Kisa cha aliyegongwa na mwendokasi (Osman): Kinahuzunisha, kinafundisha na kushangaza

Kisa cha aliyegongwa na mwendokasi (Osman): Kinahuzunisha, kinafundisha na kushangaza

Dereva gari dogo alikuwa na stress za mapenzi ehh...na mke wake [emoji848]

Wazee wa kata ndoa mmeiona hii

Ova
Ndio uhalisia huo kiongozi! Ndoa ni mateso! Ndoa ni njaa?doa ni tabu ndoa ni kifo! Faida kuwa kwenye ndoa ni chache,hasara ya kuwa kwenye ndoa ni kubwa,kataa ndoa.
 
Hii ndio hoja na hasa baada ya kujua serikali Ina mkono wake
Siyo kila mtu ana smart phone na si kila mmoja hufuatilia media hapa tz, mwamba Osman ni baharia, ngumu kufuatilia maisha ya baharia
 
Up to all yule jamaa wa gari ndogo alikamatwa?, maana kwenye sinema hapo anaonekana alimenya mbuga kwa speed kubwa sana.
Lile pigo lilimtoa kwenye control ya gari na kupelekeshwa uelekeo ambao hakuwa anaelekea. Sio kwa kupenda.
 
Huenda Osman aliaga anaenda Mtwara atakaa wiki 2 ndipo arudi Dsm.
Vinginevyo familia yake hawako siriaz.
Yaani kwa kifupi hawa jamaa hata mawasiliano ya simu hawana! Sitaki kuamini mume anaweza kuaga anasafiri na asipige simu hata kwa mkewe kumjulisha kuwa amefika salama au hata mke kumpigia simu mumewe kuulizia maendeleo ya safari yake. Umasikini kweli unaleta kutokujali.
 
Huna ukichoandika, ile CCTav haikuonyesha sura na si rahisi kumjua. Na mtu alishaaga anaweza kusafiri na chonbo, sasa wasiwasi utoke wapi
Ina maana mume na mke huwa hawapeani taarifa mmoja anaposafiri kama amefika salama!?
 
Yaani kwa kifupi hawa jamaa hata mawasiliano ya simu hawana! Sitaki kuamini mume anaweza kuaga anasafiri na asipige simu hata kwa mkewe kumjulisha kuwa amefika salama au hata mke kumpigia simu mumewe kuulizia maendeleo ya safari yake. Umasikini kweli unaleta kutokujali.
Wazee siyo kila mtu anazo hizo jerojero za vocha
 
Nilichojifunza hapa ni kuwa ukiwa masikini unakuwa huna ndugu WA karibu,

Watu wanakupa thamani ya chini sana

Ndio maana vijana wengi wanasaka Hela za ndumba.
Hili ndio jibu ukiwa huna hela watu wanakua hawana mpango na wewe hata demu wako hakujulii hali had uanze....
Ni kawaida tu ukifulia kukaa siku nzima simu haijaita so unaeza potea watu wakastuka baadae sana
 
Ajali ya mwendokasi ilyotokea wiki moja iliyopita maeneo ya kisutu ina shangaza mengi!

Ajali ile ilitokea majira ya asubuhi na kuhusisha gari dogo kugongana na mwendokasi ulikochangia majeruhi kadhaa akiwemo bwana mmoja aliyekuwa mtembea kwa miguu (Osman)

Taarifa za vyombo vya habari, report za hospital na report za kipolisi zilieleza wazi kila kitu kilichojili (sitarudia)

Takribani karibu siku saba baadae zimepita hadi Jana 27 February 2023! Taarifa za hospital ziliendelea kueleza HAKUNA MTU aliyejitokeza kwenda kumtambua mhanga wa ajali (bwana OSMAN)

Baada ya taarifa ya hospital kutaja kwamba yule mtu kazinduka! Ufahamu umerejea! Leo tarehe 28 ndipo Tunamshuhudia mke wa Osman pamoja na ndugu akijitokeza kumtambua (Yote ni kheri ya Mungu).

Tunashukuru ndugu wamepatikana, lakini kupatikana kwao kwa vyovyote vile kunaibua maswali mengine ingawa tunashukuru wamepatikana!

Simulizi za mke wa Osman!

