Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Sie twatafuta utamu wa asali ila ndio hivyo na mdudu nae yupo kwenye asaliNani alikwambia kwenye uzinzi huwa tunatafuta UKIMWI
Hakuna mtu amewahi tafuta UKIMWI na haita tokea
hyo ilikua mwaka ganNilikuwepo siku hiyo,, hahahaaa! Huyo Hp alikuwa anaitwa Gwamaka,, jamaa kutoka Mbeya. Alikuwa anasoma HGE mimi PCB Aisee umenikumbusha mbali sana yani. Sisi ndiyo tuliosimamia cruel iliyobaki shuleni isiende kuungana na wahuni waliokwenda kutafta bomba huko mtaani ukizingatia ilikuwa usiku.
Vita ikageuka kati ya walioshiriki na wale ambao hawakushiriki, kwakuwa lilikuwa ni tukio la kushtukiza kweli mwanzoni ilibidi tuikimbie shule maana hao vijana waliokuwa wamevaa ninja walikuwa wanapiga balaa na wakaitwaa mess ikawa chini yao.
Ila tulivyokuja kung'amua ni wanafunzi wenzetu tukaretreat kwasababu sisi tulikuwa wengi zaidi yenu,,, tulitumia mawe sasa. Ninja wao wanatumia stick wakawa hawana namna ila nakumbuka yaliisha usiku huo baada ya walimu kusuruhisha ila kesho yake waliohusika wakachukuliwa hatua.
Hii ilipelekea performance yetu mtihani wa mwisho kuwa chini,,, hadi wengine ndoto ya kusoma MD ikayeyuka nikaishia kusoma BBA na baadae kuingia jeshini.
Pale Shinyanga Sec sitapasau tuliishi kama tupo jeshini.
Chaugingi njombe moja we lazima ni njoss boyKuna siku nmetoka zangu skuli niende nikale chakula cha mchana mtaani(chaugingi) sasa nmetoka maeneo ya shule nafika nje kidgo ya shule naona kwa mbele kuna kundi flani la watu wamesimama, mim nikahisi labda kuna walimu kati yao so ngoja nipite uku kulia nikatokee mbele(hili lilikua ni kosa namba moja nililofanya)
Kumbe pale kuna Wizi ulikua umetokea mchana ule so wakawa wanajadili sasa waliponiona mim nachungulia kwa mbali afu nasita kwenda wakahisi labda ndo Mwizi mwenyew. Ile njia nlopitia jamaa wawili wakanifuata wakanisimamisha, wakaanza kuniuliza natoka wapi naenda wapi. Nikawadanganya kua natoka uko narud hom chaugingi(kosa namba mbili nlilofanya) mara ghafla naona jamaa wameongezeka wamenizunguka wakanambia kaa chini ghafla nikapigwa mtama nikajikuta nmekaa chini. Wakaanza kusema mim ndo mwizi nmepita kuja kusikilizia nin nikaendelea.
Ili kujiokoa na kufanya mambo yasiwe mengi ikabidi niseme mim ni mwanafunzi apa napita naenda kula nifikiri kuna mwalimu pale ndo mana nlikua nawakwepa. Ilibidi adi nimtaje rafiki yang wa chaugingi ambaye hua naenda kula jirani apo na hua namsalimiaga, nikaongozana na wale manyambizi (walikua mob la watu) hadi chaugingi njiani watu wanashangaa tu na wakanichimba mkwara nikikimbia tu wananiita "Mwizi"! Baada ya kutoka chaugingi tukarud tena pale waliponikamata mara kidogo akapita Mwalimu wakamuita "mwalimu akanihoji maswali weee akagundua kua mim ni Innocent sema tu nlifanya WRONG TURN. Badae jama wakaniachia lakin ndo ukaja msala mwingine kwa Ticha kua nlikua natoroka nikiwa Civil tena bila ruhusa. Kosa moja lakin Walimu wanatengeneza makosa 8 apo. Kushukuru msala uliisha sikupewa Sunspaa wala kufukuzwa shule. Kesho yake kama balaa tu Dingi alikua amekuja kunitembelea ndo akakuta kijana wake nina msala huo. Sipati picha kama wale Manyambizi wangechukua maamuzi ya haraka, dingi angekuta maiti ya kijana wake
Utoto ni utoto tu Sikukoma na sikuacha kutoroka
[emoji1787]na matokeo yako yalikuwaje?[emoji1787]Nakumbuka A-level mi na mwanangu cayafas tulikuwa hatupigi msuli na kuingia darasani ilikuwa kwa makando makando
Muda wetu mwingi tulikuwa bwenini tunapiga stori, kucheza draft nk, sometimes tulikuwa tunashinda kijijini.
Ilifika time mwalimu wa darasa alinikana kuwa mimi sio mwanafunzi wake maana hajawahi kuniona darasani.
