Kisa cha mtoto wa shehe na paka; Bulembo, Mama Lwakatare na Zitto; Mdomo huumba na mdomo uliponza kichwa

Kisa cha mtoto wa shehe na paka; Bulembo, Mama Lwakatare na Zitto; Mdomo huumba na mdomo uliponza kichwa

Superbug

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2018
Posts
13,864
Reaction score
35,079
Wakati tunasoma shule alikuwepo mtoto mmoja baba yake alikuwa Shehe.

Mtoto yule Kuna siku aligombana na sisi wanafunzi wenzake wote bwenini.

Kwa bahati mbaya Sana alitutishia kwamba baba yake ni Shehe na anafuga majini hivyo usiku atakuja kwa njia ya paka akiwa Kama jini.

Basi sisi tulilala kwa kujihami sana tukijua leo kazi ipo.

Kwabahati mbaya sana usiku ule akaja paka bwenini na kama mjuavyo shule nyingi za bording mapaka ni mengi kwa sababu kuna misosi ya bwerere.

Hakika tulitaka kumuua yule mtoto wa Shehe pona yake ilikuwa ni walinzi waliwahi kuja bwenini vinginevyo angekufa siku hiyo na maafa yangekuwa makubwa.

Maskini ya Mungu mtoto wawatu Wala familia yao haina Mambo yoyote ya kishirikina na baba yake ni Shehe kweli ila mwislam Safi mzee yule rafiki yake na mzee Benjamin William Mkapa.

Mdomo ulitaka kumponza mtoto yule kwa kututishia kwamba atakuja usiku bwenini kama jini kwa sura ya paka ili tukione cha mtema kuni.

Sasa kitendo cha mzee Bulembo Mama Rwakatare Ndugai na wabunge wa CCM kutaka Zitto auwawe ni kucheza na Moto kama ule wa mtoto wa Shehe.

Mdomo huumba muombeeni sana Zitto abaki kuwa salama vinginevyo mnaweza kuta jumba bovu linawaangukia nyie in case ZITTO akidhurika. (Kuna Mambo yanatokea coincidentally) mfano unamtishia mtu ajali kwa utani na kweli anapata ajali ujue Hilo linakuhusu huchomoki lakini pia Kuna maadui wanaweza kutembelea kauli zenu kweli watamdhuru victim ili tu jumba bovu liwaangukie kumbe maskini mliongea kimuhemko.

Jitafakarini sana hasa Mama Rwakatare mchungaji.
 
Nikiwa shule nakumbuka kuna rafiki yangu alikuwa anapenda sana utani.

Siku moja tunarudi kutoka shuleni huku tunafuata reli basi akaja kwa nyuma akanipiga mtama nikaangukia kwwnye mawe ya kwenye reli nikaokota jiwe nimpige nalo akawa amekimbia.

Bibi yake alikuwa mwalimu wetu alikuwa anaumwa amelaźwa hospitali. Nilitamka kwa hasira kuwa bibi yako atakufa Leo. Kesho yake asubuhi tunaenda shule nimeshasahau tunafika shuleni wanafunzi wenzangu wameniambia mwalimu amefariki kama ulivyomwambia mwenzako Jana

Niliumia sana kupita maelezo. Tangia pale nilijifunza sana kulopoka sio kitu kizuri
 
Inasikitisha kwa umri wa Bulembo kuongea maneno yale..

Inasikitisha zaidi kwa mama rwakatare kwa anavojifanya mfia dini kushangilia kauli ile..
Maskini mama wa watu..!! Huenda hata hakujua anashangilia nini maana ni kawaida yao kushangilia na kupiga meza kada mwenzao akiongea haijalishi ni cha maana au pumba

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bunge letu limekuwa kituko sana,

Mbaya zaidi wanaojinasibu kuilinda Amani ya nchi, CCM ndiyo wao wanachochea Mh,Zitto auwawe tena wanashangilia mbele ya Spika na hakuna hatua zilizochukuliwa mpaka sasa dhidi Bulembo.
 
Umenikumbusha ishu ya kiongozi mmoja wa CHADEMA, watu wa 'kampuni" walichochea ugomvi kati yake na viongozi wenzake, ugomvi ulipofika kileleni wakamshughulikia kisha wakatengeza "movie" kuwahusisha wale wagomvi wake na kifo chake ila Mungu aliwaaibisha movie ikabuma japo hawajaacha kuifanyia rejea mara kwa mara.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duniani tunapita tu ila hawa viongozi wanaona Mungu ni baba yao na wao ndo wenye haki hapa duniani cha msingi tuwalee watoto wetu ili waje waliendeleze hili taifa ktk misingi bora.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom