Kisa cha Kweli: Sitasahau nilivyopendwa na mchawi nikaishia kurogwa

Kisa cha Kweli: Sitasahau nilivyopendwa na mchawi nikaishia kurogwa

Inaendelea sehemu ya 3

Baada ya matukio hayo kupita maisha yaliendelea kama kawaida. Baadae baba yangu alikuja kupona ugonjwa wa akili uliokuwa unamsumbua. Baada ya kupona alienda kuuza eneo ambalo tuliliacha kule Bunda, akaja kununua eneo pale kijijini. Akafyatua na tofali na kuzichoma baadae akajenga nyumba ndogo ya vyumba viwili na sebule maarufu kama mgongo wa tembo na nyumba nyingine akajenga ya tope na bati zilizoezekwa kwa mtindo wa flat hujulikana zaidi kama "slope". Tukaanza kuishi pale, tuliendelea na maisha kama kawaida wakati huo nikiwa darasa la tano mwaka 2007, tukijikita hasa hasa kwenye shughuli ya kilimo. Na huo ndio mwaka ambao babu alifariki dunia (RIP). Niliendelea na shule hadi nikamaliza darasa la saba, baadae nikajiunga na sekondari katika shule ya kata iliyokuwa katika kijiji cha mbali kidogo na Kijiji chetu ambako ndio ilikuwa kata yetu. Ili kufika mahali kata ilipo ulikuwa unavuka kijiji kimoja katikati ndio unafika, umbali sio chini ya masaa matatu kwa mwendo wa mguu. Hivyo vijana ambao tulitoka vijiji vya mbali tulilazimika kupanga vyumba hapo katani, ili kupunguza umbali wa kwenda shule. Vyumba hivyo vijana waliita "ghetto" sio kama la Mangwair lakini lenye kapeti manyoya, mashine ya dry cleaner na kistudio cha kiaina. La kwetu lilikuwa na godoro lisilo na kitanda, vyombo vichache kwenye beseni, kibatari na vimadaftari vya kiaina hakuna duu ambaye lingeweza kumchengua.

Ilipita miaka mingi nikiwa sijashuhudia tukio lolote la kishirikina, kiasi kwamba hadi kumbukumbu za tukio lile zikawa zimeshafutika. Mambo yalikuja kubadilika nilipokuwa sekondari. Nikiwa ndio niko likizo ya mwisho wa mwaka kuingia kidato cha tatu. Nakumbuka ilikuwa likizo ya mwisho wa mwaka kama sikosei ni either ilikuwa mwezi wa 12 mwaka 2011 au tarehe za mwanzo wa mwaka 2012. Kulikuwa na mechi ya Arsenal sikumbuki vizuri ilicheza na timu gani, lakini ilikuwa ni mechi ya ligi kuu. katika ile mechi Arsenal ilishinda 2-1 magoli ya Arsenal yalifungwa na Van- Persie kwa penalty na Benayoun dakika za mwishoni. Kipindi hicho kocha wa sasa wa Arsenal Michael Arteta bado anakipiga uwanjani. Sasa mimi huwa ni shabiki wa damu wa hii timu tokea enzi za mzee Wenger. Sasa kama unavyojua mazingira ya kijijini kulikuwa hakuna umeme hivyo mechi tulikuwa tunaenda kuangalia centre yaani yalipo maduka. Kuna jamaa alikuwa na banda la video anatumia generator linalopiga kelele kama mziki wa Young Lunya. Kulikuwa na umbali kidogo kutoka nyumbani hadi huko madukani umbali kama wa nusu saa kwa mwendo wa mguu. Sasa wakati naenda kucheki mechi nilikuwa na washikaji zangu watatu, sasa mechi ilivyoisha nataka nirudi nyumbani nikawa siwaoni. Na ilikuwa ni usiku kama saa sita hivi, kumbe jamaa walichoka kuangalia mpira wakaondoka kimya kimya Sasa ikabidi nirudi peke yangu, maana kitongoji chetu hakikuwa na watu wengi wapenzi wa mpira. Hivyo wengine waliokuwemo mle bandani sio wa maeneo ya kwetu.

Njia tuliyokuwa tunapita ina miti vichaka na nyumba za mbalimbali. Nikaanza kutembea peke yangu usiku ulikuwa kimya Kweli Kweli ni sauti ya upepo na wadudu tu ndiyo vilisikika. Kuna sehemu nikafika huwa hakuna nyumba kwa umbali kama wa mita mia mbili hivi ila kuna miti mingi sana na vichaka vichaka. Wakati natembea nikawa nasikia vishindo vya mtu kwa nyuma, kama yuko nyuma yangu umbali mdogo tu anakuja. Nikageuka kuangalia sikuona kitu, niliogopa kidogo lakini nikaendelea na safari nikidhani labda ni mawenge ya usiku tu. Nilipoanza kutembea nikaanza kusikia tena, safari hii kwa karibu zaidi kuliko mwanzo ni kama mtu alikuwa yuko mita chache sana nyuma yangu. Aiseee! Mapigo ya moyo yalienda kasi sijapata kuona!. Haraka haraka nikageuka tena kuangalia lakini sikuona kitu. Aisee nilitimua mbio zaidi ya Hussein Bolt! Nilikimbia kwa mwendo kama wa dakika tatu, nikashangaa kwa mbele yangu nikamuona mtu anatembea. Nikasimama ghafla kusoma kumuangalia nilikuwa naogopa sana nisingemuamini yeyote tena. Nilivyomuangalia, nikabaini alionekana kama mwanamke bibi mzee sana anatembea polepole kwa kujivuta kizee amevaa nguo zilizoonekana nyeusi tii. Niliweza kuona vizuri kwa sababu alikuwa mita chache sana! Akili iliniambia ndio walewale Kuona hivyo nilibadili njia kwa kasi na kuanza kukimbia huku nikipita kwenye mashamba nikikimbia hovyo. Kwa sababu nilikuwa mwenyeji haikunisumbua kukimbia nikikatiza kuelekea uelekeo wa nyumbani.

