Kipindi cha njia Panda

Nukta5

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2014
Posts
1,182
Reaction score
1,288
Nimesikiliza njia panda ya huyu jamaa ambae anaitwa Musa toka mwanzo had sasa imeniogopesha sana kama haya mambo yapo duniani. Nimeleta hapa jamvin niweze kushare na ninyi wenzangu kama mnaijua vizuri.
 
Inaweza ikawa kweli au uongo maana mambo ya ushirikina kuyaamini ni ngumu mpaka yakutokee mwenyewe.
 
Mimi huyo bwana toka story imeanza nimekua mzito Sana kumuamini hasa pale aliposema kasema amekutana na shetwani mkuu dah ...... nasaivi naona imegeuka biashara tayari hapo ndo nikapoteza imani kabisaaaaa
 
Na wamesema wanatoa movie yake, ila itahitaji technolojia ya hali ya juu ikibid wachukue production movie za south africa kwenye swala la kuruka na Ungo isije poteza maana kati ya story na movie
 
Nimesikiliza yaani nimeogopa vya kutosha duh!! Lkn aliyoyasema nimeshawahi kuyasikia! Hii dunia tusio haina ni mengi sana
 
Tupen umbea bas na sisi
Mleta uzi anadhani wote tumesikiliza hiyo njiapanda!! Tupe kidogo' kilichokufanya uanzishe huu uzi ili tupate pakuanzia ambao hatujasikiliza hiyo njiapanda..
 
Mleta uzi anadhani wote tumesikiliza hiyo njiapanda!! Tupe kidogo' kilichokufanya uanzishe huu uzi ili tupate pakuanzia ambao hatujasikiliza hiyo njiapanda..
Kwa kifupi jamaa alikuwa anaelezea historia yake jinsi alivyokuwa anasaka maisha mazuri kwa kuanzia ujambazi had kuja kutumia njia za kishirikina hadi kufikia kumuua mtto wake kuchukuwa watu misukule, kula nyama za watu had kuruka na ungo pia hata kusababisha ajali za barabaran kutumia njia za kichawi, kushuka kuzimu daa naomba mwingine aliyeckiliza aendelee kuweka ambavyo cjaweka
 

Ukiwa mcha MUNGU mambo kama hayo hayakutishi wala kukushtua,
Mtegemeeni bwana katika maisha yenu yote.
 
We acha tu Mdau mpaka Ajali ya Juzi Makongo nikasema ndio Jamaa wametengeneza nini ? Hii Dunia hii Inamambo ya Ajabu sana
 
Nilimsikia mara moja nikaona kama fix zimezidi... nikaghairi kuendelea kumfuatilia!
 
Nilimsikia mara moja nikaona kama fix zimezidi... nikaghairi kuendelea kumfuatilia!

Kwa wanaomjua wanasema ni kweli huyo jamaa alikuwa hivyo
 

Kwahiyo kashazipata hizo faranga? Hilo litakuwa kubwa jinga. Over!
 
Kwahiyo kashazipata hizo faranga? Hilo litakuwa kubwa jinga. Over!



azipate wapi mi fix kibao hata mtt mdogo anakushitukia yaani kunasehemu hadi alikuwa anabug inabidi wapige tangazo sasahiv eti wanauza tape Zake sasa sijaelewa wanataka kuwafunza raia ushirikina nini
 
Kwa wanaomjua wanasema ni kweli huyo jamaa alikuwa hivyo
binafsi sikatai suala la ku-hustle kwa staili anayoelezea bali ninachokana mimi ni yale mambo yenyewe! Mathalani, sehemu ambayo mie niliacha kumsikiliza ni pale aliposema kwamba alipewa dawa kisha akafanya tukio! Kati kati ya tukio, wajomba wakatokea... zikaanza kupigwa shaba! Jamaa akasema risasi zilikuwa zinadunda tu mwilini... RISASI? KUDUNDA MWILINI? asin'tanie... hofu yangu ni kwamba sehemu kama hizo alikuwa anachezewa viini macho tu na hao waganga wake... anajiona anapiga tukio, kumbe yupo usingizini... anajiona anakula shaba live, kumbe viini macho... unaweza kuroga vyote lakini sio risasi jombaa... kitu lethal kina-fail kupenya kwenye medium yenye mautundu ya kisayasansi lakini si haya mautundu yetu!!!
 

Kwenye uchawi inawezekana
 
Ni utapeli tuu, hakuna lolote....niliwahi kuwalaumu RFA kuendekeza stori za hawa jamaa , na sasa naona Maro naye anaingia kwenye mkumbo huo.

Kuaminisha watu kuwa kuna binadamu anaweza kukutana na shetani, au kati ya wanaokufa kuna wanaochukuliwa kimazingara....huu ni ujinga mtupu na ni aibu kutumia chombo kikubwa cha habari kueneza ujinga wa aina hii.

Kuna redio za mikoani nazo zina vipindi kama hivi, na utamsikia binti wa miaka kumi na mbili anaelezea jinsi alivyokuwa anaishi na misukule na kula nyama za watu.

Unless dokta Isac awe anatumia kipindi chake kutengeneza mkwanja kupitia hawa matapeli, na sioni sababu ya kufanya hivyo coz kuna watu wana stori za ukweli (uhalisia)...na zinasisimua kusikiliza aachane ni hizi za kitapeli.
 
Hicho kipindi kinakosa mwelekeo sasa, maana halisi ya njia panda hata siioni tena, kuna watu walikuwa wanakuja hapo na wako njia panda kweli, na wanaeleweka, na msaada pia wanapata, lakini ss hv wanakuja wahuuni tu na mistori yao ya uongo tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…