Kipigo cha magoli 9 chamfuta kazi Kocha wa Bournemouth

Kipigo cha magoli 9 chamfuta kazi Kocha wa Bournemouth

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Klabu hiyo imemfuta kazi Scott Parker aliyekuwa meneja wake ikiwa ni siku chache baada ya kufungwa magoli 9 - 0 dhidi ya Liverpool. Parker anakuwa kocha wa kwanza ndani ya Ligi ya England kufungashiwa virago tangu msimu ulipoanza.

Taarifa iliyothibitishwa na Mmiliki wa klabu hiyo, Maxim Demin imesema "Ningependa kuweka kwenye rekodi shukrani zangu kwa Scott na timu yake kwa juhudi zao wakati wa kukaa nasi. Kupanda kwetu kurejea Ligi Kuu msimu uliopita chini ya uongozi wake kutakumbukwa daima kuwa moja ya misimu yenye mafanikio zaidi katika historia yetu.

“Hata hivyo, ili tuendelee kusonga mbele kama timu na Klabu kwa ujumla, ni lazima tuwe sawa katika mkakati wetu wa kuendesha klabu kwa uendelevu. Ni lazima pia tuoneshe imani na heshima kwa wenzetu. Hiyo ndiyo njia ambayo imeiletea klabu hii mafanikio makubwa katika historia ya hivi karibuni, na ambayo hatutakengeuka kutoka sasa. Msako wetu wa kumtafuta kocha mkuu utaanza mara moja.”
 
9 nyingi sana.Anaondoka akiwa kajiwekea rekodi chafu sana,mwishoni.
 
Yule wa simba anasuburia mpaka aje atolewe Caf champions league ndio wamtimue wakati inajulikana hamna kocha pale.
 
Yule wa simba anasuburia mpaka aje atolewe Caf champions league ndio wamtimue wakati inajulikana hamna kocha pale.
lakini bila kumsahau yule wa Yanga tangu ajiunge na Yanga hajawahi kushinda hata mechi moja ya kimataifa
 
Naona kama wamemuonea game ya kwanza alicheza na aston villa alishinda.
game zote zilizofata kacheza na arsenal,man city,Liverpool

Sasa hapo kwa kiwango cha hizo timu alizokutana nazo kama kaonewa.
 
Liva wanafkuzisha sana makocha,
Halafu hizi tisa zilikuwa za manu hizi sema tu bahati mbaya waliwahi liva hawajachanganya,
Sema nini marudiano wanakula tisa bila
 
Back
Top Bottom