Kipindi hiki ni cha kufunga mkanda haswa

Kipindi hiki ni cha kufunga mkanda haswa

Bushmamy

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2019
Posts
9,140
Reaction score
15,963
Karibu kila Mwananchi anajionea hali jinsi ilivo mtaani, ngano bei juu, mafuta ya kupikia,mchele,nk. kulinganisha na hali ya pesa mtaani ilivo mbaya wengi wanashindwa kununua mahitaji ya msingi nyumbani

Watu wamekuwa wakilalamika kwenye mitandao bila kujua wafanyeje maana kilio Chao kimekuwa kikiishia hewani tu, kulia sana mitandaoni haitaondoa hali halisi iliyopo hivyo ni bora kufunga mkanda haswa.

Ulevi, kulingana na hali ilivyo mitaani watu wazima na vijana wameamua kunywa pombe za bei rahisi kuanzia 500 alewe ilimradi kujitibu na stress,. Maana wengi wao hawaijui kesho yao.

Uraibu wa mtandaoni, vijana wengi kutokana na Kukosa ajira. Kayumba kibiashara,pesa kidogo wanayoomba kwa wazazi, ndugu huitumia kwa vocha kushinda mitandaoni ilimradi tu kujipa furaha maana furaha ya kweli mitaani na kwenye familia hakuna.

Viwanda vidogo kwa vikubwa vimekuwa vikijitahidi kutengeneza pombe kali tena za bei rahisi na hii ni Kutokana na uhitaji wa soko lenyewe na pombe hizi mwisho zinaleta athari kwa watumiaji.

Vijana ambao ni nguvu kazi kwa Taifa wamekuwa wakifanya juu chini kwenda Ng'ambo wakiamini ni bora zaidi kuondoka nchini kuliko kuendelea kuumia nchini kwao.

Viongozi wetu kwa sasa hawana msaada wa moja kwa moja kwa wananchi na hii imesababisha kuwa na mstari mkubwa kati ya viongozi na wananchi, kwani wananchi wamekuwa wakipapambana wenyewe kiuchumi, kiafya hadi kilimo.

Hali ni Ngumu kweli wote yatupasa kufunga mkanda huku tukiamini kuwa baada ya muda uchumi unaweza kukaa sawa hivyo tuwe wavumilivu
 
We angalia fursa ambazo zipo mtaani,acha kulalamika

Kama kuna unywaji mkubwa wa pombe za bei che,basi wewe kuwa dalali uwauzie hao maskini

Fursa haziishi,ni wewe tu kuziangalia
 
2025 watamchagua raisi huyuhuyu aliyekuwa madarakani trust me!!! Mara nyingi hapo huwa baada ya kupewa doti za khanga na kofia za kijan
 
Yaani katika kitu ambacho tunakosea ni kupandisha bei za vyakula nchi kama Dubai ni jangwa ila utakosa vitu vyote ila sio msosi yaani hapo kupanda bei za vyakula kama nchi tunayumba sana ndio maana ukuwaji wetu ni tofauti na nchi nyingine angalia hapa zikija team za kigeni kucheza unaona jamaa wameshiba wameenda hewani kuliko Sisi hata Somalia kwenye vita wanaonekana wanakula vizuri kuliko Sisi tatizo hii nchi ina wapiga deal wengi sana na ukitaka vita waguse.
 
Yaani katika kitu ambacho tunakosea ni kupandisha bei za vyakula nchi kama Dubai ni jangwa ila utakosa vitu vyote ila sio msosi yaani hapo kupanda bei za vyakula kama nchi tunayumba sana ndio maana ukuwaji wetu ni tofauti na nchi nyingine angalia hapa zikija team za kigeni kucheza unaona jamaa wameshiba wameenda hewani kuliko Sisi hata Somalia kwenye vita wanaonekana wanakula vizuri kuliko Sisi tatizo hii nchi ina wapiga deal wengi sana na ukitaka vita waguse.

Kama hutaki vyakula vipande bei nenda kalime. Hivi wakulima mnatuchukuliaje!
 
Kama hutaki vyakula vipande bei nenda kalime. Hivi wakulima mnatuchukuliaje!
Kinachosababisha chakula kipande bei sio wakulima ila baada ya kutoka kwa mkulima kila mtu anafanya anavyotaka Kwan wakulima mpaka leo wanapata wanavyostahili kupata kweli?
 
We angalia fursa ambazo zipo mtaani,acha kulalamika

Kama kuna unywaji mkubwa wa pombe za bei che,basi wewe kuwa dalali uwauzie hao maskini

Fursa haziishi,ni wewe tu kuziangalia
Na hii tabia ya Ubinafsi umimi ndio part ya matatizo tuliyonayo..., As an individual mtu hata Syria au Somalia unaweza ukatoboa.., ila kama jamii kuondokana na hizi shida inahitajika Sera ambazo zinajumuisha majority...

Unadhani hata wewe ukiwa dalali ukapata hizo pesa za kumwaga kama wanaokuzunguka hawana kitu unadhani utapata muda au amani ya kutumia hizo pesa zako ?

Au utatumia lumpsum ya hicho ulichokipata kwa jasho kuweka ulinzi ili kujilinda ? (In short hata wewe utakuwa hauna enjoyment zaidi ya kuishi kwenye Rat Race)
 
Ukiona ndani ya nyumba Baba au mama anakopa sana au anaomba misaada sana kwa majirani na matajiri lazima watoto ndani ya nyumba mjue kuwa hali ndani ni mbaya.
 
Back
Top Bottom