Kipa Gani wa Simba mkali zaidi kuliko wote tangu -labu ilipoanzishwa?

Hii survey sio ya kiufundi. Kuna mtu hapa amewahi kuwaona wote toka klabu ianzishwe?

Mimi sijawahi, nimeanza na era ya Moses Mkandawile na kuendelea, hivyo siwezi na sitaki ku comment kuhusu kina Mambosasa na Mahadhi.
Kaangalie video clips zao
 
Mimi nimewaona wote.laivu,na kipa anayemkaribia kidogo mahadhi atakuwa Isega Isindani(wa yanga).
 


...Omar Mahadhi 'Bin Jabir' ni huyo wa pili kulia!...mnyama mkali miaka hiyo, mnamuona Moh'd Bakari 'Tall', Abdallah 'King' Kibaden, Abdallah Mwinyimkuu, Adam Sabu, Abubakar Salum 'Bruce Lee,' etc...

Abdallah Kibaden siku moja nimemwona kwenye clip ya TBC1 ya habari enzi hizo anapokea zawadi kama mwanamichezo bora wa kiume, na huyu Omar Mahadhi ndo baba yake Wazir Mahadhi halafu naona kama Mambosasa na Iddi Pazi wanavuma zaidi hata huyu Juma Pondamali naye anavuma sana.
 
Marehemu Omar Mahadhi Bin Jabir ndie the greatest Tanzanian goalkeeper of all time. Hakuna ubishi. Wengine ni wazuri lakini huyu ndio baba lao.
 
Kaangalie video clips zao
Wapi?

Mkubwa, Simba imeanzishwa mwaka 1936, nikaangalie video clip za Simba toka mwaka 1936 ziko wapi? Hii survey haijaenda shule kwa sababu watu wanaongea kama vile walikuwepo mwaka 1936. Katika makipa wa Simba uliowahi kuwaona, ni yupi unaeona mkali zaidi, hapo tungeelewana.
 
Mpigie simu Rage na muulize atakupatia clips zote unazohitaji
 
Napita tu wakuu maana mie nipo Jangwani ila frankly speaking Msimmbazi mmejaaliwa kuwa na makipa..... nilimkuta mkandawile ambaye hakuwika sana lakini Iddi Pazi, Mwameja na Kaseja..... Mh! Chiboko..... Namheshimu zaidi kaseja kwani ndo ammetunyima usingizi jamgwani hadi tukamsajili ili walau tuondoe nuksi ya kuchapwa mfulilizo.....
 
Nillibahatika kuwaona akina Hassan Mlapakolo, Athumani Mambosasa, Omari Mahadhi, Iddi Pazi na wengine waliofuatia. Hakika MAHADHI aliyesajiliwa na Simba kutoka African Sports ya Tanga mwaka 1975, ndiye kipa bora wa wakati wote wa SIMBA SC. Mwaka huo pia alisajiliwa Mohamed Bakari Tall kutoka Cosmo ya Dar na kutengeneza ukuta mgumu sana ambao waandishi wa michezo wa wakati huo akina Mwamoyo Hamza (Daily News) walikuwa wanauita ukuta wa Berlin. Kwa miaka mitano mfululizo tangu wakati huo Yanga walichezea kichapo kutoka kwa Simba, ikiwemo kichapo cha 6-0 (1977).
 
...Omar Mahadhi 'Bin Jabir' ni huyo wa pili kulia!...mnyama mkali miaka hiyo, mnamuona Moh'd Bakari 'Tall', Abdallah 'King' Kibaden, Abdallah Mwinyimkuu, Adam Sabu, Abubakar Salum 'Bruce Lee,' etc...
"Bruce Lee" ni jina alilopewa Daud Salum sio Abubakar Salum. Abubakar Salum ni "SureBoy"
 
Nimeanza kufuatilia soka mwishoni mwa miaka ya themanini, toka kipindi hicho kwa wachezaji niliowaona mwenyewe bila kusimuliwa au kusoma kwenye magazeti Mohamed Mwameja ndiye kipa bora kabisa. Kwa mafanikio binafsi, kwa kuisaidia timu na mafanikio ya kiujumla kitimu Mohamed Mwameja was the greatest. Hao wengine wa miaka ya sabini tunawasoma kwenye magazeti.


Nikitoka nje ya mada kidogo, kuna kiungo mchezesha timu alikuwa Simba miaka ya mwanzoni mwa tisini, huyu jamaa hakika kiuwezo huwa namfananisha na mzee mzima, Zinedine Zidane. Hapa namzungumzia kocha mchezaji Hassan Afif, huyu jamaa sijui yuko wapi ? Alikuwa very talented na creative play maker japo hakukaa sana na Simba.
 
Daima kipa bora amekuwa akitoka SSC, ndio maana hata wenzetu wa Yanga waliwahi kuwa na makipa 3 ambao kuna nyakati wote kwa pamoja walikuwa Simba msimu mmoja, yaani Juma Kaseja, Ally Mustapha na Deogratius Munisi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…