Nilikimbia bila kuchoka umbali mrefu sana, wakati nakaribia sasa kufika home. Nikaikamata sasa barabara inayonyoka kuelekea nyumbani. Nikawa kama nimechoka kukimbia nikawa natembea ila kwa kasi Sana ! Nilishtuliwa na sauti ya mwanamke wa makamo ikiniita!

"We mtoto" alisema yule mwanamke tena kwa kiswahili

Nilishtuka na kuanza kupepesa macho ili nione ile sauti ilitokea wapi. Nilipigwa na butwaa nilipomuona mwanamke amechuchumaa pembeni ya barabara amevaa nguo nyeusi amejifunika hadi usoni huku akiniangalia.

" We mtoto haunisikii"

Mr the Dragon nikakaa kimya. Wazee wetu walitufundisha ukisikia unaitwa usiku hata na mtu unayemfahamu usiitike ovyo. Wakati mwingine wachawi wanaweza kutumia uchawi wao kuigiza sauti hata ya mtu unayemfahamu na wakakuita. Ukiitika tu wanachukua sauti yako inakuwa rahisi wewe kulogwa. Kwa hiyo nilichagua kukaa kimya. Sikuweza kukimbia ni kama mwili ulikuwa umepigwa ganzi.

"Wewe mtoto kwa nini unatembea tembea usiku"

Mimi kimya!

"Usirudie tena kutembea usiku,potea hapa haraka"

Aisee hizo mbio nilizotoka nazo nadhani ingekuwa ni kwenye mashindano ya Olympic mita mia ningeweza kuibuka na gold medal. Nilikimbia hadi nyumbani nikamkuta brother wangu ninayemfata amelala. Nilimgongea mlango akafungua nikaingia ndani.

"Mbona unahema hivyo"

"Nimekuja peke yangu nilikuwa nimeogopa nikawa nakimbia" niliamua kuficha

"We nae muoga sana" alisema huku akipanda kitandani kulala.

Na mimi nilipanda kulala, usingizi ulikuwa wa mang'amung'amu sana, usiku mzima nilifikiria mambo yaliyotokea siku hiyo. Tukio la kusimamishwa na yule mwanamke ndio lilinitisha zaidi. Yule mwanamke alikuwa anatisha vibaya mno. Niliwaza Yule mwanamke atakuwa nani lakini sikupata jibu, nilijaribu kuikumbuka sauti yake na kuangalia kama nilishawahi kuisikia pale kijijini lakini niliambulia patupu. Kesho yake niliendelea na kazi kama kawaida, sikumwambia yeyote kuhusiana na tukio lile. Kuna muda mama yangu alihisi kulikuwa na shida na kuniuliza kama kulikuwa na shida lakini niliamua kuficha, sikumwambia chochote.

Baada ya siku kadhaa shule ilifunguliwa, sasa ukawa muda wa kurudi kwenye kile kijiji ambako shule ilipatikana yaani katani. Nilitembea nikiwa na washikaji na mabinti tuliokuwa tunasoma nao hadi tukafika. Getto kwetu tulikuwa tunaishi mimi na marafiki zangu wawili, jumla tukawa watatu. Hao wote nilisoma nao tokea shule ya msingi Mwanono. Usiku nikiwa nimelala niliota ndoto moja iliyonitisha kidogo.

Niliota mimi ni mtu mzima kidogo ambaye nilikuwa nimeshaondoka kijiji cha Mwanono nikaenda mjini kuishi huko. Nikaishi miaka mingi bila kurudi pale kijijini, sasa siku hiyo nikawa nikawa ndio nimerudi sasa kwa ajili ya kusalimia ndugu jamaa na marafiki. Kwenye ndoto niliota nimeshushwa na bodaboda pale madukani Mwanono nikapokelewa Kwa bashasha na marafiki zangu kitambo hapo kijijini ambao niliwakuta pale centre. Tukaanza kupiga story mbalimbali, miongoni mwa mazungumzo jamaa wakaanza kuniambia Mwanono Sasa hivi pamebadilika pamekuwa mjini, itabidi tukutembeze ujionee. Wakati tukiwa tunaendelea na mazungumzo hayo alikuja pale msichana mmoja niliyemfahamu vyema akiwa na baiskeli akasema

" Nyie mnataka mumtembeze lini, mimi naanza kumtembeza leoleo, hebu Mr the dragon panda hii baiskeli nikubebe nikutembeze" alisema yule msichana

Bila hiyana wala kipingamizi nikapanda baiskeli akanibeba, halafu huyo binti akawa anaendesha. Aliendesha baiskeli kwa dakika kadhaa ikafika sehemu kulikuwa na kona, tulipokunja ile kona tulitokea kwenye mazingira ambayo nilikuwa mgeni kabisa. Nilijaribu kukumbuka pale itakuwa ni sehemu gani kwenye kile kijiji lakini sikupatambua kabisa. Kulikuwa na nyumba nzuri za kisasa na mama mandhari ya kuvutia Sana. Msichana yule aliendesha baiskeli hadi kwenye nyumba moja nzuri sana, kisha akaniambia ingia ndani. ile naingia ndani nikakuta kundi kubwa la watu

Ghafla nikashtuka kutoka usingizini. Niliposhtuka tu nilihisi maumivu mgongoni. Nikajishika nikawa nahisi maumivu ya kuchanwa chanwa mgongoni na kitu chenye ncha kali. Ilibidi niamke nikawasha kibatari kuangalia mgongoni

LAHAULAH!!! nilikuwa na Chale mgongo mzima zikiwa mbichi kabisa na damu kana kwamba ndio nimetoka kuchanjwa na nimepakwa dawa nyeusi na nyekundu. Wazo la kwanza lilikuwa kwenye ile ndoto niliyotoka kuota

Hasahasa msichana aliyenibeba kwenye baiskeli kwenye ile ndoto, ndio yule yule aliniambia mimi ni muoga wakati nilipoona wachawi nikiwa darasa la tatu miaka kama saba iliyopita.

