Kisa hiki kimemkuta rafiki yangu. Kuna watu hapa duniani wanapitia maisha magumu kwenye ndoa kwa kawaida huwezi kuamini

Ni aina Fulani ya mwanamke mpumbavu kupindukia.
Mwanamke ambae amejaliwa utashi mwema hawezi kumfanyia hivyo mumewe hata siku moja, Lau akifanya Jambo Kama Hilo kwa mwanamke mwenye na akili huwa anapeleka maendeleo, hapo huyo ndugu wangekua na nyumba kadhaa.

Lakini mwanamke was namna hio huwa mwishowe hutafuta njama za kumuua mumewe na kuolewa na mwanamme mwingine.


Mleta mada kwa vile huyo ndugu amepata bahati ya kukushirikisha hayo anayopitia huwenda wewe ndie msaada pekee kwake.

Kule kuletwa kwenye hio ofisi Ni mipangilio tu ya muumba kumokoa huyo ndugu, Mungu huwa anatumia watu kuwasaidia watu wanaopitia maagumu,

Hivyo wewe Ni Kama mjumbe wa Mungu alietumwa kumuokoa just do any thing sir.
 
Nitajitahidi kwa uwezo wangu wote, pia nitafanya namna ili nimjue tu huyo mke wake maana nilionywesha kwa picha
 
Hizo ni imani sio sayansi, siku kizi vijana wananyonya kabisa, hata kumi
 
Nadhani hapa hatuongelei bank,.nimkuuliza je unadhani kwamba uchawi unaweza kusababisha mtu akawa katika hali kama hiyo.
Hapana siamini ila najua kwa kutumia sayansi unaweza kumfanya mtu awe hivyo
 
Ngoja niongee na ndugu zake kwanza maana mimi siwezi kwenda kwa mganga wa kienyeji ila nitajitahidi kabla sijaondoka hapa kwenda sehemu yangu ya kazi lazima niwe nimempeleka kwenye maombi, hilo ndo ninalo weza pekee
Uwezekano hapo mdogo sana.
 
Ndo maana mimi sitaoa Forever ushenzi gani huu tunafanyiwa na Madem.
Msela ndiyo kaolewa, ndiyo maana unaona anapangiwa mashariti na yeye anaogopa!! Hivi kweli Wanaume hawa wapo kweli au story za kunogesha Baraza!?
 
Ndio maana wife hajui kiwango cha mshahara ninaopokea. Alipojaribu kuuliza nilimjibu 'dry' hakunigusa tena!

Mpe pole mshikaji. Hata hapa job Kuna jamaa wawili ATM card zao wamekabidhi kwa wake zao. Mmoja bosi aliumwa vidonda vya tumbo na alikuwa anatoka kazini saa tatu usiku,wikendi pia kutwa yupo ofisini. Mmoja mlokole anaishi maisha magumu mno kama sio mtumishi
 
ila watu huwa wanalishwa uchafu
 
Ushauri wangu Ni huu
1. Oa rafiki yako
2. Oa kutoka the same background
3. Oa mtu wa kwenu
4. Mkeo asikuzidi kipato
5. Epuka kuoa makabila usiyojua Mila na desturi zao. Wachaga wananielewa kwa hili
Wachaga wenyewe mbona siku hizi wametulizwa,wanakupikia hadi Ugali Dagaa Mzaramo anasubiri, Wanaume hawa watu tuishi nao kwa akili tuta enjoy sana!!
 
Hapana siamini ila najua kwa kutumia sayansi unaweza kumfanya mtu awe hivyo
Samahani mkuu nisaidie katika hili limewahi kunitokea mimi mwenyewe iko hivi;... Siku moja nilitoka kazini nikafika ndani nikapika, nikala nikacheki taarifa ya habari then nikazima TV, nikaingia chumbani nikalala by saa nane hivi nikastuka baada ya kusikia TV imewashwa niliamka ile nakaribia sebuleni nikaona paka sikujua idadi yao kwa haraka lakn walikuwa kama 15 hivi nikajiuliza hawa paka wameingiaje ndani na madirisha yana nyavu,... basi nikaamua kuwatisha lkn hata hawastuki, ... basi nikarudi chumbani kufika tu chumbani walianza kulia kwa sauti kubwa sana kama dakika tano hivi,... baada ya hapo kukawa kimya na ile TV Ikawa imezimwa. nilipoenda kuangalia tena sikuwakuata je kisayansi hii inaweza kuwa imesababishwa na nini kumbuka hapo nilikuwa naishi peke yangu na baada ya pale sikulala tena hadi kunakucha,... isipokuwa asubuhi jamaa wa chumba cha jirani alizungumzia kuhusu zile kelele za paka kwa usiku ule pls naomba unisaidie hili lilisababishwa na nini.
 
Ni zaidi ya ukatiliii kwa huyu mwanaumee,atakua tu amemfanyia madawa sasa ni jukumu lako kumsaidia rafikiyako atoke kwenye iko kifungoooo usiishie kuhudhunika na kusikitikaaa
 
Yes yapo,mm pia zamani kdg nyumba tulipanga na Mr kulikua na mbaba mjeshi kapanga na mwanamke mtu wa singidaa mama yule alikua anachukua mshahara wote wa yule baba anampa nauli tuuu
Pale nyumban ndugu wa mke tu ndio waliokua wanakujaa,,mjeshi alikua km zezeta,,na waziwazi yule mama alikua anatufundisha na sie twende mahala atupeleke tuwatengeneze waume zetuuu,haya mambo yapo ila mwisho wake sio mzuriii
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…