Kipa Simba Angban, amchapa ngumi Kessy

Huyu Kessy Ni Jipu Lililotukuka Na Sasa Baada Ya Yeye Kumwaga Mboga Sisi Mashabiki Tunamwaga UGALI Na Niombeeni Tu Nitaweka Kila Muamala Wake Aliotumiwa Na Viongozi Wa Upande Wa Pili.

Anakuja Yanga huyo mikia endeleeni kulalamika
 
Wapo wachezaji waliokosa magoli ya wazi mf Mgosi.Jamaa kichwa cha ovyo akilitazama goli,wakati Deo alishapotea. Acheni kumsakama Kessy,huo ndo uwezo wa mikia.
 
Wanamuonea tuu kessy mwenyew aliondoka washapigwa goli tayar, asa cjui alijifunga yy!!
 
Eti oooooooh kuna miamala nitaweka hapa iliyokuwa inafanywa kati ya Viongozi wa Yanga na Hassan Kessy, ajabu hatuoni hiyo Miamala. Simba acheni kumtwika huyo dogo lawama, kuna yule Awadhi Juma yeye na kipa alishindwa kufunga mlitaka Kessy akamshike kichwa Awadhi ili mpira ulenge golini!!!!!!!! Tatizo la Simba kufanya vibaya sio la Kessy tafuteni chanzo cha hili tatizo, lakini si ajabu simba kufanya vibaya, mbona Barca inafanya vibaya lakini hatusikii lawama wakivishwa akina Dan Alves!!!!
Simba huu mchezo hauitaji hasiraaa
 
Kizunguzungu! Sioni tatizo la Kessy japo amekua akifanya maamzi yenye mashaka.Alimpasia Ngoma & na kadi ya J2 inatia shaka maana alikuwa peke yake angeweza kujihadhari.Tatizo lipo kwaamzi watz maana ni mashabiki kama sisi tu.
 
itakua kisasi cha tangu simba na Yanga ...
 
Nini ngumi? Alitakiwa apigwe na mitama
 
Kwa mtindo huu michezo ya kimataifa wasahau
 
Hakuna cha kutumiwa, mbona akina Awadhi Juma wamekosa magoli ya wazi lakini hamsemi!!!!
kuna mambo kadhaa kwa tuliokuweo mpirani yanahitaji utafiti wa kina sana

  1. si kawaida ya Kessy kutoa krossi fyongo kiasi kile, nyingi zilikua za makusudi kabisa kwa sababu alikua anainua macho na kupiga atakavyo
  2. Kuna pasi alipewa na Mwalyanzi mpira wa kupress tu akasubiri udunde mara mbili dhahir akimsibiri kipa asogee si kosa kama ile ya msuva maana msuva alitaka kumchambua said mohamed lakini kipa akacheza na macho ya mpigaji
  3. Kessy alipokoromewa na Mgosi nilishuhudia na yeye akikoroma huku akijua Mgosi ni nahodha wa siku na timu na hata Kiiza alimfuata na akaondoka eneo la tukio bila kumsikiliza
  4. Kessy alikua wa kwanza kutoka vyumbani wakati wa mapumziko nilitafsiri kwamba huenda hakutaka lawama zaidi toka kwa wenzake maana baada ya maelekezo ya kocha wakati wa mapumziko wachezaji hulundikana kusemeshana mawili matatu
  5. Dakika mbili tu baada ya kipindi cha pili Kessy alichukua mpira ambao angeweza kuucheza muda mnrefu sana na matokeo yake akauandaa sana hadi mchezzaji wa Toto aliposoge na akapiga mpira kwa kuugandisha muu jambo ambalop ni gross misconduct katika soka, wapenzi wa simba wanasahau kwamba hili lilikua tukio la pili linalofana na hilo kwa mchezaji yue yule kipindi cha kwanza
  6. Dhahiri Kessy amenondoka mchezoni kwa kutojua mustakabali wake ama kwa kusubiri muda wake uishe huenda ana dira yake tayari
ni kweli kwamba samaki mmoja akioza wote wameoza, na kwamba meli inakwenda mrama na si vyema sana kumtuhumu mchezaji mmoja mmoja ila kuna mahali inabidi utumie circumstantial evidence for justification

kama ukitaka na wengine pia mfano unamzungumzia Awadh lakini hata Kiiza alikosa bao la wazi kabisa....any way iwapo ni kweli Kessy amefanya maamuzi binafsi namtakia kila la heri ila si kwenda kwa nafasi ya Juma Abdul ambaye ameiva sana katika nafasi yake na kuna mengi ya ziada ambayo itakua ngumu sana kupoka nafasi yake
 
Tayari kimenuka
 

Attachments

  • 1461046099190.jpg
    33.1 KB · Views: 35
Makosa yote anayofanya Kessy ni ya kimpira. Sidhani kama kuna influence yoyote ya maslahi binafsi au kutumiwa na upande wa pili.

