Kisa cha Adam Mchomvu kumuumbua Fid Q kwenye Interview ni nini?

Kisa cha Adam Mchomvu kumuumbua Fid Q kwenye Interview ni nini?

Adam ni janga nyingine hapo clouds wote mashosti.
 
Hi good people,

Leo wakati msanii Fareed Kubanda - Fid Q yuko ndani ya XXL ya Clouds fm anatambulisha ngoma yake mpya inaitwa Bongo Hip Hop, mtangazaji Adam Mchomvu amekuwa anambana na maswali sana kiasi cha Fid kumtolea uvivu kuwa "najua umeagizwa kuja kuni-harass kwenye interview yangu".

Adam alikuwa anambana sana na maswali ya kwanini amerudia ngoma hii kutoka Tongwe Records aliyomshirikisha Juma Mohamed Mchopanga (Jay Moe) na kuirudia Bongo Records akimshirikisha P.Funk Majani?

Adam anaonekana kumind hii kitu kiasi cha kulazimisha kuipiga ngoma ile version ya mwanzo ya Tongwe baada ya hii version ya Bongo Recz kumalizika (ingawa kibishi sana maana B12 alikuwa anataka kubana. Ila kabla ya ngoma kuisha B12 akaikata na Adam anasikika akimind na kusema kesho atashusha mzigo mwingine.

Kilichonipa maswali hapa ni Je Adam ni ile loyalty yake ya kuwa Record Label kule Tongwe Records ama ana ubia kule Tongwe ndiyo sababu ya kuishupalia hii kitu namna hii? Hebu mwenye idea na hii kitu atujuze wadau.
Huyu mtu anaonelana ana historia ya kuvuruga wenzake lakini yeye hataki kuguswa na hoja.

Violence has never been an option
 
Back
Top Bottom