bryan2
JF-Expert Member
- Jun 8, 2016
- 3,323
- 4,679
Pale Stand United kuna Mrundi,Mbeya city kuna Mrundi pia,Simba nao kwa sasa kuna Mrundi,Yanga kuna Mzambia Lwandamina sijawataja Mromania wa Azam wala Hans Vans Plujim nimewataja makocha wa Nchi za Kiafrika tu waliomo nchini kwani nchi nyingi za Kiafrika tunafanana karibia kila kitu.
Makocha hawa sijui wamewazidi nini makocha wazalendo wa ndani ukiangalia kwa jicho la ndani zaidi ni makocha wachache sana kutoka kwetu wanaenda kufundisha timu za nje hasa za Kiafrika na tena wanakua makocha wasaidizi kuna Kocha Kama Kitambi alikua Kenya,Mkwasa naye alitoka kidogo ila sijasikia mwingine tena hata wakienda tu nchi za kawaida kama vile Rwanda,Burundi,South Sudan ambao atleast tupo nao level moja kisoka.
Najiuliza ni uwoga wa kujaribu kutoka na kutafuta Fursa sehemu nyingine au leseni zao haziruhusu nikimaanisha hawajafikia viwango vinavyotakiwa kufundisha mpira?
Makocha hawa sijui wamewazidi nini makocha wazalendo wa ndani ukiangalia kwa jicho la ndani zaidi ni makocha wachache sana kutoka kwetu wanaenda kufundisha timu za nje hasa za Kiafrika na tena wanakua makocha wasaidizi kuna Kocha Kama Kitambi alikua Kenya,Mkwasa naye alitoka kidogo ila sijasikia mwingine tena hata wakienda tu nchi za kawaida kama vile Rwanda,Burundi,South Sudan ambao atleast tupo nao level moja kisoka.
Najiuliza ni uwoga wa kujaribu kutoka na kutafuta Fursa sehemu nyingine au leseni zao haziruhusu nikimaanisha hawajafikia viwango vinavyotakiwa kufundisha mpira?