Kipato changu kwa mwezi ni 150,000/- nipeni mbinu ya ku-save nami niondokane na umasikini wa kipato

Kipato changu kwa mwezi ni 150,000/- nipeni mbinu ya ku-save nami niondokane na umasikini wa kipato

Sigara Kali

JF-Expert Member
Joined
May 28, 2017
Posts
3,623
Reaction score
8,442
Najua hili sio jukwaa la uchumi ila kutokana na unyeti wa jukwaa hili maana naamini ndio jukwaa linaloongoza kutembelewa zaidi na watu mbalimbali mmoja wapo Mimi

Sasa kama mada inavyojieleza, kutokana na hali halisi ya maisha na ugumu wa ajira nilipata mchongo flani ambao salary yake ndo hiyo kwenye title

Kiukweli hii pesa kila nikiipata naona kabisa nashindwa kuweka akiba, manake hali ya kujitegemea inanigharimu, Kodi ya nyumba, kula, na masuala mengine ya kiafya

Nimewaza namna ya kujibana Ili nitunze kidogo kidogo nipate japo mtaji wa kuuza pipi,karanga ,sigara na hata pombe za kupima•

Sasa wale wajuvi wa mambo ya kifedha hasa matajiri wa hapa MMU nipeni techniques za kuweka akiba kutokana na hiki kipato ninachoingiza kila mwisho wa mwezi.

Kama huna ushauri mzuri bora upite kimya kimya sitaki kejeli hapa
 
Hapo we fikiria kuongeza kipato ila kusave hio pesa otherwise uwe na kipato hicho ila unausaidizi wa huduma zako za msingi /basic needs ili hio pesa isiguswe
 
Mmmh hata mungu nadhan anawashangaa viumbe aliowaumba mwenyewe but wanaume wengi hawafundishwi maana halisi ya kuwa mwanaume, mtt anakuwa Kwa kulelewa na mama bila malezi ya Mzee au mzee yupo ila MTT wa mama sana hadi wanaanza kupiga umbea na anakoleza chumvi kabisa. Hii ndio khasara yake mtt hana maamuzi mpangilio wa maisha na msimamo juu ya familia yake na maisha kiujumla.

OK anyway nikujibu swali lako kwa kutumia hela unayopata tu. Kwanza unapaswa kujua unatumia shs ngapi siku au mwezi, mfano kwa mwezi chakula ni 60,000 then kodi ni 20000 na bil maji umeme 10000 na mengineyo kama vocha 10,000 jumla ni kilo so reminder ni 50,000. Next month chukua hio 50,000 nunua chakula ndani ambacho kitaisha after 2 months na uanze kupika mwenyewe then after those two months utakuwa na akiba isiyopungua 120,000. Then just keep going after mwaka mmoja wa kujinyima una utakuwa na akiba almost laki 7😎
 
Mmmh hata mungu nadhan anawashangaa viumbe aliowaumba mwenyewe but wanaume wengi hawafundishwi maana halisi ya kuwa mwanaume, mtt anakuwa Kwa kulelewa na mama bila malezi ya Mzee au mzee yupo ila MTT wa mama sana hadi wanaanza kupiga umbea na anakoleza chumvi kabisa. Hii ndio khasara yake mtt hana maamuzi mpangilio wa maisha na msimamo juu ya familia yake na maisha kiujumla.

OK anyway nikujibu swali lako kwa kutumia hela unayopata tu..... Kwanza unapaswa kujua unatumia shs ngapi siku au mwezi...mfano kwa mwezi chakula ni 60,000 then kodi ni 20000 na bil maji umeme 10000 na mengineyo kama vocha 10,000 jumla ni kilo so reminder ni 50,000.... Next month chukua hio 50,000 nunua chakula ndani ambacho kitaisha after 2 months na uanze kupika mwenyewe then after those two months utakuwa na akiba isiyopungua 120,000. Then just keep going after mwaka mmoja wa kujinyima una utakuwa na akiba almost laki 7.........[emoji41]

Ngumu sana kama yupo mkoani anatoboa ila sio kwa dsm aseee
 
1. Bana matumizi kadri uwezavyo: Chakula kwa siku isizidi 2,000.

2. Kama una Smartphone jifunze skills ndogondogo kama kutengeneza matangazo kwa kutumia simu ( hii inaweza kukupa kipato cha ziada angalau 60,000 au zaidi kwa mwezi.

3. Hakikisha unaweza akiba kwanza kisha pesa inayobaki ndio utumie: KWa hapo ikiingia 150,000 ( fumba macho chukua 50,000 weka).

