Kisa kipi kilikufanya ujute sana?

Kisa kipi kilikufanya ujute sana?

Well kuna kisa kingine tena yani issue moja hadi leo inanichoma sana pia na kutokujua pia ilinicost sana sana.

Basi mwaka flani nyuma kidogo nilipokua nimemaliza form 6, nikapata kazi moja ya muda somewhere hapa Dsm na nikasema nitaenda chuo mwaka mwingine wacha nifanye hii job kwanza sababu ilikua inalipa poa sana so sikutaka kuiacha tu na pesa zote hizo, basi that time nikawa naishi kwa brother angu mmoja around banana na ni sababu ilikua karibu na job nikasema nitakaa kwa muda, brother alikua anaishi na mwanamke wake mzuri sana, ila walikua hawajazaa but huyo mwanamke ako na mtoto wake, basi hiyo nyumba wamepanga ziko nyumba 3 ndani ya fensi moja, sasa hizo nyumba mbili wamepanga hao single mother nyumba moja, ingine ni mmama tu ako na mtoto wake.mmoja na house girl ila mwanaume wake huwa anakuja mala moja moja na anapesa (ni mume wa mtu so ye ni mchepuko tu ulipangishiwa nyumba nzima).

Hao wamama walikua wambea vibaya sana yani wao hata ukikaa nao like 2 minutes utajua mtaa mzima nini kinaendelea, so walikua mala nyingi wako tu nyumbani , sku moja wakaniambia unajua huyo shemeji yako hampendi huyo unaemwita kaka ako, hampendi na ndio maana hamzalii mtoto, kila mala amapata mimba anatoa, wakanipa hadi ushuuda kua wao.ndo humsaidia hata kumsafisha akinywa madawa yake ya kutoa mimba ikitoka, waliongea sana na mimi maneno yakaniingia. Basi hakuna kitu nachukia kama watu wanaotoa mimba, nikaanza kumchukia kidogo kidogo yule shemeji wakati nilikua nampenda sana hata alihisi kuna kitu i think, pia alikua na roho nzuri sana yule dada ila nikamchukia na nikiona wanagombana hata siwi upande wake tena like before, basi one day kweli kumbe alikua na mimba ila wao wawili tu na mumewe ndio wanajua, basi kumbe mimba tena ilitoka akiwa ndani, akapigia simu friends wake na shangazi yake wakaja kumsaidia, me nimetoka job hapo nakuta hali ndo hivo analia kwa uchungu, nakumbuka niliongea maneno mengi sana that day, nae alikua na hasira mbaya hiyo tukagombana hivo hivo akiwa mgonjwa namtuhumu anatoa mimba makusudi kama hamtaki si amuache, tuligombana sana hadi akanifukuza home, wale wamama wambea walikua nnje wanaskiza nilipotoka wananipongeza , mpaka wakanipa room kwao nikalala sababu ilikua usiku ila yule bro alikua hajarudi, nikaona kwenye dirisha shemeji katoa vitu vyangu vilivyobaki akavichoma moto hapo analia kwa uchungu na hasira, kumbe bwana anamatatizo tu ya kiafya na mimi nilikua sijui thats why mimba hua zinatoka pia.

Tukaachana me nikaenda kwa my friend mwingine alikua ashaanza chuo IFM alikua amepanga nyumba somewhere. Basi after like 1 year ushapita yule bro akanicall shemeji yako amejifungua mtoto wa kiume, nikampongeza hapo bado hatuongei na yule shemeji hata sikumpigia hata simu.

One day kama after 3 month yule bro tena usiku akanipigia akiwa na hudhuni kuu , akaniambia aisee shemeji yako hatunae tena, niliogopa sana nikamuuliza what happened akasema miaka yote shemeji yako ana kisukari, tena kikali sana na anaishi kwa hayo ma insulin, akasema jana yake waliendesha gari hadi morogoro kulikua na msiba wa babu wa huyo mwanamke so wakawachukua na ndugu baadhi wakaenda nao, walipofika shemeji akakumbuka amesahau kubeba insulin, na akamwambia please ninunulie insulin huku tafadhari manake nina stress ila bro akasema haina shida tutawahi kurudi (ubahili japo anasema aliona.mbona huwa anaweza kukaa hata 4 days au wiki nzima bila kuchoma so akaona kawaida tu hakuna kitu kitatokea in 24 hours) wakasema kesho yake wawahi kurudi (alikua muslim family so walizika siku hiyo hiyo) basi akasema asubuhi yake wameamka fresh tu akiwa mzima ila huyo bro kumbe alimgombeza sana wakafokezana na according tu doctor kumbe alikua haruhusiwi hata kua na stress sababu hiyo inapandisha sukari yake kwa haraka sana anaweza kufa, kumbe sukari ilipanda na alikua hana insulin, wakawasha gari kurudi Dar na kwenye gari wanasema alikua fresh tu, wamefika wanaita maili moja akasema wacha nilale, akalala, hadi wanafika ubungo bado amelala , sasa wanawashusha watu wengine walikua kwenye gari wanamuamsha haamki, kumbe ashakufa kitambo ni wa baridi na kaacha katoto kachanga ka 3 month, nikakumbuka lile tukio nilomfanyia na kumbe halikua kosa lake mimba kutoka ila ni sababu ya kisukari, nikaja kujua kumbe yeye ndio alikua hata anataka mtoto sana sana ila anashindwa na hicho kitu kimemuuma miaka mingi, hadi leo najiskia vibaya sana, nikaja kuangalia account yangu ya facebook nikakuta kumbe alinitafutaga kunijulia hali few days ago na akanipigia pia ila number ikawa haipatikani as nilimblock, aisee shemeji.nisamehe sana , hii kitu hadi leo inaniuma sana, sikupata nafasi ya kumuomba samahani eeeh Mungu i hope umenisamehe kwa hili. Alikua anakisukari thats why hata nilipomuapset wale wamama walinipia simu after two days amelazwa hospital. God forgive me kwa kile nilifanya[emoji20].

Sent from my vivo X6D using JamiiForums mobile app
 
Yamenikuta km yako mi ni mwaka mmoja nyuma tena mke wangu na nina watoto nae tumegombana kwa kisa kdgo tu nikamludisha kwao amekaa km mwaka kwao lkn tunaendelea na mausiano yetu km kawaida siku ya tarehe 1 mwenzi wa 10 saa kumi 11 nampigia cm anapokea mtoto analia ananiambia baba njoo kanisani mama kaanguka nampigia mkubwa wao ananiambi njoo anaendelea vzr yupo hospital nafika naambiwa amefariki njiani.HAWA POPOTE ULIPO JUA BADO NAKUPENDA JAPO NINA MKE MWINGINE NA MTOTO WA KIUME AMBAE MI NAWEWE HATUKUBAHATOKA KUMPATA ILA MAISHA YA WOTOTO NI MAZURI SN MKUBWA YUPO CHANG'OMBE ANAINGIA KIDATO CHA SITA MWINGINE YUPO KIDATO CHA KWANZA NA G YUPO DARASA LA PILA ILA YULE MWANAMKE ULIEMCHUKIA NDO AMEKUWA MKE WANGU NA ANALEA WATOTO VZR PAKA NDUGU ZAKO WANAMWONA KM NDUGU YAO
Ooh pole sana mkuu. Na hongera kwa kupata mke anayewalea vizuri watoto wako.

Btw huyo mke wako wa sasa hivi; umesema kuwa marehemu mkeo alikuwa akimchukia. Alikuwa mchepuko wako au alichukiwa kwa sababu gani?
 
Well kuna kisa kingine tena yani issue moja hadi leo inanichoma sana pia na kutokujua pia ilinicost sana sana.

Basi mwaka flani nyuma kidogo nilipokua nimemaliza form 6, nikapata kazi moja ya muda somewhere hapa Dsm na nikasema nitaenda chuo mwaka mwingine wacha nifanye hii job kwanza sababu ilikua inalipa poa sana so sikutaka kuiacha tu na pesa zote hizo, basi that time nikawa naishi kwa brother angu mmoja around banana na ni sababu ilikua karibu na job nikasema nitakaa kwa muda, brother alikua anaishi na mwanamke wake mzuri sana, ila walikua hawajazaa but huyo mwanamke ako na mtoto wake, basi hiyo nyumba wamepanga ziko nyumba 3 ndani ya fensi moja, sasa hizo nyumba mbili wamepanga hao single mother nyumba moja, ingine ni mmama tu ako na mtoto wake.mmoja na house girl ila mwanaume wake huwa anakuja mala moja moja na anapesa (ni mume wa mtu so ye ni mchepuko tu ulipangishiwa nyumba nzima).

Hao wamama walikua wambea vibaya sana yani wao hata ukikaa nao like 2 minutes utajua mtaa mzima nini kinaendelea, so walikua mala nyingi wako tu nyumbani , sku moja wakaniambia unajua huyo shemeji yako hampendi huyo unaemwita kaka ako, hampendi na ndio maana hamzalii mtoto, kila mala amapata mimba anatoa, wakanipa hadi ushuuda kua wao.ndo humsaidia hata kumsafisha akinywa madawa yake ya kutoa mimba ikitoka, waliongea sana na mimi maneno yakaniingia. Basi hakuna kitu nachukia kama watu wanaotoa mimba, nikaanza kumchukia kidogo kidogo yule shemeji wakati nilikua nampenda sana hata alihisi kuna kitu i think, pia alikua na roho nzuri sana yule dada ila nikamchukia na nikiona wanagombana hata siwi upande wake tena like before, basi one day kweli kumbe alikua na mimba ila wao wawili tu na mumewe ndio wanajua, basi kumbe mimba tena ilitoka akiwa ndani, akapigia simu friends wake na shangazi yake wakaja kumsaidia, me nimetoka job hapo nakuta hali ndo hivo analia kwa uchungu, nakumbuka niliongea maneno mengi sana that day, nae alikua na hasira mbaya hiyo tukagombana hivo hivo akiwa mgonjwa namtuhumu anatoa mimba makusudi kama hamtaki si amuache, tuligombana sana hadi akanifukuza home, wale wamama wambea walikua nnje wanaskiza nilipotoka wananipongeza , mpaka wakanipa room kwao nikalala sababu ilikua usiku ila yule bro alikua hajarudi, nikaona kwenye dirisha shemeji katoa vitu vyangu vilivyobaki akavichoma moto hapo analia kwa uchungu na hasira, kumbe bwana anamatatizo tu ya kiafya na mimi nilikua sijui thats why mimba hua zinatoka pia.

Tukaachana me nikaenda kwa my friend mwingine alikua ashaanza chuo IFM alikua amepanga nyumba somewhere. Basi after like 1 year ushapita yule bro akanicall shemeji yako amejifungua mtoto wa kiume, nikampongeza hapo bado hatuongei na yule shemeji hata sikumpigia hata simu.