Ndio yule aliyeniambia usiku ule nakimbia wachawi kurudi ndani, wao walienda kula nyama kwenye mkwaju wa kwa mzee Lugota. Yule Yule ambaye tulisoma nae darasa moja na sasa tunasoma darasa moja sekondari. Yule ambaye bibi yake ni mchawi anayeogopeka Kijiji kizima.

Itaendelea tena kesho majira na nyakati kama hizi

Usiku mwema.
 
Inaendelea sehemu ya 3

Baada ya matukio hayo kupita maisha yaliendelea kama kawaida. Baadae baba yangu alikuja kupona ugonjwa wa akili uliokuwa unamsumbua. Baada ya kupona alienda kuuza eneo ambalo tuliliacha kule Bunda, akaja kununua eneo pale kijijini. Akafyatua na tofali na kuzichoma baadae akajenga nyumba ndogo ya vyumba viwili na sebule maarufu kama mgongo wa tembo na nyumba nyingine akajenga ya tope na bati zilizoezekwa kwa mtindo wa flat hujulikana zaidi kama "slope". Tukaanza kuishi pale, tuliendelea na maisha kama kawaida wakati huo nikiwa darasa la tano mwaka 2007, tukijikita hasa hasa kwenye shughuli ya kilimo. Na huo ndio mwaka ambao babu alifariki dunia (RIP). Niliendelea na shule hadi nikamaliza darasa la saba, baadae nikajiunga na sekondari katika shule ya kata iliyokuwa katika kijiji cha mbali kidogo na Kijiji chetu ambako ndio ilikuwa kata yetu. Ili kufika mahali kata ilipo ulikuwa unavuka kijiji kimoja katikati ndio unafika, umbali sio chini ya masaa matatu kwa mwendo wa mguu. Hivyo vijana ambao tulitoka vijiji vya mbali tulilazimika kupanga vyumba hapo katani, ili kupunguza umbali wa kwenda shule. Vyumba hivyo vijana waliita "ghetto" sio kama la Mangwair lakini lenye kapeti manyoya, mashine ya dry cleaner na kistudio cha kiaina. La kwetu lilikuwa na godoro lisilo na kitanda, vyombo vichache kwenye beseni, kibatari na vimadaftari vya kiaina hakuna duu ambaye lingeweza kumchengua.

Ilipita miaka mingi nikiwa sijashuhudia tukio lolote la kishirikina, kiasi kwamba hadi kumbukumbu za tukio lile zikawa zimeshafutika. Mambo yalikuja kubadilika nilipokuwa sekondari. Nikiwa ndio niko likizo ya mwisho wa mwaka kuingia kidato cha tatu. Nakumbuka ilikuwa likizo ya mwisho wa mwaka kama sikosei ni either ilikuwa mwezi wa 12 mwaka 2011 au tarehe za mwanzo wa mwaka 2012. Kulikuwa na mechi ya Arsenal sikumbuki vizuri ilicheza na timu gani, lakini ilikuwa ni mechi ya ligi kuu. katika ile mechi Arsenal ilishinda 2-1 magoli ya Arsenal yalifungwa na Van- Persie kwa penalty na Benayoun dakika za mwishoni. Kipindi hicho kocha wa sasa wa Arsenal Michael Arteta bado anakipiga uwanjani. Sasa mimi huwa ni shabiki wa damu wa hii timu tokea enzi za mzee Wenger. Sasa kama unavyojua mazingira ya kijijini kulikuwa hakuna umeme hivyo mechi tulikuwa tunaenda kuangalia centre yaani yalipo maduka. Kuna jamaa alikuwa na banda la video anatumia generator linalopiga kelele kama mziki wa Young Lunya. Kulikuwa na umbali kidogo kutoka nyumbani hadi huko madukani umbali kama wa nusu saa kwa mwendo wa mguu. Sasa wakati naenda kucheki mechi nilikuwa na washikaji zangu watatu, sasa mechi ilivyoisha nataka nirudi nyumbani nikawa siwaoni. Na ilikuwa ni usiku kama saa sita hivi, kumbe jamaa walichoka kuangalia mpira wakaondoka kimya kimya Sasa ikabidi nirudi peke yangu, maana kitongoji chetu hakikuwa na watu wengi wapenzi wa mpira. Hivyo wengine waliokuwemo mle bandani sio wa maeneo ya kwetu.

Njia tuliyokuwa tunapita ina miti vichaka na nyumba za mbalimbali. Nikaanza kutembea peke yangu usiku ulikuwa kimya Kweli Kweli ni sauti ya upepo na wadudu tu ndiyo vilisikika. Kuna sehemu nikafika huwa hakuna nyumba kwa umbali kama wa mita mia mbili hivi ila kuna miti mingi sana na vichaka vichaka. Wakati natembea nikawa nasikia vishindo vya mtu kwa nyuma, kama yuko nyuma yangu umbali mdogo tu anakuja. Nikageuka kuangalia sikuona kitu, niliogopa kidogo lakini nikaendelea na safari nikidhani labda ni mawenge ya usiku tu. Nilipoanza kutembea nikaanza kusikia tena, safari hii kwa karibu zaidi kuliko mwanzo ni kama mtu alikuwa yuko mita chache sana nyuma yangu. Aiseee! Mapigo ya moyo yalienda kasi sijapata kuona!. Haraka haraka nikageuka tena kuangalia lakini sikuona kitu. Aisee nilitimua mbio zaidi ya Hussein Bolt! Nilikimbia kwa mwendo kama wa dakika tatu, nikashangaa kwa mbele yangu nikamuona mtu anatembea. Nikasimama ghafla kusoma kumuangalia nilikuwa naogopa sana nisingemuamini yeyote tena. Nilivyomuangalia, nikabaini alionekana kama mwanamke bibi mzee sana anatembea polepole kwa kujivuta kizee amevaa nguo zilizoonekana nyeusi tii. Niliweza kuona vizuri kwa sababu alikuwa mita chache sana! Akili iliniambia ndio walewale Kuona hivyo nilibadili njia kwa kasi na kuanza kukimbia huku nikipita kwenye mashamba nikikimbia hovyo. Kwa sababu nilikuwa mwenyeji haikunisumbua kukimbia nikikatiza kuelekea uelekeo wa nyumbani.