4. Sahau kuhusu anasa au marafiki wanaopenda anasa.
 
Nenda feri kanunua pweza ,kamba,ngisi uuze jiono hadi usiku kwenye bize roads hutokola hela nzuri

Niliwahi vijana wawili wanafanya hii biashara

Wa kwanza wako shekilango stendi hata ukienda utawakuta

Wengine wako pale mlimani city 5N pub wana supu tamu sana pweza ngisi naadudu fulani bahari matu sana

Ningeukuwa niko dar ningepiga biashara

Ningetafuta kibanda chakisasa mobile usikutu masaa 5 napiga biashara nasepenq kibanda
 
1. Bana matumizi kadri uwezavyo: Chakula kwa siku isizidi 2,000.
2. Kama una Smartphone jifunze skills ndogondogo kama kutengeneza matangazo kwa kutumia simu ( hii inaweza kukupa kipato cha ziada angalau 60,000 au zaidi kwa mwezi.
3. Hakikisha unaweza akiba kwanza kisha pesa inayobaki ndio utumie: KWa hapo ikiingia 150,000 ( fumba macho chukua 50,000 weka).
4. Sahau kuhusu anasa au marafiki wanaopenda anasa.
Matangazo wateja unapatia wapi?
 
Kabla ya yote unatakiwa uwe na malengo yako, unataka kusave kwa muda gani? je ni miezi 6 au mwaka au miaka?

Fahamu sababu zinazokufanya u save pesa,je unataka ufungue biashara,au unataka ununue chombo cha usafiri?

Ukishafahamu target yako (labda target n 1 year) hapo sasa piga kazi ndani ya mwezi ukipokea pesa,kaa ndani tuliza akili..

Mkononi una 150k.. Jiulize matumizi yako makubwa n nini? najua kubwa n Malazi(kodi) na msosi.. Afya n muhimu ila kwenye mwanzo mgumu wa namna hii afya Muachie Allah....

Ukishajua matumizi yako makubwa n kodi na chakula,jiulize Unaweza kuondoa kipi kati ya hivyo viwili ili kibaki kimoja?

Jibu chakuondoa n Kodi,sasa utaishi wapi? Hapa sasa ndio ule msemo wa Maana halisi ya maisha unatokea eneo hili, Hapo Rudisha room ya watu..

Kama ulikua na vitu Uza vyotee bakiza nguo zako na begi tu kama mwana apolo,vitu utanunua huko mbeleni saivi havina maana yeyote maana hata kama una hotpot huna uwezo wakupka hata wali nusu uweke so hapa Ondoa mzigo uliokuganda.

Ukishauza kila kitu ukabaki mweupe n wewe begi lako na nguo zako ndani,sasa Rudsha chumba cha watu, Chukua siku 1 anza kuzunguka huko kwa vijana wanaopga kazi either wabeba tofali au au zege au mizigo ilmrad wawe vijana wapga kazi kweli unawaona.

mfate mmoja wao au waite wote waambie ndugu zangu mimi n mwanaume mwenzenu,nmekuja Mjini sina pa kuishi ila nmekuja kufanya kazi na nimepata kazi sehemu naomba mnifadhili pakulala tu walau mwezi huu tu,nkipata kodi nitahamia kwangu nikapange..

Amini nakwambia ktk lile kundi hatokosekana mmoja mwenye imani maana umeshawambia ukweli kuwa umekuja kutafuta maisha na unaomba pakulala tu.

Utakubaliwa nina uhakika uspokubaliwa zunguka sehemu nyngine na nyngine hadi utakapokutana na yule mtu ataekuelewa,Yupo Mkuu Yupo nina uhakika 100% ujue tu namna yakujieleza na uwe mstarabu.

Ukipata pakulala sasa kipengele ktabaki kwenye msosi, eneo hili nalo si la kucheza nalo linapoteza hela haswa,sasa hakikisha marafiki zako n kina mama ntlie na usijifanye much know kuwa mkweli ukienda kwa kna mama ntlie nunua ukoko ule mzuri utauziwa,siku moja moja ule vizuri ili usipoteze afya ule vtu vya kukupa afya TU.

ishi kwa malengo naamini kwa mwezi mzima utaweza save walau 100k kama kweli utakua na akili zile za mtafutaji wa maisha,aibu acha,ukipewa chakula maswala ya kuzuga umeshiba eti unasema Asante Acha ukipata chance ya kufukia free fukia hadi cha kesho kutwa.

Mkuu miezi yako 6 tu inakutosha kupata 600k na kuanza biashara yako,ukjikaza to 1year utakua na 1.2m Mkuu maisha n safari ndefu na ili ulijue hilo ingiza utendaji ktk hii post,maisha yako unayoyaptia leo Kesho yatakua simulizi za kuchekesha,kuliza na hata kufundisha.

