Kipigo cha Al Ahly kwa Simba ni fedheha kwa wachambuzi maandazi waliojazana hapa nchini

Mkuu mpira hauko hivo...El Mereikh
sio ya kuibeza!
watakuja kivingine kabisa!
Hicho unakiita kisaikolojia watakuwa wanataka ushindi kwa nguvu sana! Baadaya kupoteza mbili....kumbuka hata wao ...kimehasabu bado wanaweza kufuzu!
El Mereikh Soo wa kuwabeza eti ni mataokeo ya soka wakati mwingine huwa hayaeleweki!
Simba aingie kucheza na ElMereikh kwa heshima na tahadhati kubwa Sana ,otherwise tunaweza kusshangaa!
 
Juzi Kiemba akihojiwa alisema Simba anashinda ,wachambuzi wao wanasema Al Ahly anashinda ,kweli wachezaji ndo watoe maoni siyo watu ambao hata hawajapitia ndondo cup
 
Yan wachambuzi wetu hawana aibu kbs, jana nawasikiliza wamegeuka kuisifia simba kinafki..
 
Badilisha kichwa (heading au title): ni kipigo cha Simba kwa Al Ahly. Si kipigo cha Al Ahly kwa Simba. Simba ndio iliyotoa kipigo!
 
Kwa kipindi hiki cha miezi mitatu niliyopo Tz,nimekuwa nikifuatilia sana vipindi vya michezo vya vituo vya radio na runinga,lakini niseme ukweli Tanzania hakuna wachambuzi wa soka kabisa,ni wachafuzi na wapiga ramli tu.
 
Ukweli upo pale pale, kuvuka group stage ni hesabu za mezani kwanza ukibugi umepotea. Tunatakiwa kupigana kufa na kupona tupate point 4 kutoka kwa merreikh Ili tuingie robo fainali kwasababu kuna uwezekano mkubwa ahli na vita wakabeba points zote 6 kutoka kwa merreikh na hizi mechi nyingine wakaokoteza. Vita ni timu kubwa na ina uwezo wa kutupiga home, hatutegemei kushinda au draw kwa ahli akiwa nyumbani.

Man utd imeondolewa uefa kwasababu walipoteza mechi nyepesi ambayo hata draw tu ingefaa lakini wakapoteza kule uturuki na wenzake leipzig na psg walibeba points zote 6 zilizowavusha kutoka kwa mturuki, man akabaki na 9 na hazikutosha kumvusha.
 
Juzi Kiemba akihojiwa alisema Simba anashinda ,wachambuzi wao wanasema Al Ahly anashinda ,kweli wachezaji ndo watoe maoni siyo watu ambao hata hawajapitia ndondo cup
Wale wanaotangaza mpira nje na niliowataja juu na unaowaona espn, sky sports, bt sports, bein sports pamoja na kuwa ni wachezaji pia wamemaliza na kupata leseni za ukocha fifa kwa ngazi za juu. Ukienda kuomba kazi ya uchambuzi/kutangaza mpira unatuma na vyeti vya ukocha. Angalia tofauti ya kipindi cha kipyenga cha mwisho cha ot kazi na hao kina dauda, kitenge
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…