Kwa wachambuzi makini katika mechi ngumu na zenye pressure, Kessy bado ni liability kwa Simba na anahitaji angalau misimu 2 kufikia ubora wake halisi wa kisoka. Ana kipaji kikubwa, moyo wa upambanaji, kasi, work rate nzuri na kutokata tamaa. Lakini mapungufu makubwa aliyonayo ni kiburi, kupaniki ovyo, hajifunzi haraka na pia hafanyi maamuzi sahihi kwa wakati sahihi, mfano kupiga krosi au chenga kwa wakati sahihi.

Kama anamoyo wa kuendelea kuichezea Simba, anapaswa kupewa muda na kusaidiwa zaidi ili apevuke. Naamini Simba wakiwekeza kwake hawatajuta na taifa litamfaidi muda si mrefu. Ila kama na yeye analeta issue za kuzirazira bila kukubali makosa na kujifunza zaidi, asepe zake akatafute maisha atakako.
 
NAISIKITIKIA SANA SIMBA YANGU. TIMU YOTE KUACHA DANNY LYANGA NA MKUDE HAIKUONYESHA UPAMBANAJI WA KWELI KAMA MECHI ZA NYUMA. KROSI ZA MOHAMEDI HUSSEIN NA KESSY ZILIKUWA ZA HOVYO KABISA SIJUI MAKOCHA HUWA WANAWAFUNDISHA NINI MAZOEZINI LAKINI HATA MECHI ZA ULAYA HAWATAZAMI? HATA KROSI SHUTI ZA CHINI ZA KUCHONGANISHA BEKI AJIFUNGE WALISHINDWA KUPIGA? KARIBU TIMU NZIMA NA BENCHI LA UFUNDI LILICHANGANYIKIWA NA KUKOSA NIDHAMU WAKABAKI WANACHEZA NA REFA MUDA WOTE WA MCHEZO AMBAO WALIKUWA WAMEUTAWALA KWA ZAIDI YA 50% NA WANGETULIA WANGEWEZA KUSAWAZISHA NA KUPATA USHINDI. AGBAN ALIRUDIA MAKOSA YAKE YA KUTOKA SANA NA NDIO MAANA ALIFUNGWA GOLI LA HOVYO KABISA NA HII HAIMPI NAFASI YA KUMTANDIKA KESSY AMBAYE ALICHEZA RAFU YA HOVYO KABISA AMBAYO HATA MIMI NAJIULIZA NI BAHATI MBAYA AU NI HUJUMA? HAPO NDIPO NAKUMBUKA UMUHIMU WA CHOLO KWANI JAPO UWEZO UMEPUNGUA KIDOGO LAKINI ALIKUWA NA MOYO WA KUIPIGANIA SIMBA. USHAURI WA BURE KWA VIONGOZI WA SIMBA BADALA YA KUKIMBILIA KUSAJILI TU MCHEZAJI MZURI JARIBUNI KUTAFUTA HISTORIA KIDOGO YA MCHEZAJI NA MUWE MNAWAFUTILIA BAADA YA KUWASAJILI VINGINEVYO TUTAENDELEA KULIA KILA MWAKA KWANI NIKIHESABU POINTI 6 ZA YANGA NA TOTO NAAMINI SIMBA INGEKUWA KATIKA NAFASI NZURI KWENYE MSIMAMO WA LIGI.
 

Tatizo la Simba ni kukataa kuukubali ukweli huu:
1. Tangu Kaseja aondoke, Simba haijawahi kusajili kipa wa maana
2. Simba imekuwa ikicheza bila ya kuwa na kocha.

Rekebisheni hayo mambo mawili, Inshaallah mwakani mnaweza kupata angalau FA.
 
Viongoz wa timu kwa kuua soo wanamtoa kafara kijana wa watu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…