Nilikimbia bila kuchoka umbali mrefu sana, wakati nakaribia sasa kufika home. Nikaikamata sasa barabara inayonyoka kuelekea nyumbani. Nikawa kama nimechoka kukimbia nikawa natembea ila kwa kasi Sana ! Nilishtuliwa na sauti ya mwanamke wa makamo ikiniita!

"We mtoto" alisema yule mwanamke tena kwa kiswahili

Nilishtuka na kuanza kupepesa macho ili nione ile sauti ilitokea wapi. Nilipigwa na butwaa nilipomuona mwanamke amechuchumaa pembeni ya barabara amevaa nguo nyeusi amejifunika hadi usoni huku akiniangalia.

" We mtoto haunisikii"

Mr the Dragon nikakaa kimya. Wazee wetu walitufundisha ukisikia unaitwa usiku hata na mtu unayemfahamu usiitike ovyo. Wakati mwingine wachawi wanaweza kutumia uchawi wao kuigiza sauti hata ya mtu unayemfahamu na wakakuita. Ukiitika tu wanachukua sauti yako inakuwa rahisi wewe kulogwa. Kwa hiyo nilichagua kukaa kimya. Sikuweza kukimbia ni kama mwili ulikuwa umepigwa ganzi.

"Wewe mtoto kwa nini unatembea tembea usiku"

Mimi kimya!

"Usirudie tena kutembea usiku,potea hapa haraka"

Aisee hizo mbio nilizotoka nazo nadhani ingekuwa ni kwenye mashindano ya Olympic mita mia ningeweza kuibuka na gold medal. Nilikimbia hadi nyumbani nikamkuta brother wangu ninayemfata amelala. Nilimgongea mlango akafungua nikaingia ndani.

"Mbona unahema hivyo"

"Nimekuja peke yangu nilikuwa nimeogopa nikawa nakimbia" niliamua kuficha

"We nae muoga sana" alisema huku akipanda kitandani kulala.

Na mimi nilipanda kulala, usingizi ulikuwa wa mang'amung'amu sana, usiku mzima nilifikiria mambo yaliyotokea siku hiyo. Tukio la kusimamishwa na yule mwanamke ndio lilinitisha zaidi. Yule mwanamke alikuwa anatisha vibaya mno. Niliwaza Yule mwanamke atakuwa nani lakini sikupata jibu, nilijaribu kuikumbuka sauti yake na kuangalia kama nilishawahi kuisikia pale kijijini lakini niliambulia patupu. Kesho yake niliendelea na kazi kama kawaida, sikumwambia yeyote kuhusiana na tukio lile. Kuna muda mama yangu alihisi kulikuwa na shida na kuniuliza kama kulikuwa na shida lakini niliamua kuficha, sikumwambia chochote.

Baada ya siku kadhaa shule ilifunguliwa, sasa ukawa muda wa kurudi kwenye kile kijiji ambako shule ilipatikana yaani katani. Nilitembea nikiwa na washikaji na mabinti tuliokuwa tunasoma nao hadi tukafika. Getto kwetu tulikuwa tunaishi mimi na marafiki zangu wawili, jumla tukawa watatu. Hao wote nilisoma nao tokea shule ya msingi Mwanono. Usiku nikiwa nimelala niliota ndoto moja iliyonitisha kidogo.

Niliota mimi ni mtu mzima kidogo ambaye nilikuwa nimeshaondoka kijiji cha Mwanono nikaenda mjini kuishi huko. Nikaishi miaka mingi bila kurudi pale kijijini, sasa siku hiyo nikawa nikawa ndio nimerudi sasa kwa ajili ya kusalimia ndugu jamaa na marafiki. Kwenye ndoto niliota nimeshushwa na bodaboda pale madukani Mwanono nikapokelewa Kwa bashasha na marafiki zangu kitambo hapo kijijini ambao niliwakuta pale centre. Tukaanza kupiga story mbalimbali, miongoni mwa mazungumzo jamaa wakaanza kuniambia Mwanono Sasa hivi pamebadilika pamekuwa mjini, itabidi tukutembeze ujionee. Wakati tukiwa tunaendelea na mazungumzo hayo alikuja pale msichana mmoja niliyemfahamu vyema akiwa na baiskeli akasema

" Nyie mnataka mumtembeze lini, mimi naanza kumtembeza leoleo, hebu Mr the dragon panda hii baiskeli nikubebe nikutembeze" alisema yule msichana

Bila hiyana wala kipingamizi nikapanda baiskeli akanibeba, halafu huyo binti akawa anaendesha. Aliendesha baiskeli kwa dakika kadhaa ikafika sehemu kulikuwa na kona, tulipokunja ile kona tulitokea kwenye mazingira ambayo nilikuwa mgeni kabisa. Nilijaribu kukumbuka pale itakuwa ni sehemu gani kwenye kile kijiji lakini sikupatambua kabisa. Kulikuwa na nyumba nzuri za kisasa na mama mandhari ya kuvutia Sana. Msichana yule aliendesha baiskeli hadi kwenye nyumba moja nzuri sana, kisha akaniambia ingia ndani. ile naingia ndani nikakuta kundi kubwa la watu