Mama huyu kwa mara kwanza kasikika akisimulia kwamba hakuwa na taarifa Yoyote hadi pale shemeji yake jana alipomtaarifu kwamba, Taarifa za hospital zinazomtaja OSMAN (wanahisi Osman anayetajwa kupata nafuu hospital ni ndugu yao)!

Mke wa OSMAN Anaendelea kusimulia kwamba, Siku ya tukio, mmewe alimuaga kama kawaida yake kwamba anakwenda kibaruani (kwamba OSMAN anajishughulisha na kubeba mizigo hapo Ferry) kwamba alimuaga kuwa huenda anatarajia kusafili na chombo siku hiyo kwa siku kadhaa!

Haya ni maelezo ya mkewe OSMANI!

Maelezo hayo yanaukweli mwingi kwamba huenda ni kweli kwamba alijua mme wake kasafili ndiyo maana hakuwa na wasiwasi kwamba atarudi!

Lakini maelezo hayo hayawezi kuwa kweli pasipo kusindikizwa na style yao ya maisha, history, uhusiano wao kama familia!

Ni kweli alisafili kama alivyoaga, je baada ya siku ya kwanza, ya pili ya tatu mke na ukoo wao wote na majilani hawakuona ya mtandaoni kiasi cha kushituka?
Sawa mke hana simu je majilani na ndugu hawakuona angalau kufananisha fananisha?

Majibu ya hayo yote ni mepesi tu kwamba UMASKINI HULETA TABIA YA KINYAMA!
Ninaposema tabia ya kinyama sina maana tabia ya kikatili bali namaanisha Umasikini huzalisha tabia yakutojali!

  • YAMKINI KWASABABU YA UMASKINI huenda ndugu na jamaa waliamini yule jamaa kakata moto hivyo wakaamua kukausha! (May be)
  • YAMKINI kwakuogopa bili ya hospitali (gharama za matibabu) mke,ndugu na jamaa waliamua kukausha! (May be)
  • YAMKINI kwa tabia za maisha yao ni kama UMEME WETU, kwamba mme akiondoka haagi na akirudi tunashangilia huooo! (May be)
  • YAMKINI SASA BAADA YA KUSIKIA KAZINDUKA (OSMAN) Familia na ndugu wameogopa kwamba atawaumbua kwa kuwataja! Hivyo sasa wamejitokeza chapu! (May be)
  • YAMKINI huyu wameona huyu mtu kapona sasa huenda kuna matunda mbele ya misaada (may be)

Tunashukuru ndugu wamepatikana lakini YAMKINI ...na may be ....Havitaacha kugonga vichwani mwa watu wengi.

Yote kwa yote mipango ya Mungu haina makosa , Na kila uzao hauwezi kupatikana pasipo kutungwa mimba!

Ajali ya mwendokasi ilikuwa mimba ya kumuumba OSMAN MPYA!
Mimba ile ilutungwa kwa mwenye gari dogo! Taarifa za kipelelezi zinaonesha yule mwenye gari dogo alikuwa na mgogoro na mkewe uliomjaza stress!
Stress za mapenzi kwa dreva wa gari dogo zilimfanya apoteze umakini barabarani (uzembe)

Hadi pale alipokatiza hovyo na kugonjwa na mwendokasi! Kulikopelekea gari la mwendokasi kwenda kumgonga bwana OSMAN!

MBIO ZA YULE MLINZI HAZIKUWA NA FAIDA, BALI MIMBA Ile ilikuwa kwa ajili ya kumzaa OSMAN MPYA!

Tumuombee apone mapema!

USHAURI!
1. HOSPITALI ZINAPOTANGAZA KUTAFTA NDUGU wasiache kutamka wazi kwamba HAKUNA DENI WALA BILI KWA NDUGU! Ikiwezekana anayejitokeza waseme watamsaidia kumsafilishia mgonjwa hadi nyumbani! (Hili litasaidia watu wasiwe wanauchuna na kutelekeza ndugu na jamaa)
2. NIDA wapoleshe taarifa za vidole na database! Kwamba alama za vidole ziwekwe kwenye kanzudata ya taifa ili hospital wakiskani vidole taarifa za mtu na ndugu zijazwe huko

Heri maskini wa roho kuliko maskini wa mali maana ni rahisi sana kukosa ufalme duniani na mbiguni!