Bas bwana kutokana kutoingia class perfomance ikawa siyo ya kuridhisha.
Kuepuka hilo me na kayafa tukasema kama vip hatutakuwa tunafanya mitihani, bas tukaadhimu mioyoni mwetu kuwa hatutakuwa tunafanya mitihani na huo mswada ukapitiswa.
PAUKWA PAKAWA hatukufanya baadhi mitihani kadhaa huku tukisingizia kuwa tumefanya na tumekusanya hivyo tunahitaji matokeo yetu. Issue ilikuja sanuka kuwa hatufanyi mitihani baada ya kukwepa test paper kadhaa za ticha mmoja, nae akamua kuwa anatubana tukawa tunafanya kishingo upande.
Basi siku moja huyo ticha akatangaza kuwa atatunga mtihani ila kila mwanafunzi anayetaka kufanya atatoa buku.
Me na kayafa tukajisemea "tayari huu umetupita", sio kwamba hatukuwa na pesa ila kukwepa paper maana kuna mishe tulikuwa tunazifanya pale school zinatupatia pesa za kuishi ki doni.
Siku ya paper me na mwanangu pamoja na wengine ambao hawakujisikia kutoa buku tukawa tuko huko bwenini tunapiga stori Ticha kaingia kugawa paper haoni watu kadhaa kuuliza akaambiwa ni watu ambao hawakutoa pesa.
Ticha akasema poa ila "The asker na cayafas" hawa watafanya huu mtihani bure.
Basi akaamua kutufuata bwenini kutupige paper. Sisi pale ndani tulikuwa tuna kaa kwa machale so wakati anakuja nikamuona nika msitua mwanangu.
Kumbe yule ticha alimstua ticha mwengine waje kutuvamia afu yule ticha mwingine akapita njia ambayo ni blind spot.
Basi pale bwenini kulikuwa na ki store ambacho juu tulitoboa ceiling kwa ajili ya kujificha endapo tuta vamiwa na vikosi vya urusi. Mim nikachumpa nikazama kwenye dari,cayafa akaamua kukimbilia uhamishoni( vichakani) coz bweni lilikuwa karibu na vichaka MAKOSAA
Yule ticha aliyekuwa blind spot akamnoki jamaa yetu akaanza kumuita "we cayafas unakwenda wap embu twende ukafanye mtihani" kayafa hakutaka kugeuka akaendelea kutokomea, mwalimu akasema tena "we kayafa nimekuona embu njoo hapa ukafanye mtihani" lakini kayafa asisikie.
Wakati huo mm nipo darini nawasikiliza nkatamani kucheka ila nkajizuia maana pia ningetoa siri juu la lile handaki.
Basi walimu wakatoa maneno yao pale ya ghadhabu na uchuro kisha wakaondoka.
Basi wakati wa chakula ukafika tukaenda kuchukua chakula hakukuwa na ticha na mtihani ushafanyika so amani amani.
Akatumwa Headboy akaja kutuambia tunaitwa na headmaster. Hapo hata hatujagusa msosi.
Tukaenda mpaka ofisi ya walimu tukawakuta wamejaa full maana walikuwa wanakula pamoja pale ofisini.
Basi tukasomewa mashitaka tukajitetea hatukuwa na pesa, walimu wengine wakachangia tabia zetu mbovu kama za mademu, kutohudhuria parade, class na kulala bwenini.
Basi ikaamuriwa tutafanya mtihani pale ofisini mbele yao na tukitoroka siku nyingne tutafanyia paredi mbele ya halaiki ya wanafunzi,
Tukapewa mtihani kisha wao wakapakua wali nyama na kuanza kula huku sisi tukiteseka na maswali ya physical geography. Nakumbuka ubwabwa ulikuwa unanukia sana na wakati huo sisi hatujala hivyo akili ikawa inawaza chakula kuliko contour za map.
Baada ya kumaliza paper tukakusanya tukarudi kukaa wakatuambia mnaweza kwenda, sisi tukasema huko chakula kimeisha na sisi tuna njaa tukiwa tunalenga ule ubwabwa, maana msosi wa skuli ulikuwa ugali na mchuzi wa wadudu wale weusi wa kwenye maharage maana walikuwa wengi kuliko maharage yenyewe.
Basi tukatia ngumu pale maana tuliona ubwabwa umebaki, headmaster akaamua kutupatia ule ubwabwa tukala kisha tukatokomea kama washindi.
Hadi mwili umesisimkaFUJO ZA WANAFUNZI NA WANAKIJIJI
Dah miaka hiyooo. Nipo sekondari O-level mkoa fulani hiviii waliosoma hapo wataikumbuka hii story maana nilikua aina ya wale wanafunzi ambao anafahamika shule mzima na nilikua nataniwa na kila mtu.
