Kipindi cha miezi 6 wawekezaji wamevunja rekodi ya kuja wengi nchini

Kipindi cha miezi 6 wawekezaji wamevunja rekodi ya kuja wengi nchini

Unaiamini hii Serikali iliyojaa waongo wanaodai nchini kuna Vibrant democracy na good record on human rights? Wawekezaji na Covid-19 hii?
🤣😳😳😳

KIPINDI CHA MIEZI 6 WAWEKEZAJI WAMEVUNJA REKODI YA KUJA WENGI NCHINI.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amesema katika kipindi cha miezi sita ikiwa ni kuanzia mwezi Machi hadi Agosti, 2021, idadi ya wawekezaji wanye nia ya kutaka kuweza nchini imeongezeka.

Mheshimiwa Rais Samia ameyasema hayo leo Septemba 26, 2021 wakati akisalimiana na wananchi wa Wilaya ya Dodoma Mjini waliofika kumpokea katika eneo la Chinangali, mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Dodoma akitokea jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Wananchi wa Wilaya ya Dodoma Mjini waliofika kumpokea katika eneo la Chinangali mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Dodoma akitokea jijini Dar es Salaam leo Septemba 26, 2021.

Amefafanua kuwa, kuna miradi ambayo hawakujua kuwa wawekezaji wanakuja,hivyo miradi hiyo itatekelezwa kama ilani ilivyoeleza na miradi mingine ilani inaeleza wawekezaji watafutwe.

“Ilani ilitutuma tutafute wawekezaji waje kuwekeza, nami nataka kuwaambia wawekezaji tumepata wengi mno. Lakini niwaambie kwamba katika kipindi cha miezi sita kumekuwa na idadi kubwa ya wawekezaji ambao wanataka kuwekeza Tanzania. Kati ya hao tuna kiwanda cha mbolea kinachoendelea kujengwa hapa Dodoma. Nawaahidi na wengine watakuja,” amesisitiza Rais Samia.

Hivi karibuni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji, Mhe. Geoffrey Mwambe, akiongea na vyombo vya habari juu ya juhudi zinazofanywa na ofisi hiyo, pamoja na taasisi zake katika kuweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji nchini, aliutaja mradi wa uwekezaji wa kimkakati wa Kampuni ya ITRACOM FERTILIZERS LIMITED unaotekelezwa katika mkoa wa Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akivalishwa vazi la kimila na wazee wa kimila wa Kabila la Kigogo wenye asili ya Dodoma wilayani Chamwino kama ishara ya ukaribisho mara baada ya kuwasili Chamwino Ikulu akitokea jijini Dar es Salaam leo Septemba 26,2021.

Mzee wa Kimila wa Kabila la Kigogo Wilayani Chamwino mkoani Dodoma, Bw. Goden Wenga akimkabidhi Ngao na Mkuki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, kama ishara ya ukaribisho mara baada ya kuwasili Chamwino Ikulu akitokea jijini Dar es Salaam leo Septemba 26,2021. (Picha zote na Ikulu).

Amefafanua kuwa, mradi huo, utazalisha mbolea asilia. Mradi huo una mtaji wa Dola za Marekani milioni 180 na unatarajiwa kuzalisha ajira 3000. Mradi huo utaingiza fedha za kigeni na utaongeza kipato kwa wananchi na mapato ya serikali kupitia kodi.

Mhe. Mwambe alibainisha kuwa katika kipindi cha mwezi Machi hadi Agosti, 2021 jumla ya miradi 133 imesajiliwa ikilinganishwa na miradi 105 iliyosajiliwa katika kipindi hicho mwaka 2020 ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 27.

Miradi iliyosajiliwa katika kipindi hicho inatarajiwa kuzalisha ajira 29,709 ikilinganishwa na ajira 8,252 zilizotarajiwa kuzalishwa katika kipindi hicho mwaka 2020. Miradi hiyo ipo katika Sekta ya Kilimo, ujenzi/majengo ya biashara, nishati, Miundombinu ya kiuchumi, Taasisi za fedha, rasilimali watu, viwanda, usafirishaji, utalii na huduma.

Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji pamoja na Taasisi zake inaendelea kuwahakikishia wawekezaji kuwa itaendelea kuratibu masuala ya uwekezaji ili kuhakikisha wanakuwa na mazingira wezeshi ya uwekezaji.
 
Pesa ipi? Ulikuwa uchumi feki!
Uchumi feki ndio tunataka sasa,uchumi original ndio ule mlikuwa mnapora wafanyabiashara? Mwambie dabu na genge lenu anyanyue Domo aone moto..

Kwani uchumi feki kama unanipa pesa wewe unateseka na nini? Uchumi feki ndio huo Sasa unamuwezesha mama kujenga vyumba 15,000 vya madarasa ,,vituo vya afya 250 na milioni 500 kila Jimbo huku akidabo bajeti ya Tarura na miradi mliyoshindwa kukamilisha miaka 6 itaisha ,kenge nyie mna nini cha kutuambia?
 
KIPINDI CHA MIEZI 6 WAWEKEZAJI WAMEVUNJA REKODI YA KUJA WENGI NCHINI.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amesema katika kipindi cha miezi sita ikiwa ni kuanzia mwezi Machi hadi Agosti, 2021, idadi ya wawekezaji wanye nia ya kutaka kuweza nchini imeongezeka.

Mheshimiwa Rais Samia ameyasema hayo leo Septemba 26, 2021 wakati akisalimiana na wananchi wa Wilaya ya Dodoma Mjini waliofika kumpokea katika eneo la Chinangali, mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Dodoma akitokea jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Wananchi wa Wilaya ya Dodoma Mjini waliofika kumpokea katika eneo la Chinangali mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Dodoma akitokea jijini Dar es Salaam leo Septemba 26, 2021.

Amefafanua kuwa, kuna miradi ambayo hawakujua kuwa wawekezaji wanakuja,hivyo miradi hiyo itatekelezwa kama ilani ilivyoeleza na miradi mingine ilani inaeleza wawekezaji watafutwe.

“Ilani ilitutuma tutafute wawekezaji waje kuwekeza, nami nataka kuwaambia wawekezaji tumepata wengi mno. Lakini niwaambie kwamba katika kipindi cha miezi sita kumekuwa na idadi kubwa ya wawekezaji ambao wanataka kuwekeza Tanzania. Kati ya hao tuna kiwanda cha mbolea kinachoendelea kujengwa hapa Dodoma. Nawaahidi na wengine watakuja,” amesisitiza Rais Samia.

Hivi karibuni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji, Mhe. Geoffrey Mwambe, akiongea na vyombo vya habari juu ya juhudi zinazofanywa na ofisi hiyo, pamoja na taasisi zake katika kuweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji nchini, aliutaja mradi wa uwekezaji wa kimkakati wa Kampuni ya ITRACOM FERTILIZERS LIMITED unaotekelezwa katika mkoa wa Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akivalishwa vazi la kimila na wazee wa kimila wa Kabila la Kigogo wenye asili ya Dodoma wilayani Chamwino kama ishara ya ukaribisho mara baada ya kuwasili Chamwino Ikulu akitokea jijini Dar es Salaam leo Septemba 26,2021.

Mzee wa Kimila wa Kabila la Kigogo Wilayani Chamwino mkoani Dodoma, Bw. Goden Wenga akimkabidhi Ngao na Mkuki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, kama ishara ya ukaribisho mara baada ya kuwasili Chamwino Ikulu akitokea jijini Dar es Salaam leo Septemba 26,2021. (Picha zote na Ikulu).

Amefafanua kuwa, mradi huo, utazalisha mbolea asilia. Mradi huo una mtaji wa Dola za Marekani milioni 180 na unatarajiwa kuzalisha ajira 3000. Mradi huo utaingiza fedha za kigeni na utaongeza kipato kwa wananchi na mapato ya serikali kupitia kodi.