Tubuni na kuiamini injili
Samahani mkuu umeshawahi kukaa uswahilini na maanisha uswazi kweli mke hana simu mume hana simu mume anaondoka kwenda, kutafuta kibarua akipata sawa akikosa sawa na ndo mtindo wao wa maisha akiondoka atarudi tuu kwa sababu Niko uswazi familia kama hizo nyingi mwingine alizikwa mpka na manispaa mke hajui
 
Ishu ya information kusaka taarifa ni kwa zile Jamii zilizostaarabika. Na sio uswahili wao uchagua taarifa za kuzifatilia.
Umasikini unaleta roho mbaya
Kweli, tunaona watoto wa kishua wanapelekwa school, mguu kwa mguu hadi getini, hata shule ikiwa mita chache toka nyumbani, sisi masikini hatuna time, mtoto anapiga makasia kuvuka mto kwenda shule mwenyewe
 
Lile pigo lilimtoa kwenye control ya gari na kupelekeshwa uelekeo ambao hakuwa anaelekea. Sio kwa kupenda.
Ukiangalia footage ya sinema utaona jamaa alikanyaga mafuta na kusepa, inaonekana alijua kachemka so bora akamatwe siku nyingine akiwa katulia ila siyo siku ya tukio damu ikiwa inachemka!.
 
Ukiangalia footage ya sinema utaona jamaa alikanyaga mafuta na kusepa, inaonekana alijua kachemka so bora akamatwe siku nyingine akiwa katulia ila siyo siku ya tukio damu ikiwa inachemka!.
Hapana ile gari baada ya kupigwa ilikwenda wangu wangu ikikosa kosa watu mpaka ilipoenda kusimama kwenye kituo cha mafuta pale Kisutu palipo pia na kituo cha basi cha mwendo kasi. Ni kwa vile hakuna footage ya matukio ya kule gari ndogo ilipoelekea. Kwa ule mzinga aliopigwa hiyo akili ya kuendesha gari akikimbia angeipata wapi!?
 
Maelezo ya mke wa Osman yana mashiko sana wavuvi wakiondoka na chombo hukaa Hadi wiki na zaidi na bahati mbaya baharini ama baadhi ya visiwa network sio nzuri ama hamna kabisa.

Kuhusu taarifa mpaka Osman anatoka ICU kulikua hamna picha yake halisi hata wewe sasa hujaona picha ya Osman na cctv haijatoa muonekano vizuri wa Osman

Baada ya kutoka ICU alivyotaja jina na anapotokea ilikua ni rahisi kWa ndugu kuhisi yawezekana ni ndugu Yao.
 
Umeandika vyema. UMASIKINI NI MBAYA SANAA!Tupambane wakuu tusiache pia kuwashika ndugu mikono angalau ukoo uwe na ahueni. Fikiria tu mimi niliyepo Kijijini huku KITEFU -Meru nimeona taarifa yake na kuifuatilia ila ndugu wa hapo tu wamekausha mpk jana, ingekuwa family inayojiweza lazima tu siku ile ile ingejua kutoweka kwa ndugu yao.UMASIKINI UNAFANYA UWEPO WAKO USITAMBULIKE.
 
Maelezo ya mke wa Osman yana mashiko sana wavuvi wakiondoka na chombo hukaa Hadi wiki na zaidi na bahati mbaya baharini ama baadhi ya visiwa network sio nzuri ama hamna kabisa.
Kuhusu taarifa mpaka Osman anatoka ICU kulikua hamna picha yake halisi hata wewe sasa hujaona picha ya Osman na cctv haijatoa muonekano vizuri wa Osman
Baada ya kutoka ICU alivyotaja jina na anapotokea ilikua ni rahisi kWa ndugu kuhisi yawezekana ni ndugu Yao.
Pia wanawake wengi wana viswaswadu, hawana vishkwambi kama angeona footage,,
Nyumba zingine hazina tv,, miaka hii sio kama ya zamani miaka ya 90,watu walikua wanawahi saa mbili hata baa za jirani kuangalia taarifa ya habari ya ITV,, Wakati wanasubiri kuangalia tamrhilia za kina Seki😁
 
Ni uzembe tu wangetaka mjua wangemjua kupitia NIDA, NEC finger prints
Nduu yangu wapo watu umri wa 35+ hawana kitambulisho chochote iwe NIDA (Uraia) , NEC (Kura) au leseni ya udereva au NHIF.
Wapo wengi tu nawafahamu na wengine hawana simu pia.
 
Back
Top Bottom