Kulikua na shida kubwa sana ya maji katika mji huo hivyo kulazimika wanafunzi wa shule za boarding za hapo kuwa na kawaida ya kutoka nje ya shule kutafuta maji huko mitaani yaani ilikua ni ubabe na vurugu maana kilichokua kinahitajika ni maji yawe ya kisima salama, kisima cha wazi/shimo ama hata ya mfereji lakini maji yafike shule kwa matumizi binafsi na matumizi ya jikoni endapo darasa lako litakua na zamu na kipindi hiki hata ratiba za darasani hazikua sawa maana wenye zamu ya jikoni wakizingua basi uji mnakunywa saa sita mchana😂😂😂😂😂 au kula wali saa sita usiku kosa maji yamechelewa ilikua kawaida.
Kipindi hicho ilikua inafika hatua mtu ukimaliza kula inabidi uilambe sahani yako kwani hakukua na maji ya kuoshea, tulikunywa maji machafu yaani machafu unayoyajua wewe yaani ile ndoo mnayoingia nayo bafuni(nadhani mnajua hali ya maliwato za shule za bweni za serikali) ndio hiyo mnaitumbukiza kisimani mnachota maji kwa matumizi yooote kuanzia kunywa, kuoshea, kufulia, kupikia,nk hapo kutumia maji chooni ilikua anasa zaidi ya makaratasi na magodoro🤨🤨🤨.
Basi nilikua na kakundi kangu tunajikuta manundaaa hatuogopi mbuzi yeyote baada ya chakula cha jioni tumeenda kunyanyua vyuma ikabidi tushuke kitaa kusaka maji na kuoga hukohuko ilikua mida ya saa mbili usiku no body caring about the so called night prepo.
Sasa kufika kwenye kisima cha wazi kikubwa zaidi hatukukuta foleni tukajichotea maji na kuoga. Wakati tunaoga kuna majamaa wawili ambao ofcourse tulikua tunafahamiana nao (kutokana na harakati zetu chafu na uhuni za mtaani) walikua wanaishi jirani kabisa na kisima na walikua wamelewa, sasa wakaanza kututolea maneno machafu sana na ninaamini hawakututambua kutokana na kulewa.
Kikatuuma sana wana tulikua 6 tukaamua tukiwashe, ukumbuke ni usiku sasa hiyo inaenda saa nne basi tukawachezeshea kichapo na walipiga kelele kinoma nadhani hadi wanakijiji wengine wakasikia. Ili kuonesha sisi ni wababe zaidi tukaanza kurusha mawe mazito kwenye paa la nyumba ya washkaji ASALALEEEEH kumbe wanakijiji wamejikusanya waje kutoa msaada.
Sasa kutokana na jeuri ya wanafunzi wanapokua wanafuata maji kijijini kulikua na chuki imejengeka kwa wanakijiji juu ya wanafunzi ni vile tu walikua wanakosa namna ya kulipiza sasa na sisi ndio tukawa tumeingia king wenyeweee. Ebwanaee, baada ya kumaliza hilo timbwili letu kuwapiga majamaa na kufanya vurugu tukaamua tusepe sasa njia ilikua ni ile ya imesongwa na nyasi so mnavyopita mnakaa kama msululu kama bata na wanae mimi nikiwa wa mwisho kabisa nikiwa nimebeba maji nusu ndoo na tochi mkononi.
Ghafla tunakutana na nyomi la wananzengo mzee mwenye jiwe, fimbo na silaha nyingine za jadi kumbe wanatulia timing basii nilichosikia ni WEZI WENYEWE HAWA HAPAAA KAMATAAA.
Ilikua ni nyuma geuka, mimi nikawa wa kwanza nilikimbia nikapaa kile kisima ambapo hadi leo sijui niliwezaje mbele kulikua na matuta yale ya majaruba nikajikwa nikaanguka, hapo ujue wanakijiji wametuungia na kelele za weziiii weziiiiii🔥🔥🔥🔥🔥🔥.
Ile nataka kuinuka nikasukumwaa na mwenzangu nikarudi chiniiii wanakijiji hawa hapaaa, usiombe babaangu, ndani ya sekunde kadhaa nilikua nakiona kifo hiki hapa nilipiga kelele ambazo sijawahi kupiga maishani mwangu nikijitetea kuwa mimi sio mwizi bali ni mwanafunzi wa hiyo shule.
Nashkuru kuna mzee mmoja pale wenye hekima akaingilia kati nisiendelee kupigwa japo wanakijiji kila mmoja alikua na hasira na tabia chafu za wanafunzi mfano kuchota maji kibabe wakikuta foleni( yaani unaweza kuwa na kisima kwako ila tukifika tunakusubirisha kuchota hata ya kupikia), kuiba mazao ya bustani kama miwa na matunda, kuiba mademu zao, nk ambazo nyingine hata mimi nilikua nazo basi nikawa nimepelekwa sehemu kuna taa nahojiwa pale ratiba inayofuatia ni kupelekwa polisi kwa uharibifu tulioufanya na wakati huohuo kuna baadhi ya raia wenye hasira wananipa ngumi au makofi ya kuvizia, sisahau mshkaji mmoja yuliwahi kula demu wake namkumbuka vizuri kabisa alinipa kichwa cha pua aisee nikaishia kuona nyotanyota.