Mhe. Mwambe alibainisha kuwa katika kipindi cha mwezi Machi hadi Agosti, 2021 jumla ya miradi 133 imesajiliwa ikilinganishwa na miradi 105 iliyosajiliwa katika kipindi hicho mwaka 2020 ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 27.

Miradi iliyosajiliwa katika kipindi hicho inatarajiwa kuzalisha ajira 29,709 ikilinganishwa na ajira 8,252 zilizotarajiwa kuzalishwa katika kipindi hicho mwaka 2020. Miradi hiyo ipo katika Sekta ya Kilimo, ujenzi/majengo ya biashara, nishati, Miundombinu ya kiuchumi, Taasisi za fedha, rasilimali watu, viwanda, usafirishaji, utalii na huduma.

Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji pamoja na Taasisi zake inaendelea kuwahakikishia wawekezaji kuwa itaendelea kuratibu masuala ya uwekezaji ili kuhakikisha wanakuwa na mazingira wezeshi ya uwekezaji.
Ni jambo jema sana kupata wawekezaji wenye nia ya kuja kuweka mitaji yao ili kuwekeza na kupata faida na sisi kama nchi tupanue tax base.


Ila ijulikane, kupata certificate ya uwekezaji na kuleta fedha za kuja kuwekeza ni mambo mawili tofauti. JPM amewahi kutembelewa na Germany investor back in 2016/17 na baadae mambo yakanoga mpaka akahakikishia na Chancellor Angeka Merkel kuhusu uwekezaji huo, ila mpaka ameaga dunia hamna hata jiwe la msingi la hao wawekezaji.


Naipogenza TIC, naipongeza awamu ya 6 ila yasije yakawa yale ya kuwa biashara nyingi zimesajiliwa BRELA na watu kuandikisha nia ya kuwekeza TIC yet baada ya muda tunafanya tathmini na kugundua tumepiga hatua kiasi kidogo sana au kuna majamaa yanaweka mambo sawa, wanavuta fedha zinaingia kwenye local banking systems baadae zinakwenda kwingineko; sometimes hayatokeaga haya na huwa ni sehemu ya biashara bila kuvunja sheria.
 
Kwa kweli hata hamueleweki mnatakaje hasa.
Wawekezaji wasipokuja mnalaumu sera, wakija wawekezaji mnadai wanyonyaji.
Mwatakaje haswa!!!
Hata mie sifahamu wabongo wanataka nini. Wawekezaji usipowekea mazingira mazuri wanakimbilia kwengine. Kumbukeni muekezaji ana fedha mkononi au mtaji, ana channels nyingi za kwenda.

Suala la mikataba nadhani hii mikataba ni public records, mtu kama anao ushahidi wa mkataba mbovu basi aeke tuu kwenye mitandao au awape wabunge watuekee wapi tuone. Lakini wawezekaji ni muhimu katika kukuza uchumi.
 
Ni jambo jema sana kupata wawekezaji wenye nia ya kuja kuweka mitaji yao ili kuwekeza na kupata faida na sisi kama nchi tupanue tax base.


Ila ijulikane, kupata certificate ya uwekezaji na kuleta fedha za kuja kuwekeza ni mambo mawili tofauti. JPM amewahi kutembelewa na Germany investor back in 2016/17 na baadae mambo yakanoga mpaka akahakikishia na Chancellor Angeka Merkel kuhusu uwekezaji huo, ila mpaka ameaga dunia hamna hata jiwe la msingi la hao wawekezaji.


