King Kong III
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 56,205
- 79,515
Hizo ndio akili za mafukara, subiria sasa hiko kipato kikue ufe
Kabla ya kununua Gari kaa chini na piga hesabu unataka kufikia wapi kwenye maisha yako? una malengo gani? na je gari itakusaidia kufikia malengo yako? kama unanunua gari kwa ajili kukwepa kupanda daladala, kujionyesha na wewe unazo, hapo umekosea na hio gari itakufanya maskini, number hazidanganyi kaa chini, piga hesabu ya kipato, gawanya kwa matumizi yako, ya maendeleo,ya kununua gari, na kulihudumia gari, ukipata jibu ndio ufanya uamuzi
Gari itakupa heshima binafsi mjini (japokuwa inaweza kukupa umaskini pia ukijichanganya). Nyumba ni urithi wa kudumu kimaisha katika familia. Kuna namna fulani mtu anakuwa na utulivu wa ndani akiwa anaishi kwake. Na kuna namna fulani hivi ya kujisikia ufahari na kujiamini ukiwa unamiliki gari.
Tusiokuwa na gari hii thread haituhusu kabisa
Pambana, mange kimambi na lemutuz hawana nyumba ila wana magari tu, na wanaongoza kwa kuwa na furaha nadhani kuliko hata kiumbe chochote hapa duniani.
Mkuu gari inaogopwa kuliko nyumba, hamna uchawi pale, ni mambo ya hela tu, nyumba hata ya matope unajenga kwa laki tano tu fukayosi huko
Mkuu, pambana upate gari au nenda kajenge fukayosi huko maana najua na naamini huwezi kununua kiwanja posta au upanga kule we subiri viwanja vya kata
Baelezee hayo mafukaraUkiona mtu kanunua gari basi uwezo wa kujenga nyumba ni kama kumsukuma mlevi.
Gari unatoa hela zote moja kwa moja kama 15m unatoa hapo hapo ,hakuna oprtion ya kuanza kunua chassis au matairi au milango kisha ndio uunganishe , ila nyumba unaanza kununua kiwanja kwanza kisha unatulia ,unachimba msingi na kujenga foundation unatulia,unapandisha boma unatulia ,unaezeka na kuweka grill unatulia.
Hawakufanyi chochote we vuta mkwaju tu hata kama ni tu porte namba A urudishe heshima mtaaniHuku kwetu ukinunua Gari unarogwa, siyo kwamba watu hawapendi kumiliki vitu vya aina hiyo ila tunahofia kuuwawa na watu wabaya wenye husda
Bora uwe normal tuu na siyo kufuata mkumbo
Kawaida tu kumbuka siku nyingine inakuwaga full tank hiyo mzee, hiyo ilikuwa hali ya kupita tuKuna pisi kali juzi imeshindwa kwenda kazini na BMW yake, ikaniambia ukweli nimeamua kutulia home sina hata buku kumi ya mafuta,mnyamwezi nikaiambia ungesema mapema mamayo zako.
Gari ni asset sasa kwanini isiwe sehemu ya mavuno ya mafanikio na kupiga hatuaAsikudanganye mtu wala kukutia moyo, kama wewe huna gari hata kama ni mkweche unahesabika ni fukara tu hata kama una nyumba 50, tafuta gari upate amani ya moyo na heshima kwa wakwe hata kama huna hela.
Muhimu kujilinda, korona ipo na inaua fuateni miongozo ya wataalam wa afya jamani.
Kzba.
Ujinga mbona mbali hivyo😀,unazani ata ela ya Vitz ninayo sasa🤣🤣Endelea na ujinga wako