Lakini akatokea mwana ambaye alikua tunafanya nae michongo flani haramu akateteaa pale uwongo na ukweli nikaachiwa kwa mkwara mzito, hapo nahisi maumivu kila sehemu.
***********
Sasa wale wenzangu wengine walifanikiwa kufika shule na kugonga kengele ya dharula(ile shule ni moja ya shule inayoheshimu lengele za dharula yaani mtu anaweza asikimbilie kengela ya chakula ila ya dharula usiku ni dk chache tu wapo assembly. Basi jamaa mmoja fala sana akatangaza kuwa nimedakwa na wanakijiji huko wananibaka na tunavyozidi kuchelewa watakuta nimekufa hivyo washuke fasta kuniokoa.
Mwanaaa usiombeeee, ofisi ya vifaa ikavamiwa wa kutoka na fyekeo, jembe, fito za mafagio, mwenye jiwe, na silaha yoyote alibeba shule nzima yenye 800+ students ikashuka village na hasira maana ujue hapo wanafunzi na wanakijiji hawapatani.
Aisee mimi nimeachiwa pale hata wanakijiji hawajatawanyika, nakatisha kona ya kwanza kusepa nachechemea taratibu nipo na mwana aliyenitoa kwenye msala nakutana na wale vimbelembele wa skaut aisee wataka waanze na yule mshkaji nikawapooza nikamwambia mshkaji potea jeshi la kazi limefika hapo ukumbuke wanakijiji bado hawajatawanyika pale walipokua wakinihoji na wanafunzi wanazidi kuja wananiuliza hali yangu palee nikawaambia wabaya wote wapo hapo nyuma kama vipi tuwaibukie.
Kilichotokea huwa sipendi kukumbuka kilitembea kichapo hapo yaani palichafuka, yule mshkaji aliyenipiga kichwa cha pua aisee sikumuacha tulilipana palepaleee nadhani ndie aliyejeruhiwa zaidi maana wana walikua wananiuliza nioneshe aliyenipiga wote wamewekwa mtu kati alitia huruma sana maana alipasuliwa kweli kuna jamaa alimkata na jembe kichwani ameloa damu kichwa choteee. Basi mida ya saa saba operation ya kuniokoa ikaisha tukakusanyana wale wote tuliokua kwenye kisanga tukatunga story moja na kama tulijua, polisi hawa hapa shule tukabebwa hadi kituoni tukahujiwa kila mmoja peke yake na tukatoa story inayofanana.
Pamoja hayo yote ila ni shule ninayojivunia kwa shule zote na levels zote za kielimu nilizopitia ma huwa naimiss sana.
Unamatukio 🙌COUNTERFEIT MONEY
Wakati bado nipo chuo kabla ya msala wa Receipt fake.. ilikua ni mwaka wa pili kama sikosei sem ya pili.
Hii story kama mhusika yuko humu JF atanijua rasmi mimi ni nani. Ila hakuna shida, cha kuogopa ni kifo pekee na bado kidgo kingenikuta!
Jamaa yangu mmoja nilikua naishi naye hostel nje kidgo ya chuo. Yeye kama ilivyo mimi hatukuwa na mkopo, na kwao hawakua vizuri kama ilivyo kwetu. Sema yeye alikua mtoto wa mjini kushinda mimi na alikua ameniacha parefu ki umri. Sema kuna vitabia flani hivi huwa vinafanya watu wanakua marafiki. Kwa namna yeye na mimi tulivyokua, ungeweza kutuita wazee wa michongo katika rejesta za kileo.
Kwa vile tulikua tunakaa room moja, vitu vingi kuhusu mimi vilikua wazi. Sina hela. Nimefulia. Sikua hata na confidence ya kusimamisha mwanamke nimtongoze. Akitaka tutoke out nitampeleka wapi? Kwa hela ipi? Kwaiyo nikawa ni mtu wa kutulia sana ndani na kuishi kikamilifu ndani ya ratiba za chuo na hostel. So unaweza ku imagine vile maisha yangu yalikua Boring!
Siku moja wakati tunapiga story za hapa na pale na jamaa akaniambia kuna mchongo wa siri anataka kunishirikisha. Nikatega sikio vizuri. Akaniambia kuna jamaa anamjua tukimpa kiasi fulani halali anaweza kututumia hadi mara nne yake ya bandia. Kwaiyo sisi kazi yetu ni kutafuta changes (Chenchi) tu ili tupate za halali.
