Kisa kilichonitokea kutibiwa na mwanafunzi wa udaktari, Siwezi kuja kukubali tena kuwa mwili wa kujifunzia matibabu kwa wanafunzi wa field

Kisa kilichonitokea kutibiwa na mwanafunzi wa udaktari, Siwezi kuja kukubali tena kuwa mwili wa kujifunzia matibabu kwa wanafunzi wa field

G Tank

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
2,297
Reaction score
8,760
Kuna kipindi nilikuwa ninahisi maumivu kwenye jino la mwisho, nikaenda hospitalini kupiga xray ikaonekana nina jino chini ya fizi, inabidi litolewe.

Nikaweka appointment ili niende kesho yake kulitoa.

Asubuhi na mapema nikawahi hospitalini, Daktari nilekutana nae ni kijana mdogo mwenye rika la 24 hadi 25 na nilijua ni mwanafunzi, mwalimu wake ambae ni daktari tulieonana jana yake alikuwa anampa maelekezo fanya hii fanya vile.

Kosa la kwanza kabisa alilokosea ni kuweka kiwango kidogo cha dawa ya ganzi, kwakweli nilikuwa napata maumivu makali sana, ilibidi mwalimu wake aweke tena.

Zoezi likafika la kung'oa jino anavuta vuta bila mpangilio ikabidi mwalimu wake aje kutoa jino lakini mpaka leo jino linalofuatia ni kama limechimbika, nikitafuna kitu kigumu kama mfupa ukifikia hapo huwa kuna maumivu, nyama huwa najitahidi kutafuna isifike huko.

Shughuli ilivyokamilika mwalimu wake akamwambia aniandikiea dawa za kutuliza maumivu bila kumuelekeza labda alimuamini ataweza bila kusimamiwa, nilienda kununua dawa hizo lakini hazikuwa za kutuliza maumivu.

Nililia chumbani na utu uzima wangu kwa maumivu niliyokuwa napata, niliongeza dozi lakini wapi

Maumivu yalikuwa makali uvumilivu ulinishinda, Nikaenda duka la dawa kuulizia kama dawa nazotumia ni za maumivu, wakaniambia ni vidonge vya tonsils sio maumivu, ilibidi ninunue vya kutuliza maumivu ndio niliweza kupata nafuu.
 
kuna kipindi nilikuwa ninahisi maumivu kwenye jino la mwisho, nikaenda hospitalini kupiga xray ikaonekana nina jino chini ya fizi, inabidi litolewe.

Nikaweka appointment ili niende kesho yake kulitoa.

Asubuhi na mapema nikawahi hospitalini, Daktari nilekutana nae ni kijana mdogo mwenye rika la 24 hadi 25 na nilijua ni mwanafunzi, mwalimu wake ambae ni daktari tulieonana jana yake alikuwa anampa maelekezo fanya hii fanya vile.

Kosa la kwanza kabisa alilokosea ni kuweka kiwango kidogo cha dawa ya ganzi, kwakweli nilikuwa napata maumivu makali sana, ilibidi mwalimu wake aweke tena.

Zoezi likafika la kungo jino anavuta vuuta taratibu bila mpangilio ikabidi mwalimu wake aje kutoa jino lakini mpaka leo jino linalofuatia ni kama limchimbika, nikitafuna kitu kigumu kama mfupa ukifikia hapo huwa kuna maumivu, nyama huwa najitahidi kutafuna isifike huko.

Nilipomaliza kutoa jino navyoondoka, Mwalimu wake akamwambia aniandikiea dawa za kutuliza maumivu, hakukagua itakuwa alimuamini ataweza, nilienda kununua dawa hizo lakini hazikuwa za kutuliza maumivu.

Nililia chumbani na utu uzima wangu kwa maumivu niliyokuwa napata, nilikunywa vidonge tena lakini wapi, kuja gundua baadae vile ni vidonge vya kutoa bacteria sio maumivu.
Ni kama mlikuwa na ugomvi. Yaani kakosea vyote?

Ova
 
Ukikomaa nao unapata haki yako,

kuna alielipwa milioni 100 kama fidia, alifanyiwa operesheni ya kichwa badala ya mguu.

Sasa unangojea nini na wewe kufungua kesi upate mihela.

Nyama nayo ni ya kuila upande upande sababu ya Dkt denti kakuharibu fizi.
 
Pole sana mkuu , vijana sikuizi hawasomi wanatumia chatgbt kujibu mitihani matokeo yake ndio hayo
 
Back
Top Bottom