Ghafla nikashtuka kutoka usingizini. Niliposhtuka tu nilihisi maumivu mgongoni. Nikajishika nikawa nahisi maumivu ya kuchanwa chanwa mgongoni na kitu chenye ncha kali. Ilibidi niamke nikawasha kibatari kuangalia mgongoni

LAHAULAH!!! nilikuwa na Chale mgongo mzima zikiwa mbichi kabisa na damu kana kwamba ndio nimetoka kuchanjwa na nimepakwa dawa nyeusi na nyekundu. Wazo la kwanza lilikuwa kwenye ile ndoto niliyotoka kuota

Hasahasa msichana aliyenibeba kwenye baiskeli kwenye ile ndoto, ndio yule yule aliniambia mimi ni muoga wakati nilipoona wachawi nikiwa darasa la tatu miaka kama saba iliyopita.

Ndio yule aliyeniambia usiku ule nakimbia wachawi kurudi ndani, wao walienda kula nyama kwenye mkwaju wa kwa mzee Lugota. Yule Yule ambaye tulisoma nae darasa moja na sasa tunasoma darasa moja sekondari. Yule ambaye bibi yake ni mchawi anayeogopeka Kijiji kizima.

Itaendelea tena kesho majira na nyakati kama hizi

Usiku mwema.
Nimesabuskraibuuuuuu
 
Nimeamua kushare hapa hiki kisa cha kweli kilichonitokea kwenye maisha yangu. Nikiamini wengi mtajifunza na kuburudika pia.

NB: Majina ya watu na baadhi ya Majina ya sehemu yatakuwa sio halisi ili kuficha indetity yangu. Pia sio mwandishi mzuri Ila nitajitahidi kuandika kwa mtiririko mzuri.

Naitwa Mr the dragon ni mzaliwa wa wilaya ya Bunda mkoa wa Mara. Nilizaliwa katika hospitali ya Bunda district designated hospital (DDH) katikati ya miaka ya tisini, yaani miezi sita kabla ya kifo cha 2pac na miezi miwili kabla ya kuzama kwa Mv Bukoba. Ukiwa pale ilipo Crdb bank kwa sasa ndio maeneo niliyozaliwa.

Nikiwa ndio kwanza nina umri wa miaka mitano. Baba yangu mzazi aliugua kichaa, namaanisha alianza kupata uwendawazimu ikabidi apelekwe kwa waganga wa kienyeji. Baba yangu alikuwa ni mfanyabiashara aliyejulikana vizuri mitaa hiyo. Japo baadae alikuja kupona, lakini mpaka sasa imebaki ni kitendawili juu ya chanzo cha ugonjwa ule wa akili. Inasemekana ni mkakati maalumu ulioandaliwa na baadhi ya wafanyabiashara wenzake ukitaka wafanyabiashara wote waliovuka rubana warudi kwao. Mkakati huu ulihusisha imani za kishirikina, wafanyabiashara baadhi waliovuka mto rubana kuja bunda walipoteza maisha. INASEMEKANA LAKINI!!!

Mhenga aliyesema mwanaume ni kichwa cha familia hakukosea. Baada ya baba kuugua mambo yote yaliharibika maisha yalituchapa kwelikweli. Ikabidi mama achukue familia kurudisha nyumbani kwao, yaani kwa Babu yetu mzaa mama. Nyumbani kwao na mama ni mkoa wa Simiyu wilaya ya Busega kijiji cha Mwanono (Sio jina halisi). Mimi na kaka zangu na dada zangu tukaanza kuishi kwa Babu, kipindi hicho nina miaka minane nikiwa darasa la pili.

Babu yangu aliitwa mzee Manumbu alikuwa very prominent pale kijijini. Kijana wake wa kiume yaani mjomba wetu (kaka mama mmoja na mama yangu) alikuwa na cheo kikubwa serikalini. Alimjengea babu nyumba nzuri kijiji kizima, alimnunulia ng'ombe wengi na trekta jambo lililomfanya kuwa miongoni mwa matajiri wa kile Kijiji. Babu yangu alikuwa na wake sita walioishi sehemu moja, jambo lililofanya awe na familia kubwa sana. Watoto wake na wajukuu tulikuwa wengi sana tulioishi pale.Mabinti wa Kijiji kile na vijiji jirani walitamani kuolewa kwa mzee Manumbu.

Nakumbuka mwaka uliofuata 2005 nikiwa darasa la tatu siku moja mama yangu alialika kikundi cha watu wa kulima. Kwa jina maarufu kwa kisukuma huitwa "Luganda". Alialika hicho kikundi wakamlimie palizi ya pamba. Kikundi hiki kilitumia zeze na ngoma pindi wakiwa wanalima ili kupandisha mzuka watu wasichoke wakiwa wanalima. Muda wa usiku nikiwa nimelala nilisikia sauti ya ngoma na vifijo nje ya nyumba. Nilifikiri ni wale wa kikundi wamekuja kuwapitia watu wa nyumbani waende shamba. Nilikurupuka kutoka nje ili nikawaone wanavyocheza.

Nilifungua mlango nikiwa na shauku kubwa. Nilipofungua niliona kundi kubwa la wanawake na wanaume wanaimba na kucheza katikati ya uwanja wa pale nyumbani wengine wakiwa uchi, wengine wamevaa nguo nyeusi. Kwanza nilipigwa na butwaa na kujikuta nikikaza jicho langu kuangalia wanavyocheza. Baadae ndipo wazo la kwamba wale ni wachawi ndio lilikuja akilini, nikatimua mbio kurudi ndani nikajifunika shuka gubigubi. Cha ajabu niliporudi ndani tu zile ngoma zilikoma, niliogopa sana japo sikufanikiwa kumtambua yeyote katika kundi lile.