Duh, wakati ananiambia mimi natetemeka. Nikamwambia mwanangu hii issue si inaweza ikatufanya tufungwe kabisa? Akaniambia "Ufungwe na nani?" .. "Tulia nikuoneshe", na mimi nikatulia.
Jamaa akaagiza mzigo, ukafika. Ilikua kama Mil 1 hivi ya Bandia. Nikamuona kwenye zile pande mbili za kuwekea hela kwenye Wallets; upande mmoja kaweka pesa halali kama 30K, na upande mwingine kaweka bandia kama 100K (Laki). Kaoga kamaliza, huyoooo kasepa!
Alikua ni mtu wa viwanja sana, sikumsikia wakati anarudi usiku. Kwaiyo kesho yake ahsubui namuona kakaa kwenye angle ya kitanda anahesabu hela, Duh. Ni kaki na buku be za kutosha. Mshenzi kashikisha watu zaidi ya elf 90 za bandia. Kabaki na 10 tu. Mimi tamaa ikawa imeanza kugonga mlango, nikawa sitaki kuifungulia. Unajua ukiwa umefulia sana vishawishi ni rahisi sana kukuzidi nguvu. Nikaendelea kujikaza huku jamaa yangu anazidi kuagiza mizigo na anapiga hela vibaya mno.
Mimi nampiga tu vi mizinga vya hapa na pale mwisho wa siku nikajikuta na mimi kanigawia fungu la kuchekecha. Ilikua kama laki 5. Laki 4 bandia, laki 1 halali.
Kama uko viwanja pesa za kwanza unatoa halali, halafu unatafuta mhudum mmoja mwenye tamaa unampiga vi ofa vya Beer huku ukiandaa mazingira ya yeye tu kukuhudumia. Akianza kuchangamka unamsukumia hizo noti mdogo mdogo kama hatasanuka ndio imeisha hiyo. Kazi inakua imebaki kuhesabu changes(Chenchi) nikifika hostel.
Shetani ni mjanja sana. Huwa anakulinda ukiwa unaanza magendo halafu baadae anakutelekeza ukisha kolea. Ndio kilichonikuta mimi, sikumaliza hata mwezi kwenye huo mchongo. Mungu huyu ni wa kumshukuru sana! Nisingekua naandika huu uzi hapa sasa hivi.
Kuna mahali nilikuja kusoma kuwa "Katika magendo yoyote yale, daima epuka kuwafanyia watu wenye hali za chini [kama masikini na wenye disabilities] kwa sababu ina create a very bad luck".Mfano mzuri ni watu wanaoiba vipochi vya wa Mama barabarani au sokoni, nadhani mnajua kinachowakuta wakidakwa! Na ndio kilichoniponza, kwa sababu nilikua desperate sana kupata hela haraka haraka nikaanza kuwafanyia hako ka mchezo mpaka boda boda na dereva taxi. Eh bhana eeh. Kumbe walikua wakifika sheli wanakataliwa pesa zao, wengine mpaka wanaitiwa polisi mimi sijui.
Wakawa wamejipanga siku wakimkamata huyo anayetoa pesa za bandia wanamuua. Mimi sikua nafahamu, nilikuja kugundua baadae huko. Sasa kuna boda wawili ambao nilikua napenda sana kuwatumia katika mishe zangu ambao nilikua nawapa pesa halali, hao ndio walikuja kuniokoa siku nimebananishwa nataka kumalizwa.
Siku yenyewe ilikua hivi. Mida ya jioni nimetoka zangu misele nikapita kijiwe kimoja kipya cha toyo nika scan sura za wajomba nikamuona mmoja kama boya boya hivi nikamchagua anipeleke maeneo karibu na Hostel (Huwa napenda kushukia kwa nyuma kidgo). Sasa kosa la kwanza, sikuwa na pesa ya halali hata moja kwenye wallet.
Sijui ilikuaje nikatumia zote huko nilipotoka halafu sikukagua kabla sijapanda boda. Ile nimeshuka si nikampa jamaa ten. Akaanza kuikagua akakuta ni bandia, akanikwida shati faster. Akasema wewe ndio tulikua tunakutafuta. Nikawa nabishana naye pale kwani vipi, kama ni bandia huenda hata mimi nimeshikishwa nikatoa wallet nikachomoa ten nyingine kumpatia alivyoicheck nayo ni bandia. Mama yangu!
Akapigia simu washkaji wa kijiweni na wao wakapigiana simu na wengine wakajaa pale. Mimi najifanys sielewi nimepanick najisachi kila mahali. Akaja jamaa mmoja akasema huyu mnamuhoji wa nini nikapigwa kofi moja la maana mpka nikajikuta niko chini. Nikaanza kulia kwa huruma. Wahuni wengine wanasema litafutwe tairi nichomwe. Ghafla mmoja kati ya wale jamaa naowatumiaga mara nyingi akawa na yeye amefika eneo la tukio. Hapo nimesha shikwa shikwa sana mpaka shati limechanika. Sura yangu imeanza kufanana kabisa na ya mwizi. Moyoni mwangu nimeshakubali kuwa leo ndio mwisho wangu!