Naipogenza TIC, naipongeza awamu ya 6 ila yasije yakawa yale ya kuwa biashara nyingi zimesajiliwa BRELA na watu kuandikisha nia ya kuwekeza TIC yet baada ya muda tunafanya tathmini na kugundua tumepiga hatua kiasi kidogo sana au kuna majamaa yanaweka mambo sawa, wanavuta fedha zinaingia kwenye local banking systems baadae zinakwenda kwingineko; sometimes hayatokeaga haya na huwa ni sehemu ya biashara bila kuvunja sheria.
Biashara nyingi zikisajiliwa na watu kufanyaa biashara wewe unateseka nini? Sekta binafsi itakuwa imetatua tatizo la ajira Sio kila ajira lazima TRA wachukue pesa..

Turudi Uchumi wa JK ndio uchumi wa kumpa purchasing power mtu na kumtoa kwenye kuishi kama mashetani ..

Kwani hukumbuki kipindi Cha JK watu walikuwa wanaacha Kazi ya serikali na kujiajiri? Spirit ya kujiajiri ilianza kujengeka,sasa tuulizane nani alipenda kujiajiri awamu ya Dhalimu Mwendazake?
 
Hata mie sifahamu wabongo wanataka nini. Wawekezaji usipowekea mazingira mazuri wanakimbilia kwengine. Kumbukeni muekezaji ana fedha mkononi au mtaji, ana channels nyingi za kwenda.

Suala la mikataba nadhani hii mikataba ni public records, mtu kama anao ushahidi wa mkataba mbovu basi aeke tuu kwenye mitandao au awape wabunge watuekee wapi tuone. Lakini wawezekaji ni muhimu katika kukuza uchumi.
Achana na kuwajibu wapumbavu na misukule ya mwendazake,usituhusishe wote unaposema wabongo.
 
Biashara nyingi zikisajiliwa na watu kufanyaa biashara wewe unateseka nini? Sekta binafsi itakuwa imetatua tatizo la ajira Sio kila ajira lazima TRA wachukue pesa..

Turudi Uchumi wa JK ndio uchumi wa kumpa purchasing power mtu na kumtoa kwenye kuishi kama mashetani ..

Kwani hukumbuki kipindi Cha JK watu walikuwa wanaacha Kazi ya serikali na kujiajiri? Spirit ya kujiajiri ilianza kujengeka,sasa tuulizane nani alipenda kujiajiri awamu ya Dhalimu Mwendazake?
Mkuu sina hisia yoyote ya kuteseka na mafanikio yanayochochea mtiririko wa fedha mtaani kupitia shughuli za kibiashara halali.

Kutoa tahadhari sio kukosoa/kuwa na nongwa; ila kama tutafikia kwenye mambo ya kughushifi kama boss mmoja wa TRA zamani na kupiga cha juu kama ndio Tanzania tunayoitaka, hakuna atakaezuia.
Cha msingi tu kusiwa na kampuni kama Kagoda and the like, zinasajiliwa hapa, wanakwapua BoT then vijinsenti vinabaki hapa, lion share inaondoka
 
Uchumi feki ndio tunataka sasa,uchumi original ndio ule mlikuwa mnapora wafanyabiashara? Mwambie dabu na genge lenu anyanyue Domo aone moto..

Kwani uchumi feki kama unanipa pesa wewe unateseka na nini? Uchumi feki ndio huo Sasa unamuwezesha mama kujenga vyumba 15,000 vya madarasa ,,vituo vya afya 250 na milioni 500 kila Jimbo huku akidabo bajeti ya Tarura na miradi mliyoshindwa kukamilisha miaka 6 itaisha ,kenge nyie mna nini cha kutuambia?
Hii ya madarasa ni unyang'anyi kupitia kitu kinaitwa tozo,halafu nia na matokeo ni vitu viwili tofauti,sema mna nia ya kujenga vyumba 15k vya madarasa
 
KIPINDI CHA MIEZI 6 WAWEKEZAJI WAMEVUNJA REKODI YA KUJA WENGI NCHINI.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amesema katika kipindi cha miezi sita ikiwa ni kuanzia mwezi Machi hadi Agosti, 2021, idadi ya wawekezaji wanye nia ya kutaka kuweza nchini imeongezeka.

