Kiongozi wa Iran Ayatollah Khamenei, anafanya kosa kubwa kwa kutangaza wazi mahali na muda wa hotuba yake

Kiongozi wa Iran Ayatollah Khamenei, anafanya kosa kubwa kwa kutangaza wazi mahali na muda wa hotuba yake

Hana haja ya kuogopa kifo maana mwislamu kufa ni ibada😃 na kichapo kitaendelea hata wakiua viongozi.
Kimsingi, hakuna anayeogopa kifo. Kinachoogopwa ni kutangulia kufa. Hata Ayatollah wa Iran kuna wakati huwa anapelekwa kwenye secure location akiamini kuwa ndio sehemu salama zaidi.
 
Ayatollah kwa Iran ni zaidi ya rais. Ukimshambulia umetangaza vita ya moja kwa moja na Iran.
Israel haihitaji kumshambulia Ayatollah ili itangaze vita ya moja kwa moja na Iran. Hizo nchi mbili tayari zilishatangaziana vita zamani sana (de facto war).

Kitendo cha kushambulia ubalozi wa nchi ni tangazo tosha la vita dhidi ya nchi husika. Wala hauhitaji hata kusaini document yoyote ile.
 
Nimeshangaa sana kusoma taarifa kuwa kiongozi huyo anatarajia kutoa hotuba leo Ijumaa wakati wa swala ya Ijumaa kwani anajiweka katika hatari ya kushambuliwa na majeshi ya Israel kama ilivyokuwa kwa viongozi wakuu wa Hesbolah na Hamasi(asijiamini sana kiulinzi, lolote laweza tokeo)

Bado inaweza isiwe leo, ila hapaswi kuendelea kufanya hivi kwa siku za usoni kwani wanaweza kumla kichwa( Netanyau ni mental case).

Nieleweki kabisa kuwa Siwapendi wa Israel kwasababu moja kubwa: kuwaonea wapalestina na kuwaua hovyo kama wanaua kuku au panya. Hawana ubinadamu kabisa na wanajiona wao ni binadamu wa daraja la juu kulinganisha na wapalestina wanaowaona kama sio binadamu.

Kwa msingi huo, nisingependa kuona Israel anafanikiwa katika vita yake na Iran na ndio maana namtahadharisha Ayatollah asijaribu kujianika maana Israel huwa hawajali nini kitatokea baadae(hawapimi maamuzi yao) la muhimu kwao ni kutaka kuonyesha dunia kuwa wao ni bora kivita katika hilo eneo lote la Mashariki ya Kati.

Kwahiyo, hawatasiita kumshambulia Ayatollah kwa kushitukiza sambamba na kushambuliwa vituo vya kijeshi na nuclear facilities za muajemi pamoja na kushambulia raia kwa kushambulua mfululizo kuhakikisha Iran hapati muda wa kujipanga.

Mpaka sasa Israel ameshaona uwezo wa Iran na hatari iliyopo kuingia nae vitani. Hivyo, njia pekee ya kupambana nae ni kuanzisha mashambulizi ya non stop (full blown war) jambo ambalo linaweza kuwafanga Iran watumie unconventional weapons kama vile sila za nyuklia na hii ndio hatari ambayo mmarekani ameshaiona.

Kwa kifupi, Israel alijaa sana kiburi hasa baada ya kuua viongozi wa Hamasi na Hesbolah huku Iran akiwa katulia, ila sasa kiburi hicho mbele ya Iran hakitavumiliwa tena na unaweza kuwa ni mwanzo wa janga la kibinadamu katika hilo eneo. Dunia ikizembea, tunaweza shuhudia vita ya tatu ya dunia kiutani utani tu.

Muda utaongea.

NB: Kuingia katika vita au kuendelea kupigana vita wakati kiongozi wa juu wa nchi ameuwawa au kujeruhiwa, ni disadvantage kubwa sana na ni advantage kubwa sana kwa adui na Israel huenda anapanga kufanya jambo kama hili akijua faida ya kufanya hivyo.
Hakuna kitu kibaya kama kumuua kiongozi wa dini wa kishia.
Israel ikithubutu hakuna rangi itaacha kuona.
 
Hakuna kitu kibaya kama kumuua kiongozi wa dini wa kishia.
Israel ikithubutu hakuna rangi itaacha kuona.
Shia wakorofi sana , Indonesia imekuwa na nguvu kwa sababu yao .....Wkimuua wajiandae ya matukio ya watu kujitoa muhanga ..
 
Kimsingi, hakuna anayeogopa kifo. Kinachoogopwa ni kutangulia kufa. Hata Ayatollah wa Iran kuna wakati huwa anapelekwa kwenye secure location akiamini kuwa ndio sehemu salama zaidi.
Muda wake ukifika atang'oka tu ila sio kwa mapenzi ya Nyauba aina ya Neta
 
Back
Top Bottom