Jamaa kuniona si ndio akawambia mbona huyu ni mwanafunzi wa chuo namchukuaga sana. Boda wengine wakakataa kata kata kuwa hakuna huyu ni jambazi hakuna kutetea. Wengine wakataka ninyang'anywe pochi waangalie ID. Ndio wakaona kweli mimi ni mwanafunzi. Hapo nimeshalia nimechoka, nawambia mimi sio mwizi jamani, mtaniua bure tu, nawaelewesha kuwa nilikua na shida nikaamua kuuza simu yangu ya kupangusa nahisi wale jamaa niliyowauzia ndio wamenifanyia huo mchezo hata mimi sielewi kama ni bandia.
Wakanichukua wakanipeleka kituo kidgo cha polisi hakikua sana mbali na pale. Nikaandika maelezo yangu na wao wakaandika maelezo yao. Sikumaliza hata siku tatu jamaa yangu akaja na wenzake wawili kuniwekea dhamana. Mambo yalikuja kuisha lakini baada ya hilo tukio na jamaa yangu akaachana na hayo mambo kabisa.
Bado nakumbuka vile nilikua najuta na kusali kule kituoni. Kumbe kufa ni kitu kidogo sana. Nikasema nikitoka hapa naenda nyumba za ibada kutoa sadaka ya shukrani. Washkaji walivyoisikia issue yangu, waliniambia nina bahati sana. Lazima kuna kusudi la Mungu katika maisha yangu ndio maana nimeponea kwenye tundu la sindano.
Kabisa haya mambo inabidi yakemewe, maana hawa jamaa huwa wanafanya dhulma za wazi kabisa.Nashangaa haya mambo kuwepo na Polisi wanajua
Dah pia hii mada imenikumbusha mbali sana, tukio ambalo najutia na likabiharibu kabisa psychologically na hadi leo sijapona na sjui taponaje, but one day tatafuta psychologist anisaidie.
Nimeishi na kulelewa na father pamoja na step Mother tangu nikiwa na 4 years, sababu mzee na mother waliachana (hawakuwahi kuoana ila walizaa tu) then kila.mtu akaendelea na maisha yake, so tulisaliwa wawili na my brother, walivoachana mama akamchukua ny brother (sjui why mzee hakumpenda) na mzee akanichukua mimi , mzee alioa mke mwingine na mother nae aliolewa kwingine kwa kifupi ni kua sikuwahi kuishi na mama yangu mzazi kwa muda mrefu wala brother angu kwa hiyo hatukua na that strong bond japo mother alikua anatravel anakuja Mkoa tulioko anafikia kwenye hotel alafu mzee ananidrop tunasalimiana tutakaa hata for 3 days then anarudi kwa familia yake.
Mwaka flani mzee akafariki, then sad enough mume wa mama yangu pia alifariki mwaka ulioisha kabla ya mzee. Vurugu za ndugu hapa na pale msibani kugombea mali na nini ikabidi step mother ajitoe sababu alikua na mali zake na nyumba zake akaogopa akabidi amcall mama aje akae na mimi (wakati huo kulikua na watoto wengine wawili wa rafiki zake mzee ambao mzee alikua akiwasomesha pia) basi mama akaja ili mali zisipotee ikabidi ahamie kabisa mkoa tuliopo, akahamishia na biashara zake huku. Nilifurahi sana sababu pia alikua na watoto wengine nikajua tayari nina ndugu zangu wengine,.so i was very happy kabisa.
Baada ya muda kidogo nikajikuta upendo wangu mkubwa uko kwa step mother, sababu nilikua naona kama vile ndio mama yangu sababu tulikua na strong bond na alinipenda sana, mother mzazi alikua very strict sana hadi nikaanza kumchukia. Kwanza huyo brother pia alikua muhuni muhuni kiasi nikakuta one day kachukua video game yangu kauza akasingizia wezi walikua, yani wezi waingie getini, waingie ndani pia, kuna vitu vingi vya thamani eti aingie aibe play station 2, nikaanza kumchukia pia.
