Chizi Maarifa
JF-Expert Member
- Jul 29, 2013
- 10,931
- 24,816
Tulikuwa busy sana na kuandaa namna ya kuwabeba akina kisinda, Sarpong, Hersi, Mukoko n.k hii ilinipa shida kiasi kikubwa sana kwa ile imani kuwa tumesajili team kabambe na hakuna team ambayo itatuzuia. Huu wazimu nikikumbuka huwa naumia sana maana nilikuwa mmoja ya watu ambao walipinga sana jambo hili.
Nikaonekana mimi ni mamluki nk. niliwauliza wenzangu kama sisi wenye akili tukichambua mnatuzogoa na kusema kuwa ni mashabiki au mamluki wa Simba je, hii maana yake ni kuwa wenye akili ni Simba tu?
Utamaduni wa kuwabeba wachezaji na viongozi uliasisiwa msimu huu kwa makusudi maalum. Sisi wenye akili tulifahamu kilichokuwa kinaendelea. ni suala la siasa chafu za mpira. Niliwahi waambia GSM maneno flani kuwa wawe serious na uwekezaji wao. kiukweli tunataka wawekezaji ambao wana nia ya dhati ya maendeleo ila si wajanja wanjanja na wenye kutufanya sisi hatuna akili.
Simba walipoteza matches mbili kipindi ambacho sisi tulikuwa hatujapoteza match hata moja. Waliendelea kujenga utulivu. kwa team kama ya Simba ilikuwa rahisi kuamini kuwa haitotokea kupoteza match hata moja.
Walipoteza wakakaa na kuangalia tatizo nini wakajirekebisha. Hukusikia wakilalamikia waamuzi kwenye press au TFF ingawa kuna match kama ile ya T Prisons kiukweli kuna uhuni mwingi ulifanyika. Waliendelea na ligi wakijua kila kitu kinaweza kutokea.
Sisi tulipomleta Kaze ilikuwa issue Duniani nzima ikajua tumemleta Kaze. tukampa mzigo mkubwa sana kisaikolojia tulimwathiri. lakini pia GSM imetengeneza matabaka kwa wachezaji. Kwa sasa kuna wachezaji wa GSM na wachezaji wa Yanga ya Msolla.
Haya yamekuwa matatizo. Kuna wachezaji wanacheza Yanga lakini hawana furaha ya kuwa Yanga. wengi tu nafahamu kuna baadhi ya wachezaji wanatamani sana kwenda SIMBA na wanacheza kwa nia kubwa ya kwenda Simba. wapo. kuna wachezaji hawana mikataba ya ukweli. Hawa wapo Yanga kwa ajili ya kutafuta soko la Kisoka. wachezaji wengi wa nje hamna kitu kinachoeleweka pale Yanga.
Yanga tunapaswa kutulia na kujipanga kuangalia ni wapi tulianguka. ingawa pia kuna maneno mengi sana kuhusiana na Senzo. Yapo nachelea kutoyasema haya sababu sitaki kuleta taharuki. Ila ni kipindi cha kuangalia sana wahujumu wa Yanga wamo ndani ya Yanga kwa Maslahi binafsi na kwa maslahi ya makundi yao. Tujipange team icheze bila pressure matokeo yatakuwepo tu. Lakini kuiweka team katika pressure ni kuukosea sana mpira wa Miguu tunashindwa elewa mpira wa miguu una nidhamu yake.
Nikaonekana mimi ni mamluki nk. niliwauliza wenzangu kama sisi wenye akili tukichambua mnatuzogoa na kusema kuwa ni mashabiki au mamluki wa Simba je, hii maana yake ni kuwa wenye akili ni Simba tu?
Utamaduni wa kuwabeba wachezaji na viongozi uliasisiwa msimu huu kwa makusudi maalum. Sisi wenye akili tulifahamu kilichokuwa kinaendelea. ni suala la siasa chafu za mpira. Niliwahi waambia GSM maneno flani kuwa wawe serious na uwekezaji wao. kiukweli tunataka wawekezaji ambao wana nia ya dhati ya maendeleo ila si wajanja wanjanja na wenye kutufanya sisi hatuna akili.
Simba walipoteza matches mbili kipindi ambacho sisi tulikuwa hatujapoteza match hata moja. Waliendelea kujenga utulivu. kwa team kama ya Simba ilikuwa rahisi kuamini kuwa haitotokea kupoteza match hata moja.
Walipoteza wakakaa na kuangalia tatizo nini wakajirekebisha. Hukusikia wakilalamikia waamuzi kwenye press au TFF ingawa kuna match kama ile ya T Prisons kiukweli kuna uhuni mwingi ulifanyika. Waliendelea na ligi wakijua kila kitu kinaweza kutokea.
Sisi tulipomleta Kaze ilikuwa issue Duniani nzima ikajua tumemleta Kaze. tukampa mzigo mkubwa sana kisaikolojia tulimwathiri. lakini pia GSM imetengeneza matabaka kwa wachezaji. Kwa sasa kuna wachezaji wa GSM na wachezaji wa Yanga ya Msolla.
Haya yamekuwa matatizo. Kuna wachezaji wanacheza Yanga lakini hawana furaha ya kuwa Yanga. wengi tu nafahamu kuna baadhi ya wachezaji wanatamani sana kwenda SIMBA na wanacheza kwa nia kubwa ya kwenda Simba. wapo. kuna wachezaji hawana mikataba ya ukweli. Hawa wapo Yanga kwa ajili ya kutafuta soko la Kisoka. wachezaji wengi wa nje hamna kitu kinachoeleweka pale Yanga.
Yanga tunapaswa kutulia na kujipanga kuangalia ni wapi tulianguka. ingawa pia kuna maneno mengi sana kuhusiana na Senzo. Yapo nachelea kutoyasema haya sababu sitaki kuleta taharuki. Ila ni kipindi cha kuangalia sana wahujumu wa Yanga wamo ndani ya Yanga kwa Maslahi binafsi na kwa maslahi ya makundi yao. Tujipange team icheze bila pressure matokeo yatakuwepo tu. Lakini kuiweka team katika pressure ni kuukosea sana mpira wa Miguu tunashindwa elewa mpira wa miguu una nidhamu yake.