Elections 2010 Kipindi cha Dk Slaa kilichokuwa kirudiwe chaahirishwa

Elections 2010 Kipindi cha Dk Slaa kilichokuwa kirudiwe chaahirishwa

Hivi mnajua kuwa ITV wamepata msuko msuko sana toka jumamosi? Chadema kimezuia marudio hayo kufanyika leo, na badala yake itakuwa trh 30 jumamosi ....
 
hao 28 gusts hapo chini ndo kina thithiem wanacount reaction, masikini watz wengi hawana acss to media km internet etc
 
Kwani wao hawajipendi hadi waseme ni nani aliyekataza mahojiano na Rais Mtarajiwa kutorudiwa? Inajulikana wazi ni nani, hao ITV wameshatishiwa labda wanaweza kunyang'anywa leseni yao kama wakiyarudia.Tuwape kazi nzito ya kuiba kura kwa kuwapigia wabunge wa chadema na Rais Mtarajiwa kwa kishindo

Dah hawa watu wasanii sana.They think we don't see what's going on.Njia peke ni kushusha hasira zetu kwenye ballot box.They just can't play with our emotions like this Damn!..Limewafika shingoni,wanachokosea kufaham ni kuwa huu moto umewashwa na Dr. Slaa hakuna wa kuuzima,it's here to stay!..There are a lot of Dr. Slaas out there coming gun em down!..Mafisadi kaa chonjo,enuf z enuf!
 
Hivi mnajua kuwa ITV wamepata msuko msuko sana toka jumamosi? Chadema kimezuia marudio hayo kufanyika leo, na badala yake itakuwa trh 30 jumamosi ....
i doght km itarudiwa hii siku mmh, well tusubiri yetumacho
 
Hivi mnajua kuwa ITV wamepata msuko msuko sana toka jumamosi? Chadema kimezuia marudio hayo kufanyika leo, na badala yake itakuwa trh 30 jumamosi ....

Chadema walipie kipindi ili kifanyike mara mbili, kesho au keshokuwa na tarehe 30. Chadema wasitegee tarehe 30 pekee kwa sababu CCM wanazima umeme. Ili kuongeza idadi ya waangaliaji kipindi kirudiwe mara mbili kesho na tarehe 30.
 
Hivi mnajua kuwa ITV wamepata msuko msuko sana toka jumamosi? Chadema kimezuia marudio hayo kufanyika leo, na badala yake itakuwa trh 30 jumamosi ....

Mkuu naomba ututhibitishie hili laa sivyo huu utakuwa udaku mkuu, mwaga source yako isije ikawa issue za magazei ya rangirangi.
 
jana usiku pale sitting room kwangu nilitukana matusi mpaka mdomo ukakauka

waliniudhi sana hawa ITV.
 
Pole sana emmathy, nami yamenikuta! Nilisubiri mpaka saa 7 uciku lakini hakikuoneshwa. Leo asb nimempigia mshirika mmoja ITV, anadai dakika tano kabla ya kuanza kuoneshwa, walipokea order ya kutorudia kipindi hicho!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

What? Si mnaona? Tumetawaliwa na watu wasio itakia mema nchi kwa muda mrefu, huu ni uhalifu usiokuwa na mfano.

Laki wazanzania HATUDANGANYIKI Tena! This time we need a big change for NATIONAL DEVELOPMENT

wakuu kumbe huu ni uchaguzi wa Raia wema dhidi ya UFISADI!
 
Hakuna asiyejua kuwa ITV wamewekewa mkwila yakuwa wasikirushe kipindi, lkn hatujali sana, kwani dr slaa ndiye rais wetu tunayemjua ss jk akishinda atatueleza vizuri kura za ushindi kazipata wapi.
 
Taarifa zilizotoka katika chumba cha utangazaji cha ITV zinasema Mda mchache uliopita wamepigiwa simu Joyce Mwavile kuwa wasitishe kukirusha kipindi hicho.

Baada ya kudadisi asubuhi nimeambiwa asubuhi Riziwani alitinga katika ofisi za ITV na kukutana na watu kadhaa. Alipotafutwa Steven Chuwa ambaye alikuwa amelala nakumuuliza habari hizo akajibu kuwa watu hawa wamefanya usanii flani japo hakutaka kuwa wazi.

Baada ya kupiga chumba cha utangazaji wao walikuwa wamepitisha taarifa ya kuomba radhi, Tanzania hii lazima tuikomboe.

Taarifa nyingine muhimu ni kuwa Kikwete anatarajiwa kuwa Live kesho asubuhi Star TV katika jiji la Mwanza kuanzia saa 1:30 kwa kipindi kama alichofanya Dk Slaa. Hizi habari zimekuwa za kificho na tayari amewaamuru watangazaji wa Star TV kutoruhusu maswali magumu, Mtu huyu amekuwa anapanga mpango huu kwa kutokuwa wazi mpaka sasa haijulikani kama itakuwa hivyo.

Ndugu wana JF tujiandae......
Hivi Ridhwani ni nani kwenye nchi hii?
kwa nini Mwema asimkamate kwa kuingilia shughuli za serikali ilhali yeye si mwajiriwa wa serikali?
msisubiri wananchi wakachukua hatua jamani.
 
ITV, tujulisheni marudio yatakuwa lini? ile Jmosi tuliwapa big-up sana, msituangushe sasa. Hivyo ndio vipindi vyenye soko, mtuambie na kuadvertise kabisa, lini mtafanya marudio.

Marudio yatakuwa Jumapili tarehe 31.10.2010 saa 1 kamili usiku. Wana CHADEMA woooote mnaombwa msikose kutazama.:smile-big:
 
Marudio yatakuwa Jumapili tarehe 31.10.2010 saa 1 kamili usiku. Wana CHADEMA woooote mnaombwa msikose kutazama.:smile-big:

Fullish!!!!!!!!!!!! What? Why 31/10? Hata hivyo UFISADI utaambulia patupu.
 
Kwa kweli hata mimi nimesikitika sana kwa kuwa nilikuwa nimechoka sana nililala mapema na kuweka alarm na alarm ilifanikiwa kuniamsha ajabu nikakutana na Mieleka imenisikitisha sana na mimi sikubahatika kuangalia live na nikatumaini nitampata recorded ITV tunaomba mtuambie mtarudia lini ili tupate nondo za DR.Hata hivyo kwenye tube naangalia na kusikiliza sio mbaya sana.Saa ya ukombozi imefika Watanzania tufanye mabadiliko sasa.
 
Kinana, January Makamba na Ridhiwani hawalali usingizi ili kuhakikisha kwamba mengi zaidi hayaendelei kuanikwa kuhusu mgombea wa CCM. Wameonekana sana wakipitapita kwenye media mbalimbali. Lakini wajue kwamba wameshachelewa; watanzania wameamka toka usingizini na sasa kwa hakika wanataka mabadiliko. Bahati nzuri Mungu amesikia kilio chao na amewaletea Dr Slaa, ili kupitia kwake nchi ipige hatua ya maendeleo. Kumchagua Kikwete kwa kipindi cha miaka mingine mitano ni kuirudisha nchi nyuma kwa miaka mitano mingine.
 
Nawaambia hao itv ya kuwa kila jambo na mwisho wake,watafanya hivyo mpaka itafika siku watachoka na hawataweza kuingia ndani ya mioyo ya watanzania iliyobadilika!
 
Back
Top Bottom