Tresor Mandala
JF-Expert Member
- Aug 20, 2010
- 40,905
- 86,203
Miaka 15 ya Wale jamaa wa Mjengoni, 88.5.
==========
==========
Leo Nimewasikia hawa watangazaji wabunifu na Machachari wa Radio hii ya Clouds FM ambao waliacha kazi muda mrefu sasa. Waliitwa kwa ajili ya kuadhimisha Miaka 15 ya kituo hicho tangu kuanzishwa kwake.
Nimependa uongozi wa Clouds, pamoja na tofauti zilizowahi kuwakumba baina yao, kuamua kuwaalika hawa watu kwa kuwa walikuwa na mchango mkubwa sana enzi hizo.
Nani Hakumbuki enzi za Anko Masoud kwenye kipindi cha watoto akiwa na Kaka Bonda pamoja na Marehemu Amina Chifupa? Nani amekisahau kisauti maridhawa cha Fina Mango pale Kati?
Happy Anniversary Clouds Media - Viva forever!