One day kama after 3 month yule bro tena usiku akanipigia akiwa na hudhuni kuu , akaniambia aisee shemeji yako hatunae tena, niliogopa sana nikamuuliza what happened akasema miaka yote shemeji yako ana kisukari, tena kikali sana na anaishi kwa hayo ma insulin, akasema jana yake waliendesha gari hadi morogoro kulikua na msiba wa babu wa huyo mwanamke so wakawachukua na ndugu baadhi wakaenda nao, walipofika shemeji akakumbuka amesahau kubeba insulin, na akamwambia please ninunulie insulin huku tafadhari manake nina stress ila bro akasema haina shida tutawahi kurudi (ubahili japo anasema aliona.mbona huwa anaweza kukaa hata 4 days au wiki nzima bila kuchoma so akaona kawaida tu hakuna kitu kitatokea in 24 hours) wakasema kesho yake wawahi kurudi (alikua muslim family so walizika siku hiyo hiyo) basi akasema asubuhi yake wameamka fresh tu akiwa mzima ila huyo bro kumbe alimgombeza sana wakafokezana na according tu doctor kumbe alikua haruhusiwi hata kua na stress sababu hiyo inapandisha sukari yake kwa haraka sana anaweza kufa, kumbe sukari ilipanda na alikua hana insulin, wakawasha gari kurudi Dar na kwenye gari wanasema alikua fresh tu, wamefika wanaita maili moja akasema wacha nilale, akalala, hadi wanafika ubungo bado amelala , sasa wanawashusha watu wengine walikua kwenye gari wanamuamsha haamki, kumbe ashakufa kitambo ni wa baridi na kaacha katoto kachanga ka 3 month, nikakumbuka lile tukio nilomfanyia na kumbe halikua kosa lake mimba kutoka ila ni sababu ya kisukari, nikaja kujua kumbe yeye ndio alikua hata anataka mtoto sana sana ila anashindwa na hicho kitu kimemuuma miaka mingi, hadi leo najiskia vibaya sana, nikaja kuangalia account yangu ya facebook nikakuta kumbe alinitafutaga kunijulia hali few days ago na akanipigia pia ila number ikawa haipatikani as nilimblock, aisee shemeji.nisamehe sana , hii kitu hadi leo inaniuma sana, sikupata nafasi ya kumuomba samahani eeeh Mungu i hope umenisamehe kwa hili. Alikua anakisukari thats why hata nilipomuapset wale wamama walinipia simu after two days amelazwa hospital. God forgive me kwa kile nilifanya[emoji20].

Sent from my vivo X6D using JamiiForums mobile app
Duuh pole sana nkamu. Aisee tujitahidi kutafuta amani na watu wote; kama inawezekana. Hivi vinyongo na uchungu huwa vinatumaliza wenyewe tu tunaovibeba
 
Lazima tuwe realistic, hakuna anayeishi asiye na regrets.

Unaweza ukasema hauna regrets ila kuna vitu vilivyopita unatamani ungevifanya vizuri zaidi, au kuna watu ambao haupo nao tena ila unawish wakati walikua karibu yako maybe unge care a little more, au kuna vitu vichache ulikosea wakati unalea watoto wako na unawish muda ungerudi nyuma uvirekebishe, au kuna fursa kubwa ulizikosa/zilikupita kwa sababu hukuweka jitihada fulani ambazo zilikua ndani ya uwezo wako, au kuna vitu ulivikubali kwenye maisha yako ambavyo unawish usingevikubali, au kuna matukio ulishayafanya huko nyuma, and you are not proud of kwa sababu yameweka doa katika historia yako.

Kuna mengi yanayofanana na hayo ambayo kila anayeishi anayapitia. Regrets are there, kikubwa tujifunze kupitia hayo. Tunaposema "No Rear View Mirrors in Life" hatumaanishi kutokuangalia nyuma kabisa, bali kutokuangalia nyuma muda wote i.e. kutokuendesha usukani wa Maisha tukitegemea yaliyopita pekee.

All Love [emoji1479]
Umesomeka na kuekeweka vyema lakini je huoni kwamba uki entertain hizo regrets utaambulia maumivu???

Pamoja na uliyosema regrets zitumike Kama kumbukumbu tu vinginevyo zitakuletea madhara

Solution ya regrets ni kupambana na wakati uliopo maana hizo regrets zilifanywa na akili ya kipindi hicho usiidharau hiyo akili, sasa una akili nyingine unaweza kufanya makubwa zaidi.

The only time is right now
 
kipindi Iko keko hukatizi kimama....Kuna wahuni wa kuitwa wasumbufu ao noma....!nashangaa hao Wana eti kiwanja Chao cha kutambia kilikuwa king palace dah....umeacha inferno au uku JJ amani ya kutosha
Shida totoz that time zinasomeka sana king , nigga huko kwingine ni mbilingembilinge za washua.
 