One day bwana nilikutana na rafiki mmoja nilimpenda sana, ni mdada.ananizidi ila nilimpenda na.alikua anasoma chuo me nipo primary hapo [emoji16], alikua ananirubuni sana nampea vipesa pesa sometimes nafungua pochi ya mother natoa pesa ili tu nikampe yule dem. Na tuliwahi kusex kabisa ila niseme tu alikua ananibaka manake ni mkubwa me wakati niko na 13 years yeye ana 26. Siku moja akaniambia amepoteza simu yake, basi akawa anasema nisaidie nipate simu basi [emoji23] hani mdada mkubwa ananishawishi nimtaftie pesa abuy simu anasema mdanganye mama ako akupee pesa uniletee, basi nikawaza nikasema brother ako na simu, naikumbuka sana wakati huo zile simu za kufunua zina scree nzuri na internet, nikasema huyu fala aliniibia game yangu ngoja nimkomeshe, nikachukua simu yakw alikua anacharge nikamoelekea yule dada, akafurahi, kumbe bwana mfanyakazi aliniona nimeishika wakati natoka nnje, brother akaanza kutafta simu yake haioni, akachanganyikiwa naskia, hapo mama katoja job pia naskia wakatafta balaa nani alikuja home maybe wameiba basi housegirl akasema lakini nilimuona mnyakyusa ipinda ameishika ameenda nayo nnje. Wakanisubiri, sitasahau hiyo siku ambayo imebadirisha kabisa maisha yangu.
Walinichangia wote mama na brother kunipiga nioneshe simu iko wapi, imagine walinifungia kwa chumba changu, wakanichangia walinipiga kamq hawanijua kisa ile simu, mbaya zaidi bro alitumia nondo na mama akawa hadi ananikaba pumzi mpaka nahisi nakufa, nilipigwa kipivo ambacho sikuwahi kuimagine, then nilipoona hapa takufa sababu nilianza kutoka damu puani nikawaambia nilipopeleka simu, nikawaambia wachukue simu yangu number nimesave flani wamcall ndio ako na simu. wakaniacha wakaondoka chumbani kwangu, kumbe nilikua nineumia sana, nikawa nashindwa kupumua, usingizi ukanipitia hapo hapo chini, na baridi la tyles ila nikalala chini hadi asubuhi, wala hakuna aliekuja kunitizama, nikashindwa kunyanyuka, nikajivuta hadi kwenye ukuta, nikaona damu puani zimeanza tena kutoka, mwili unauma kila mahali, nikaanza kukohoa , dah nikajua nakufa pale.jilipianza kukohoa damu, housegirl alipoona sitoki chumbani saa saba tayari akaja kunicheck, alipanick sana akawapugia simu waje wanipeleke hospital wakamjibu nini sjui, ila hawakuja, ikabidi aende nyumba inayofuata akamuita jirani, akaja , daha alipoona hali yangu akachukua gati faster akaniwahisha hospital, akawacall nduo wakajua serious mama akaja amepanick hadi analia , ananibembeleza, nimelala sijielewi hospital, nikapigwa xray hapo, nakumbuka dr anasema bana usitoe pumzi ila nashindwa , after kustruggle ndio akaweza kuchukua picha nzuri ya xray. Majibu hapo dr wakasema mapafu yanechubuka na yameanza kujaa damu , na pia kichwani kuna damage sjui nini , wqkaulizwa what happened , mama akasema nilikua napanda kwenye mti nikaanguka[emoji34][emoji34][emoji34] huku analia, doctor akasema hapo wakiniacha naeza kufa sababu mapafu yanazidi kujaa damu, wakanipa rufaa kwenda bugando, kesho yake tukasafiri faster hadi mwanza na tukafika bugando , nikapokelewa , nakumbuka nililazwa juu kabisa sijui ghorofa ya ngapi, chumba kikubwa cha private tuko wagonjwa wawili tu mmoja mbaba hadi leo namkumbuka nae alipata ajari ya gari na ameungua mwili wote, hata hajalala kitandani ila wamekua kama ametundikwa kitaalamu sana. Nami nikalazwa na kuekea ndoo pembeni ili niendelee kutema damu ,Wakaja wazungu flani wa doctor wakanifanyia xray tena na vipimo kibao wakasema is too complicated how that happened,ila mama akashkilia tu nilianguka kwenye mti, to make story short is just mirracle kupona ilikua tu mirracle sababu walitaka hata nipelekwe india but alitokea dr mmoja usiku kama saa nane amevaa kama masister (hadi leo najiuliza alikua dr ama malaika?) alikua kama mzungu ama muhindi i dont know, akanifata kwa bed akasema tu hebu tusali mtoto wangu, akasari pale after kusali akanipa two pills, akasema meza na ulale, nikameza nikalala, you cant believe kesho asubuhi niliamka sikohoi damu , niliamka na nguvu hadi nikashangaa, kwa mala ya kwanza nikatoka kitandani nikatembea just like that, wakaja madoctor wakaenda kunicheck tena wakasema mbona mapafu yamekua sawa , basi nikapoba just like that na safari ya India ikaishia hapo, nikawahadishia kilichotokea wakawa wanaulizana dr nani alikuhudumia huyo hata hawaelewi.