Mheshimiwa Rais Samia ameyasema hayo leo Septemba 26, 2021 wakati akisalimiana na wananchi wa Wilaya ya Dodoma Mjini waliofika kumpokea katika eneo la Chinangali, mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Dodoma akitokea jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akisalimiana na Wananchi wa Wilaya ya Dodoma Mjini waliofika kumpokea katika eneo la Chinangali mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa ndege wa Dodoma akitokea jijini Dar es Salaam leo Septemba 26, 2021.

Amefafanua kuwa, kuna miradi ambayo hawakujua kuwa wawekezaji wanakuja,hivyo miradi hiyo itatekelezwa kama ilani ilivyoeleza na miradi mingine ilani inaeleza wawekezaji watafutwe.

“Ilani ilitutuma tutafute wawekezaji waje kuwekeza, nami nataka kuwaambia wawekezaji tumepata wengi mno. Lakini niwaambie kwamba katika kipindi cha miezi sita kumekuwa na idadi kubwa ya wawekezaji ambao wanataka kuwekeza Tanzania. Kati ya hao tuna kiwanda cha mbolea kinachoendelea kujengwa hapa Dodoma. Nawaahidi na wengine watakuja,” amesisitiza Rais Samia.

Hivi karibuni Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Uwekezaji, Mhe. Geoffrey Mwambe, akiongea na vyombo vya habari juu ya juhudi zinazofanywa na ofisi hiyo, pamoja na taasisi zake katika kuweka mazingira wezeshi kwa wawekezaji nchini, aliutaja mradi wa uwekezaji wa kimkakati wa Kampuni ya ITRACOM FERTILIZERS LIMITED unaotekelezwa katika mkoa wa Dodoma.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akivalishwa vazi la kimila na wazee wa kimila wa Kabila la Kigogo wenye asili ya Dodoma wilayani Chamwino kama ishara ya ukaribisho mara baada ya kuwasili Chamwino Ikulu akitokea jijini Dar es Salaam leo Septemba 26,2021.

Mzee wa Kimila wa Kabila la Kigogo Wilayani Chamwino mkoani Dodoma, Bw. Goden Wenga akimkabidhi Ngao na Mkuki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan, kama ishara ya ukaribisho mara baada ya kuwasili Chamwino Ikulu akitokea jijini Dar es Salaam leo Septemba 26,2021. (Picha zote na Ikulu).

Amefafanua kuwa, mradi huo, utazalisha mbolea asilia. Mradi huo una mtaji wa Dola za Marekani milioni 180 na unatarajiwa kuzalisha ajira 3000. Mradi huo utaingiza fedha za kigeni na utaongeza kipato kwa wananchi na mapato ya serikali kupitia kodi.

Mhe. Mwambe alibainisha kuwa katika kipindi cha mwezi Machi hadi Agosti, 2021 jumla ya miradi 133 imesajiliwa ikilinganishwa na miradi 105 iliyosajiliwa katika kipindi hicho mwaka 2020 ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 27.

Miradi iliyosajiliwa katika kipindi hicho inatarajiwa kuzalisha ajira 29,709 ikilinganishwa na ajira 8,252 zilizotarajiwa kuzalishwa katika kipindi hicho mwaka 2020. Miradi hiyo ipo katika Sekta ya Kilimo, ujenzi/majengo ya biashara, nishati, Miundombinu ya kiuchumi, Taasisi za fedha, rasilimali watu, viwanda, usafirishaji, utalii na huduma.

Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji pamoja na Taasisi zake inaendelea kuwahakikishia wawekezaji kuwa itaendelea kuratibu masuala ya uwekezaji ili kuhakikisha wanakuwa na mazingira wezeshi ya uwekezaji.
Labda wawekezaji wa kuuza alkasusu na urojo
 
Hata kipindi cha mwendazake mlimwambia anavunja rekodi kila siku [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Back
Top Bottom