Kiongozi wa CIA atangaza Marekani kusitisha kuipa Ukraine taarifa zozote za kijasusi na za kiusalama zinazohusiana na vita

Sasa kumbe ukreni ushiriki wake ulikua eneo Gani katika hii vita kama Hadi taatifa za kiinterejesia zilikua zunatoka USA na nchi nyingine washirika?
Hujui kitu wewe nyamaza hata wewe huwezi kuwa vitani na unaweza kupata taarifa zote kwa usahihi. Lazima ulipe watu wafanye kazi hizo. Military intelligence ni tofauti na battlefield intelligence (IPB).
 
Hujui kitu wewe nyamaza hata wewe huwezi kuwa vitani na unaweza kupata taarifa zote kwa usahihi. Lazima ulipe watu wafanye kazi hizo. Military intelligence ni tofauti na battlefield intelligence (IPB).
Mzeeenuki deep hawajui hao labda uwafungulie code
 
Kisa kukataa kuwapa madini.

US imekuwa taifa la hovyo
 
Kwa iyo unamsema Yeriko nyerere, kila kitabu chake cha Moscow.............
 
Dah sasa kwanini lakini..US hawana huruma kabisa si watasababisha Ukraine Ipigwe kama paka mwizi
 
Hiyo kauli ilikua ni kabla USA na NATO hawajaingia kuisaidia Ukraine.
Na kwa hiyo Kiev haikuanguka kwa sababu ya misaada kama hiyo.
Sivyo. Biden alimpa Zelenskyy taarifa za kiinteljensia kuwa Urusi tayari iko hatua za mwisho kuvamia Ukraine na kuichukua “in a matter of days” akamshauri aondoke haraka sana na familia yake kwani wao ndio target namba moja ya Putin kutesa na kuuawa. Marekani walishampangia msaada wa kumtoa Kyiv.

Zelenskyy akasema NO; watapigana. Akaomba msaada wa silaha. Kuanzia wakatumia javelin walizokuwa nazo tayari; walizopata toka utawala uliopita wa Trump na kuzitumia kusambaratisha msafara wa vifaru, malori, na mizinga ya Urusi iliyokuwa ikielekea kuzingira Kyiv na helikopta zilizokuwa zikifanya mashambulizi sehemu mbali mbali.

That was the turning point.

Marekani walipoona Ukraine wameweza kutimua majeshi ya Urusi toka Kyiv na sehemu zingine ndipo wakajua jamaa wako serious. Ndipo mpango mzima wa NATO kutoa misaada ya silaha na intelijensia ikaanza kufanyika chap chap.

Nchi za Magharibi tatizo lao kubwa ni wapiganaji (boots on the ground). Sio pesa wala silaha. Hawako tayari kumwaga damu ya watu wao kirahisi rahisi tu. It’s too valuable. Ndio maana waliishia kukimbia Afghanistan na kwingineko walipoona hakuna mafanikio.

Kwa Ukraine hilo tatizo halikuwepo. Wenye nchi yao walikuwa tayari kumwaga damu yao kwa nchi yao. Shida yao ilikuwa ni uwezo mdogo wa kiuchumi. Hivyo walihitaji silaha, teknolojia na gharama zinazohusika.
 
Tatizo ni Zelensky hajui siasa za US hapo mpaka wamuondowe madarakani ndo maelewano yaanze upya na hawatashindwa kumuondoa alicho fanya ni ujinga kubishana na trump hadharani.
Tatizo si zelensky, yeye anapigania nchi yake, siasa za marekani inategemea na rais aliepo. Akitoka trump atakuja mwingine si ajab akarudisha misaada

Siku europe iki terminate msaada kama huo kwa ukraine ndipo hali itakuwa mbaya zaid kwao.
 
Bangi zimemzidi. Uko vitamin halafu kiongozi unaongoza kwa kuvuta bangi......lazima kichwa kiende resi
 
🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣😂😂😂😂😅Ma alikiabakisifiwa sana na wapenda vita humu.
Mambo nyewe ukiyasikiliza utachoka😂😂😂kule trampo kashawahi kuropoka kua askari wa nchi za umoja wa ulaya waliokua ukreni hawataendelea kuhudumiwa chini ya NATO 😁😁😁 inaonekana hata ground Kuna mambo watu hawataki kufunguka 🤓Aya bhn sie yetu macho
 
Tatizo si zelensky, yeye anapigania nchi yake, siasa za marekani inategemea na rais aliepo. Akitoka trump atakuja mwingine si ajab akarudisha misaada

Siku europe iki terminate msaada kama huo kwa ukraine ndipo hali itakuwa mbaya zaid kwao.
Akitoka trampo akiingia rais mwingne atakayerudisha iyo misahada nistue ,Kuna million mbili zako zipo kwangu😂
 
Kwa lugha nyingine urusi inapigana na Marekani kupitia mgongo wa Ukraine...


Cc: Mahondaw
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…