ya Chombo cha Habari hivi Karibuni, TUNDU LISSU alishangazwa na kauli ya Msemaji Mkuu wa CHADEMA, JOHN MREMA kutokuwa na taarifa juu ya nia yake ya kuwania nafasi ya Urais katika Uchaguzi Mkuu Ujao na U- Makamu Mwenyekiti wa Chama katika Uchaguzi unaotarajiwa kufanyika miezi michache ijayo. LISSU alinukuliwa akisema ".... Hilo sasa waulize wahusika, lakini nakuambia siku unazungumza na Bwana MREMA, Karibu Mkuu wa Chama (John MNYIKA) alikuwa tayari ameshapata hizo barua za kusudio la Makamu Mwenyekiti na Rais"
Nini Maana Yake?
VIONGOZI wa CHADEMA wameshasoma alama za nyakati kuwa, LISSU hahitajiki na Wanachama wa CHADEMA kutokana kutokana na matendo yake. Baadhi ya Tabia zinazopunguza Umaarufu wa LISSU na kutohitajika na wanachama nazitaja hapa chini:-
Mosi, Uwanaharakati. LISSU amekuwa amekuwa akitiliwa shaka kutokana na ukaribu alionao na baadhi ya Mataifa ya Magharibi hali inayowapa taabu wanachama wa CHADEMA kuendelea kumuamini kushika nafasi za juu za maamuzi.
Pili, Uropokaji. LISSU anashtumiwa kuwa na tabia za kuropoka mambo mbalimbali pasipo kuyafanyia Uchunguzi. Tabia hii imekuwa ikiwakera wanachama na Viongozi wengine ndani ya Chama.
Tatu, Kukosa Uzalendo kwa Taifa lake. LISSU ni Kiongozi ambaye hana Uchungu na Taifa lake na Chama chake. Kama ambavyo alikimbia kupambania Chama kwa miaka kadhaa hata baada ya kupona.
Nne, Dharau na kujiamini kupita kiasi, jambo ambalo limekuwa likisababisha kukaidi maelekezo mbalimbali ya Chama na kumdharau Mwenyekiti wa Chama Taifa, Freeman Mbowe. Hali hiyo imekuwa ikisababisha kujitokeza kwa makundi yanayokipasua chama.
Tano, Sera za Ushoga: Ni moja ya eneo linalomuondolea TUNDU LISSU sifa kwa kuwa, vitendo vya namna hiyo haviungwi mkono na Jamii ya Kitanzania kwa Ujumla. Ambapo, wanachama wengi wa CHADEMA wanaona kuwa endapo LISSU atachaguliwa kuwa Rais wa Nchini, anaweza kuwa kinara wa kuharibu tamaduni za Kitanzania ili kuwafurahisha mabeberu.
Katibu Mkuu MNYIKA shikilia hapo hapo, sikiliza sauti za sisi Wanachama wako. Utakuja kutushukuru baadaye.