Kipi ni bora, Watu au wanyama pori?

Kipi ni bora, Watu au wanyama pori?

koryo1952

JF-Expert Member
Joined
Mar 7, 2023
Posts
948
Reaction score
1,627
Mhe. Waziri Mkuu aliwatuma Mawaziri wa kisekta kubaini mpaka halali wa Hifadhi ya Serengeti na Wilaya ya Tarime maeneo ya Gorong'a na Gibaso baada ya kilio cha muda mrefu kutoka kwa wananchi kuhusu mpaka huu.

Matokeo ya Tume hiyo ni kuwa malalamiko ya wananchi wa eneo husika hayana mashiko. Sasa ninakuja na swali: GN ya alama za mpaka huu uliwekwa katika miaka 1958 wakati Watanzania kwa wakati huo Idadi ya Watanzania wote ni kama 8 millioni. Mpaka sasa imepita takriban miaka 65 tangu alama hizo kuwekwa na kwa sasa idadi ya Watanzania inakadiriwa kufikia 61 millioni.

Inawezekana kwa wakati huo idadi ya wananchi kwa maeneo yanayogombaniwa walikuwa watu 200 na sasa inawezekana wako 30000. Kama Serikali ni serikali inayojali wananchi na ni Serikali sikivu je wanyama ni bora kuliko wananchi?

Kama wananchi wameongezeka kwa nini Serikali isisogeze alama za GN kilomita 50 ndani ili wananchi wapate nafasi ya makazi?

Ninaishauri Serikali kwa kuwa watu wameongezeka sana na thamani ya binadamu haiwezi kulinganishwa na mnyama basi ni vema Serikali ifikirie kusogeza GN ndani ya kilomita 50 ili mgogoro huu uweze kuisha jumla.
 
Kwa hiyo baada ya miaka 20, watu wataongezeka mfano elfu 70, mtasogeza tena?

Baada ya miaka 30 ijayo hapo watu watakuwa Milioni 1 mtaombewa mpewe kilomita 200 ndani zaidi?

Kuhusu Maisha binadamu na Wanyama wote Wana umuhimu sawa ila binadamu ni Invasive species ambaye anazidi kupunguza maeneo ya kuishi viumbe wengine.

Kama tunavyodhibiti magugu kule Victoria na Mimea mingine mbugani ndio inabidi Homo sapiens nao wawekewe mipaka ili tuweze kuexist in harmony na Ecology iplay part yake.
 
Kati ya wanyama pori na binadamu nani kamkuta mwenzake?! Halafu wanyama pori hawaharibu mazingira wanayatunza.
 
Mwanadam anajifanya yeye ndiyo Ana haki miliki ya kuishi duniani
Wanyama nao wana haki pia

Ova
 
Mhe. Waziri Mkuu aliwatuma Mawaziri wa kisekta kubaini mpaka halali wa Hifadhi ya Serengeti na Wilaya ya Tarime maeneo ya Gorong'a na Gibaso baada ya kilio cha muda mrefu kutoka kwa wananchi kuhusu mpaka huu.

Matokeo ya Tume hiyo ni kuwa malalamiko ya wananchi wa eneo husika hayana mashiko. Sasa ninakuja na swali: GN ya alama za mpaka huu uliwekwa katika miaka 1958 wakati Watanzania kwa wakati huo Idadi ya Watanzania wote ni kama 8 millioni. Mpaka sasa imepita takriban miaka 65 tangu alama hizo kuwekwa na kwa sasa idadi ya Watanzania inakadiriwa kufikia 61 millioni.

Inawezekana kwa wakati huo idadi ya wananchi kwa maeneo yanayogombaniwa walikuwa watu 200 na sasa inawezekana wako 30000. Kama Serikali ni serikali inayojali wananchi na ni Serikali sikivu je wanyama ni bora kuliko wananchi?

Kama wananchi wameongezeka kwa nini Serikali isisogeze alama za GN kilomita 50 ndani ili wananchi wapate nafasi ya makazi?

Ninaishauri Serikali kwa kuwa watu wameongezeka sana na thamani ya binadamu haiwezi kulinganishwa na mnyama basi ni vema Serikali ifikirie kusogeza GN ndani ya kilomita 50 ili mgogoro huu uweze kuisha jumla.
ukifuatwa ushauri wako pia baada ya miaka 65 ijayo hifadhi ya serengeti itakuwa imetoweka.tanzania ni nchi kubwa na kuna mapori mengi ambako watu wanaruhusiwa kuishi.si lazima watu wajazane pale hifadhini bali watafute maeneo mengine ya kuishi ili kuzilinda hifadhi zetu kwa manufaa mapana ya vizazi vyetu.
 
Serengeti haipasi kufa lazima ilindwe.

Tanzania bado kubwa sio lazima hao raia waishi hapo, wanaweza kuhamia maeneo mengine wakaiacha hiyo paradiso ya wanyama hapo.
 
Back
Top Bottom