Pambana Mkuu,wenzako tulianza na mishahara ya 2000 per day mapito tuliyoptia ukiyaskia utajiona wewe kumbe n lakinare unamiliki milaki kwa mwezi tena uhakika...

wakat hyo 2000 nlokua nkipewa kuna siku boss anavurugwa anakuja anagomba anasema mna kazi ya kula tu hapa kazini kwangu kazi hamfanyi mnanipa hasara tu,anachukua mauzo yote anatuacha weupe... Mkuuu maisha n safari hebu ianze yako kuna utamu wake kuanza maisha kwa style yako TRUST me utanielewa siku 1 ukivuka hiki kipindi kigumu.

YES YOU CAN.
 
Kabla ya yote unatakiwa uwe na malengo yako, unataka kusave kwa muda gani? je ni miezi 6 au mwaka au miaka?

Fahamu sababu zinazokufanya u save pesa,je unataka ufungue biashara,au unataka ununue chombo cha usafiri?

Ukishafahamu target yako (labda target n 1 year) hapo sasa piga kazi ndani ya mwezi ukipokea pesa,kaa ndani tuliza akili..

Mkononi una 150k.. Jiulize matumizi yako makubwa n nini? najua kubwa n Malazi(kodi) na msosi.. Afya n muhimu ila kwenye mwanzo mgumu wa namna hii afya Muachie Allah....

Ukishajua matumizi yako makubwa n kodi na chakula,jiulize Unaweza kuondoa kipi kati ya hivyo viwili ili kibaki kimoja?

Jibu chakuondoa n Kodi,sasa utaishi wapi? Hapa sasa ndio ule msemo wa Maana halisi ya maisha unatokea eneo hili, Hapo Rudisha room ya watu..

Kama ulikua na vitu Uza vyotee bakiza nguo zako na begi tu kama mwana apolo,vitu utanunua huko mbeleni saivi havina maana yeyote maana hata kama una hotpot huna uwezo wakupka hata wali nusu uweke so hapa Ondoa mzigo uliokuganda.

Ukishauza kila kitu ukabaki mweupe n wewe begi lako na nguo zako ndani,sasa Rudsha chumba cha watu, Chukua siku 1 anza kuzunguka huko kwa vijana wanaopga kazi either wabeba tofali au au zege au mizigo ilmrad wawe vijana wapga kazi kweli unawaona.

mfate mmoja wao au waite wote waambie ndugu zangu mimi n mwanaume mwenzenu,nmekuja Mjini sina pa kuishi ila nmekuja kufanya kazi na nimepata kazi sehemu naomba mnifadhili pakulala tu walau mwezi huu tu,nkipata kodi nitahamia kwangu nikapange..

Amini nakwambia ktk lile kundi hatokosekana mmoja mwenye imani maana umeshawambia ukweli kuwa umekuja kutafuta maisha na unaomba pakulala tu.

Utakubaliwa nina uhakika uspokubaliwa zunguka sehemu nyngine na nyngine hadi utakapokutana na yule mtu ataekuelewa,Yupo Mkuu Yupo nina uhakika 100% ujue tu namna yakujieleza na uwe mstarabu.

Ukipata pakulala sasa kipengele ktabaki kwenye msosi, eneo hili nalo si la kucheza nalo linapoteza hela haswa,sasa hakikisha marafiki zako n kina mama ntlie na usijifanye much know kuwa mkweli ukienda kwa kna mama ntlie nunua ukoko ule mzuri utauziwa,siku moja moja ule vizuri ili usipoteze afya ule vtu vya kukupa afya TU.

ishi kwa malengo naamini kwa mwezi mzima utaweza save walau 100k kama kweli utakua na akili zile za mtafutaji wa maisha,aibu acha,ukipewa chakula maswala ya kuzuga umeshiba eti unasema Asante Acha ukipata chance ya kufukia free fukia hadi cha kesho kutwa.

Mkuu miezi yako 6 tu inakutosha kupata 600k na kuanza biashara yako,ukjikaza to 1year utakua na 1.2m Mkuu maisha n safari ndefu na ili ulijue hilo ingiza utendaji ktk hii post,maisha yako unayoyaptia leo Kesho yatakua simulizi za kuchekesha,kuliza na hata kufundisha.

Pambana Mkuu,wenzako tulianza na mishahara ya 2000 per day mapito tuliyoptia ukiyaskia utajiona wewe kumbe n lakinare unamiliki milaki kwa mwezi tena uhakika...

wakat hyo 2000 nlokua nkipewa kuna siku boss anavurugwa anakuja anagomba anasema mna kazi ya kula tu hapa kazini kwangu kazi hamfanyi mnanipa hasara tu,anachukua mauzo yote anatuacha weupe... Mkuuu maisha n safari hebu ianze yako kuna utamu wake kuanza maisha kwa style yako TRUST me utanielewa siku 1 ukivuka hiki kipindi kigumu.

YES YOU CAN.
Ningekua mahakamani na mm ndio judge ningegonga nyundo mara tatu, kuashiria CASE CLOSED...
CONTROLA umemaliza thread mzee, huu ushaur ni wa [emoji91][emoji95]
 
Back
Top Bottom