But after hilo tukio nikamchukia sana mama yangu na brother angu, hadi leo napoandika hivi, siwezi hata feel comfortable kuishi nao, hata nyumbani hatujaishi sana wote, nimesoma boarding school tangu hapo so hatujawahi ishi hata for two month pamoja, hata likizo nilikua naenda hata kwa frineds family tu ili kuwaepuka, kiukweli nashindwa kuelewa , yani nawachukia lafu siwachukii, nawapenda halafu siwapendi, yani hadi leo siwezi ongea na mama hata for 3 minutes kwenye simu, tulivotoka hospita aliniomva samahani na tukasameheana lakini nineshindwa. Nikiwa mbali nao nawakumbuka sana sana yani vibaya mno, hata nataka kuwapigia, ila nikiwaona tu moyo wangu unakua hauna upendo tena, yani sjui nielezee vipi mtu aelewe, manake hata mimi sielewi. Yani nimejitahidi sana kuwapenda tukiwa wote ila nashindwa, mama ananijali sana na ananipenda sana sana ila hata siku nilipomwambia hiyo hali alilia sana hakua na la kufanya. Kiukweli hasa brother angu namchukia sana sana, yani hata nikiona picha yake hakuna upendo kabisa moyoni, sometimes natamani kuwa kama wengine wanavoenjoy na family na wazazi wao kwa furaha ila nashindwa, nafeel very happy nikiwa peke angu ama na watu wengine ila sio mama wala brother. I hope tasaidika one day niwe normal, nimekua affected psychologically na inaniuma sana, ila nimejaribu nimeshindwa na miaka inazidi kuenda, na mpenda sana mama yangu nikiwa peke angu ila nikiwa na yeye moyoni nakua sina furaha kabisa, na kadri anavozidi kunipenda na kunijali , kujaribu kufanya nifurahi basi mimi ndio nazidi kukasoroshwa hadi sometimes naona kabisa anakua analia kindani ndani anahuzunika.
Wazazi muwaadhibu watoto kuendan na umri na pia kwa umakini sana, usipige mtoto kama unaua nyoka, unaeza kuua mtu ama kuleta shida zingine , sometimes kupiga is not a solution at all, handle things kimakini sana. I wish nisingechukua ile simu maybe nisingepatwa na haya ila ndio vile. I will be normal one day for sure.
Sent from my vivo X6D using JamiiForums mobile
Uliukwaa ama ni nini mkuu?Ninachojutiaa ni 2016 dem mmoja hv sister aliniombaa niendee kwakee nikamsaidiee kufungaa kitandaa chake alinunuaa ,nikaendaa bhanaa kilichonikutaaa baada ya kufungaa kitandaa nikaanza kupigishwa story za hapa napale wkt nataka kusepaa akaniambia unaondokaje ujanywa hata soda c ndio akaletaa coca na wine bhanaaa tukaanza kunywa hapo ilikuwaa mida ya saa nne asubuh cku ya jpili huku tunapiga story ,maraa akasemaa ngojaa aandaee breakfast bhanaa bhanaa breakfast ikajaa tukaendeleaa na winee nikamtaniaa ,
Wine aipandi bhanaa nifanyie mpng wa safari mbili kubwaa nikampaa ten afate dukani akakataa akasemaa nisijali ataninuliaaa bhanaa akafata safar akaja nazo ,yy nikamwachia wine [emoji485] mm nikaanza kunywa safari mdg mdg tu ,baada safari zikakoleaa na dem wine ishamlegeza macho full kujichekeshaa tu mwishowee nikatakaa kusepaa ndipo dem akaniambia JIONGEZE nikamwambia hapanaaa ww n km sister tu bhanaa ,
Weeee akakimbilia mlango akafungaa na funguo akachomoaaa bhanaa bhanaa akawaa sasaa ananitaka tuduuu wt uku akiongeaaa mambo mengi na jinc anavyonizimiaaa tokaa cku aliponionaaa mtaani kwangu tokaa ameamia akaona mm ndio mwanaume namfaaaa bhanaa ajaongeaa mengi mwishowee ALINIBAKAAA ,,,baada yakubakwaa na yulee dem ckutegemeaa kbs kilichokujaa tokeaa maishan maana nawaambiaaga watu nilibakwa na mwanamkeee hawaamini kbs
Siata sahau matokeo yametoka nimeongoza mkoa ,mama wa kambo kazushq eti nimeangalizia dah,nilikuwa stiki kwa ndugu woote yaani.
Pole sana mkuu.Aise nikimkumbuka yule mwanamke naishia kujuta kwa nini nilimgegeda siku ile....ndio safari yangu ya arv ilipoanza[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
Kwanini mkuu? Embu tuokoe wengine hapaMm najuta kutoka na demu wa kimbulu na kuapa mimba aisee Hilo kabila ni shidaa.samahan lakin
Badala ya kusikitika nimejikuta nacheka [emoji1787][emoji1787][emoji1787] mkuu kuwa serious.Dah yule demu falansana kaniunganisha kwenye grid ya taifa[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]hapa ni kuishi kwa matumaini tuu