Kisa cha Prof. Khigoma Malima na Sheikh Mavumbi, Uchaguzi wa 1995

Ok kumbe wewe ndio mkewe
Bujibuji,
Hapana haja ya lugha kali tufanyeni mjadala wa kiungwana.

Hivyo ndivyo ilivyokuwa.

Alishukuru kisha akafariki na siku ya mazishi yake hapakuwa na msikiti wowote uliokuwa na nafasi ya kumsalia sala ya jeneza ikaamuliwa jeneza lake likasaliwe Viwanja Vya Mnazi Mmoja.

Hii ilikuwa haijapata kutokea.

Baada ya sala mwanae Adam Malima alipanda jukwaani na akaeleza jinsi baba yake alivyofariki.

Maziko ya Prof. Malima hayajapata kutokea hadi hii leo.
 
bujibuji kama una chuk na mtu sema ila usimsem mayti vibaya.watu wengin kama wa kheri shaur yako utaj kufa kifo kibaya weweulimi ufike mpaka magoti.nini chuki yako kwa almarhum.?
 
Mzee MS
Hadithi yako haijakaa Vizuri hata kidogo
Naamini uliandika ukiwana haraka
Tafadhali fanya hima uhariri kazi yako
Uzalendo,
Hapana huwa sina haraka katika kuandika na sababu ni kuwa mengi yamo katika Maktaba yangu hivyo huwa suala la kutalii napata ninachotafuta.

Juu ya haya kazi yoyote ya mikono ya binadamu lazima itakuwa na kasoro.

Kama umeliona kosa nifahamishe nisahihishe kwani siwezi kujihariri mwenyewe.
 
Kisa nakikumbuka na nilikuwepo nilikua bado mvulana wa makamo ya elimu ya juu ya sekondari katika shule ya Uyui

Bahati mbaya Mavumbi ulimtaja alikwisha fariki aliyepo sasa ni mwanae

Ni kweli Mzee Bilali waikela aliongea na moja ya kauli aliyoitoa ambayo ilikaririwa katika ndimi za waislamu waliokua wapinzani wakubwa wa BAKWATA

Ni pale aliposema :

" ... sio tu kuchanganya dini na siasa bali tutaikoroga dini na siasa ..."

Nakumbuka ulikua mzozo mkubwa sana wakati huo, miongoni mwa watu maaru ninao wakumbuka kwa upande wa polisi operation hiyo ilikua chini OC CID Ndg. Chaka na rafikie mkubwa Kamanda Mohamed Chiko

Tabora iliwaka moto, na chama alichokua ikihamia Mareham Kighoma Malima kilikuwa kinaitwa NRA au NAREA nimesahau kirefu chake, wakati huo chama hicho pamoja na CUF vilihusishwa sana na udini

Ahsante kwa history hiyo!!!
 
Jina maarufu sana hili! Lakini kama ni Imamu inakuwaje anatajwatajwa kama mganga? Ni maarufu kwa hili la ulozi pia!
Alikuwa Mganga wa kiislam. Huo uganga wake aliokuwa akiufanya kwa kweli hakufaa kuwa na Kiongozi wa kidini. Alikuwa kama mchawi fulani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…