Kesho niliamka mapema ili niwahi kuhesabu namba shuleni, lakini nilisikia maumivu kwa mbali kwenye mguu. Kuangalia nikaona nilikuwa na kidonda mguuni japo sio kikubwa Sana. Nilijiuliza nimepata wapi hicho kidonda lakini sikupata jibu. Nikikumbuka hata jana yake usiku sikujigonga wala kujikwaa popote wakati nakimbia. Niliogopa sana lakini sikuwa na jinsi niliendelea na kunawa miguu na uso niende shule. Wakati tukiwa tunatoka kwenda shule mimi na ndugu wengine tulisikia taarifa mbaya. Mjomba wetu (kaka wa mama tofauti na mama yangu) aliyekuwa anakaa pale nyumbani alikuwa amechanjwa Chale mgongo mzima. Niliogopa sana nikawa natamani kusimulia nilichokiona usiku, ila kila nikijaribu napata uoga sana... Sikuzungumza chochote

Baadae tulienda shule, siku hiyo sikuwa na raha kabisa ukizingatia matukio yaliyotokea nyumbani. Kikubwa zaidi kilichoniogopesha ni hiki kidonda ambacho sikujua kimetokea wapi. Wakati nikiwa darasani binti mmoja tuliyekuwa tunasoma nae darasa moja alinifata, binti huyu bibi yake alikuwa ni mchawi aliyeogopeka zaidi pale kijijini. Ujio wake haukunishangaza kwa sababu nilimchukulia kama ndugu yangu, na mara nyingi tulikuwa tunapiga story. Nilimchukulia kama ndugu kwa sababu kaka wa huyo bibi yake alikuwa ni rafiki mkubwa wa baba yangu mzazi. Hata bibi yake yaani mchawi aliyeogopeka nilikuwa nikimuita shangazi. Alipofika aliniambia

" Mr the dragon kumbe ni muoga vile, nilikuona usiku ulivyokimbia kurudi ndani. Sisi tulienda kwenye mkwaju wa kwa lugota kula nyama"

Mkwaju wa kwa Lugota ulikuwa ni mti wa ukwaju mkubwa na mnene sana uliokuwepo pale kijijini.

Nilimuangalia tu nikakaa kimya, sikuzipendelea story zake kwa sababu nilikuwa naogopa sana.

Itaendea kesho...
[emoji144]
 
Tunaendelea sehemu ya nne!

Baada ya kugundua nilikuwa nimepakwa dawa, ambazo zilikuwa za unga unga za rangi nyeusi na nyekundu. Wazo la kwanza nilifikiria kuoga kuziondoa zile dawa, Lakini kwa sababu bafu lilikuwa ni la nje niliogopa kutoka nje, ningepata wapi ujasiri kwa mazingaombwe ambayo nimekuwa nikiyashuhudia. Nikapata wazo nijifute tu na kitambaa, nikachukua kitambaa nikakilowesha maji nikaanza kujifuta mle mle chumbani. Baada ya pale nikaona sikuwa na jambo lingine la kufanya zaidi ya kusali kuomba msaada wa Mwenyezi Mungu, yeye ndio kimbilio la wanyonge. Nilipiga magoti nikasali, nikamaliza nikazima kibatari nikarudi kitandani kulala. Usiku ule sikupata usingizi kabisa, ulikuwa ni usiku wenye mchanganyiko wa hisia za hasira, uoga na fadhaa. Wazo ambalo liliisumbua akili yangu niliamini kabisa ile ndoto ina uhusiano na hili tukio. Nilikumbuka kanisani tulifundishwa Mungu wakati mwingine huwapa ujumbe watu wake kupitia ndoto. Ndivyo alivyofanya kwa Yusufu, Daniel na baba wa imani Ibrahim. Niliamini ile ndoto itakuwa na uhusiano wa moja kwa moja na tukio lile. Nilipata mawazo matatu juu ya nini nifanye

Wazo la kwanza nilifikiri kesho yake asubuhi nirudi nyumbani nikawaambie wazaz wangu juu ya tukio lile lililotokea.

Wazo la pili nilifikiri niongeze bidii ya kusali halafu nisubiri hadi weekend nikirudi nyumbani, niwaambie baba na mama.

Wazo la tatu nilifikiri nimtafute msichana yule niliyemuota amenibeba kwenye baiskeli (tumpe sasa jina la Vumilia). Niliamini huyu kuna kitu atakuwa anakijua.

Nilichakata mawazo yote nikaona niende na wazo la kusubiri hadi weekend ndio niende nyumbani huku nikiongeza maombi. Mama yangu ni msabato kupita maelezo, na nimelelewa katika maadili ya kuishika imani hivyo niliamini Mungu atatenda. Kwa ufupi nitumie hii fursa kuwakumbusha hata wazazi mnaosoma hiki kisa, muwalee watoto wenu katika njia ipasayo nao hawataiacha hata watakapokuwa wazee, Mithali 22:6 . Sio mnafanya umalaya, kuvaa vinguo vifupi na kupost picha mkivuta shisha mbele ya macho ya watoto wenu. Mkijidanganya ndio usomi na usasa, kumbe ni ushamba na kukosa elimu. Siku hiyo pia nilikumbuka fungu la Hesabu 23:23 hapana uchawi juu ya Yakobo wala, wala uganga juu ya Israeli. Niliamini Mungu atatenda!

Anyway sipo hapa kwa ajili ya mahubiri! Tuendelee na kisa chetu!

Wazo la kwanza nililikataa kwa sababu niliona kuharakisha kuwaambia lingewapanikisha wazazi wangu, na sikupenda hali hiyo. Nilimpenda sana mama na baba yangu hivyo nisingependa kuwaona wamefadhaika kwa sababu yangu.

Wazo la kumuuliza Vumilia niliona ni gumu kwa sababu ningemuulizaje mambo mazito kama yale kwa kigezo kipi na uthibitisho gani. Ingekuwa ni sawa nakusema namtuhumu yeye ni mchawi! Nisingeweza kufanya hivyo!

Nilipiga chini hilo wazo!

Asubuhi kulipopambazuka nilioga na kujiandaa kwenda shule kama kawaida. Sikumwambia yeyote juu ya kilichotokea na nilijitahidi sana kuficha zile chale zisije zikagundulika. Tulitoka ndani wote watatu na kuanza kutembea mdogo mdogo kuelekea shule. Tulikuwa tunatembea umbali wa kama nusu saa hadi kufika shule. Tulifika shule na kuendelea na ratiba zingine kama kawaida, japo kimawazo nilikuwa mbali sana. Zaidi zaidi nilikuwa napata hisia za uoga sana. Darasani vumilia alikuwemo nilitamani niamke kwenda kumuuliza, lakini nilikosa courage ya kuamua. Muda sio mrefu iligongwa kengele ya mpumziko mida ya saa nne. Wanafunzi wakatoka nje kupumzika, wenye pesa walienda canteen kunywa chai na maandazi.

Japo baba alikuwa ananipa pesa ya kunywa chai kila siku. Lakini siku hiyo sikuwa na mzuka hata wa kuinywa chai yenyewe. Nilitoka nikajitenga nikaenda kupanda kwenye jiwe moja refu, linalopatikana pale shule nikakaa angalau kupata vitamin D. Wakati nikiwa nimekaa pale ghafla nilimuona Vumilia akija na sahani yenye maandazi kwenye sahani mkono mmoja, mkono mwingine amebeba vikombe viwili vya Chai. Nilitamani nimkwepe lakini nikasema hapana ngoja nione atakuwa na jipya gani, nikajiapiza sitakunywa chai yake. Vumilia kiukweli alikuwa ni msichana aliyekuwa anavutia kwa kiasi chake, si haba. Ni msichana ambaye nisingekuwa kumuogopa bibi yake na undugu wa uongo na kweli uliopo kati yetu basi ningetamani kuwa naye. Alifika pale akaniambia nishuke chini nimpokee, mtoto wa watu sikuwa na hiyana nilishuka na kutii amri bila kuuliza kama niko jeshini. Alinikabidhi kikombe kimoja akaniambia "karibu chai"

"Asante leo sijisikii kula kabisa" nilijibu
"Hujisikii kwani umekula wapi, au unaogopa nitakuwekea dawa unipende"

Nilijichekesha kwa lengo la kupotezea!

Baada ya kukataa hakunibembeleza tena, alianza kunywa chai huku nikimkodolea macho hadi akamaliza. Alipomaliza aliniangalia kwa macho ya huruma kidogo kisha akasema

"Kuna kitu nataka nikwambie"
"Kitu gani" nilijibu haraka kwa pupa
"Mbona una haraka hivyo, uko sawa Kweli"
"Niko sawa we niambie tu"

Alikaa kimya kidogo baadae akaanza kuimba wimbo fulani kwa sauti ya chini, dizaini kama ananichora hivi

Aisee! Alivyoimba palepale kuna kitu nilikumbuka!

Huo wimbo ndio wimbo ambao wale wachawi walikuwa wanauimba siku ile nilipotoka ndani usiku. Kipindi nikiwa darasa la tatu 2005.

Daktari Ben Carson katika kitabu chake cha Think Big aliwahi kusema ubongo wa binadamu una seli zaidi ya bilioni moja. Seli hizi ni nyingi sana kiasi kwamba zinaupa ubongo uwezo mkubwa wa kutunza kumbukumbu nyingi kwenye maisha. Kuna jambo linaweza kuwa lilitokea miaka mingi pengine ukiwa bado mtoto ukadhani umeshalisahau, lakini siku ikitokea "stimuli" fulani kuhusiana na lile tukio, utakumbuka kila kitu kama unaangalia runinga. Maneno hayo ya huyo daktari yalithibitika kwangu siku hiyo!

Nilikumbuka haswa ule wimbo niliusikia ukiimbwa siku ile. Kumbukumbu zangu zilinichukua hadi usiku ule nikiwaona wanawake kwa wanaume wakiwa wameshika myoto na wamevaa nguo nyeusi wakiimba na kunengua.Baada ya kumbukumbu hiyo kwa Vumilia Sikutaka kuuliza chochote kwa sababu yeye mwenyewe Vumilia aliwahi kuniambia alikuwepo siku ya tukio. Alivyoona sijaongea chochote aliniuliza

" Jana usiku ulikuwa wapi?"
Nilichanganyikiwa kidogo na lile swali, wakati mwingine nilijiona geneous kwa kudhani toka mwanzo ni lazima kuna kitu Vumilia atakuwa anafahamu.

" Nilikuwa getto tu kwani kuna nini" nilijifanya sielewi
"Sema ukweli mr the dragon jana hujachanjwa chale wewe Kweli?"

Nilishtushwa na taarifa ile ni kama nilikuwa siamini kama Vumilia kweli anajua kuhusiana na tukio lile.

"Hamna" nilikanusha

"Mmmh! Labda lakini kama unanidanganya na tayari umeshachanjwa chale, jua unajidanganya mwenyewe" alikaa kimya kidogo kisha akaendelea

" Ndio unajidanganya mwenyewe! Maana kama umeshachanjwa chale tayari wewe ni nusu mfu nusu hai! Usipoharakisha kutafuta tiba utaitwa marehemu na mimi nipo hapa kwa ajili ya kukusaidia"

"Nimechanjwa" nilikurupuka kujibu pasipo kujiuliza kama ni jambo sahihi au sio sahihi kujibu vile. Uoga ulikuwa umenitawala isivyo kawaida

"Sasa na ulivyokuwa unanificha,ulitegemea nini"

"Naomba unisaidie unajua ni kama nimechanganyikiwa tokea nilivyogundua hilo usiku wa jana nimechanjwa"

Nilivyomwambia hivyo alivuta pumzi ndefu kama mtu aliyekuwa ananionea huruma.

"Kuna kitu nataka nikwambie ila usiogope, unahitaji kuwa jasiri" alikaa kimya kisha akaendelea!

"Kama umeshachanjwa chale mpaka hapo maisha yako, yako mikononi mwa wachawi waliokuchanja, Wewe unaonekana mizimu ya ukoo wa kwenu ina nguvu sana lakini pia umezaliwa na nguvu fulani za asili"

"Kwa nini"

"Unajua wachawi kabla hawajamloga mtu ni lazima waijue kwanza nguvu yake inayomlinda hasa kimizimu. Maana ili mchawi akuloge kwanza kabisa huwa kuna makubaliano baina yake na mizimu yako yaani ya upande wa baba yako pamoja na mama yako, makubaliano yakishindikana haulogeki kamwe, labda atakutesa tu ila hawezi kukuua. Ukionekana mizimu ya kwenu ni mikali na makubalino hayawezi kuwepo ni lazima kuna tambiko lifanyike likihusisha kafara ya kondoo mweusi ili kuua nguvu zako. Sasa kilichofanyika jana wachawi wamekuja kukuchukua usiku wakakupeleka hadi kwenye makaburi ya ukoo wenu upande wa baba yako. Wakafanya tambiko lao, ambalo ndio lilihusisha wewe kuchanjwa chale. Baada ya kumaliza ndio wakakurudisha. Na tambiko hilo likishafanyika unakuwa hauna nguvu tena inayokulinda kimizimu hivyo mchawi kukuloga ni kazi nyepesi zaidi ya kusukuma mlevi. Hivyo nguvu zote zilizokuwa zinakulinda wewe zimeshaondolewa na sio muda mrefu wataanza kukushughulikia na nina uhakika usipofanya jitihada kutatua hiyo shida wiki moja humalizi"

Mpaka hapo nilikuwa nimechanganyikiwa kijasho chembamba kilikuwa kinanitoka. Swali ambalo nilijiuliza ni kwa nini wanataka kuniua, nimewakosea nini na wamejuaje yalipo makaburi ya ukoo wa baba yangu ilhali ni kijiji kingine kabisa japo ni jirani.

"Kwa nini sasa wanataka kuniua nimewakosea nini"

"Hata mimi sijajua bado lakini huwezi amini wanaotaka kukufanyia hivyo ni ndugu zako kabisa"

"Heeeeh! Wakina nani hao?"

"Utawajua tu tena utajionea kwa macho yako mwenyewe"

Nilimuuliza tena

"Wamejuaje yalipo makaburi ya ukoo wetu"

"Wachawi ni shirika kubwa lenye ushirikiano mkubwa, hakuna ukoo usio na wachawi. Na huwa wanasaidiana kutimiza mambo yao" alinijibu

"Sasa naomba unisaidie" niliomba kwa unyenyekevu

"Nitakusaidia ila mpaka ukubali sharti langu"

"Sharti gani"

"Uwe mpenzi wangu kuanzia leo na ukubali kuja kunioa"

Ulikuwa ni uamuzi mgumu kuufanya lakini kwa sababu niliogopa sana. Niliamua kukubali bila kufikiria mara mbili. Niliona ngoja kwanza nipambane na kifo baadae ndio nipambane na mapenzi.

"Asante kwa kukubali, Mr the dragon nimefanya hivi kwa vile nakupenda tu, nakupenda tokea tukiwa wadogo. Na ujue mimi ni miongoni mwa watu wachache ambao wanaweza kukuonyesha njia ya kukusaidia. Nasema hivyo kwa sababu mimi naijua siri iliyoko kwenye mwili wako ambayo bila hiyo siri kuifumbua hakuna mtu anaweza kukusaidia"

"Siri gani"

"Kuhusu hiyo siri nitakwambia muda mwingine, tupambanie maisha yako kwanza, usiku nitakuja kukuchukua twende sehemu ila unahitaji uwe jasiri. Tukishamaliza hili suala sitegemei utaniacha" alisema Vumilia

Baada ya mazungumza hayo tulielekea darasani sikuamini kama nilikuwa katikati ya bonde la kifo na uzima. Ni kama nilikuwa nimechanganyikiwa nikimkumbuka mama yangu, baba yangu, kaka, dada na marafiki zangu halafu lisipofanyika jambo ndani ya wiki moja nitakuwa nimewaacha wote. Sikupata hata mood ya kuendelea kukaa darasani nilichukua begi langu nikatorokea porini na kuanza kutembea mdogo mdogo kuelekea getto. Njiani machozi yalinibubujika mashavuni. Wakati mwingine niliiangalia ardhi na kutabasamu mwenyewe yaani mimi huyu mr the Dragon kijana barobaro wa shule ndani ya wiki hii nitakuwa nimefukiwa na hii ardhi ninayoikanyaga. Ama kweli dunia ni uwanja wa fujo kila mtu atafanya fujo zake na kuondoka!

Lakini pia niliyawaza maneno aliyoniambia Vumilia kwamba kuna ndugu zangu ndio wanataka kuniua, nilijiuliza ndugu gani huyo lakini sikupata jibu. Nilijiapiza sitomsamehe kamwe kama nitapona.

Itaendelea baadae kidogo ngoja nipate lunch!
 
Back
Top Bottom