Ooh pole sana mkuu. Na hongera kwa kupata mke anayewalea vizuri watoto wako.

Btw huyo mke wako wa sasa hivi; umesema kuwa marehemu mkeo alikuwa akimchukia. Alikuwa mchepuko wako au alichukiwa kwa sababu gani?
Alikuwa mchepuko hii ndo faida ya kuwa na mchepuko pindi inapotokea km hivi huwa wanasaidia sn huyu mchepuko alikuwa anajua wanangu kitambo hata watoto nilikuwa nawatuma kwake
 
Alikuwa mchepuko hii ndo faida ya kuwa na mchepuko pindi inapotokea km hivi huwa wanasaidia sn huyu mchepuko alikuwa anajua wanangu kitambo hata watoto nilikuwa nawatuma kwake
Aaah kwa hiyo ulitegemea mkeo aupende mchepuko wako? Yaani ni kama unamsimanga marehemu mkeo kwamba mwanamke aliyemchukia ndiyo amekuwa mwema kwa watoto wake leo; una-justify kila ujinga na unyama ulioufanya kwa marehemu mkeo na ndoa yenu. Yaani ulikuwa na mkeo wa ndoa; ila hadi watoto ulikuwa unawatuma kwa mchepuko??? Huyo mkeo wa sasa hivi; hata awe mwema kiasi gani haibadili ukweli kwamba wakati mkeo yupo hai; wewe na huyo mchepuko wako ndiyo mlivunja ndoa yenu kwa uzinzi, na mlimsababishia marehemu mkeo mateso, maumivu na stress. Na usikute yeye ndiyo alichangia hata kumrudisha marehemu mkeo kwao. Mtubu, yasije yakawarudi na ninyi

So na sasa hivi una faida nyingine pembeni (mchepuko?). UMENISHANGAZA, UMENISIKITISHA....... Anyway, to each his own.
 
Sitahau Tuliuza mbuzi wa headmastress .iAlisema kama mnatak shule tulimpe mbuzi wake bila ivyo nyumbani bila hadhabu shule huna. bahat nzur nilikuwa na kadem kiongozi wa chakula Ili nisfukuzwe shule aliniambia ataniibia mahidi nikauze nipate hela ya kulipa mbuzi.Yule dem alikuwa ananielewa balaa .Akaniambia siku ya kwenda kusaga atazidisha hesabu ya kilo za kupeleka mashineni akazidisha loba mbili debe kumi kila roba pale ilitakiwa 140,000/= coz walikuwa mbuzi wawili kweli Tulanikikwa kulipa wale mbuzi kesi ikaisha lakin yule dem alikuwa ana wivu sana alikuwa akion nipo na msichana ana nimaindi sana.mim nikaona isiwe kesi bhna ngoja niachane nae la kuwa liwepo kunasiku nikaamzaba vibao kwnye michezo alikuwa ananitukana baadae mambo yakaisha nashangaa nimeitwa kw mwlim wa nidham anasema nilienda kwenye bwen la wasichana kumfata msichana mwingine tofauti na uyu aliekuwa dem wangu kumbe yule demu alienda kunichongea kwa walimu kwmba mm nalala bweni la wasichana daah niliumia sana kusingiziwa vile na yule dem baadae akaletwa dem mwingn at sijawai kumtokea nikaaambiwa ulikuw unamfata uyu bas pale tukalimwa adhabu wote mim na yule dem kufatua tofali elf tatu kila.mmoja. Sitahau .
 
Aaah kwa hiyo ulitegemea mkeo aupende mchepuko wako? Yaani ni kama unamsimanga marehemu mkeo kwamba mwanamke aliyemchukia ndiyo amekuwa mwema kwa watoto wake leo; una-justify kila ujinga na unyama ulioufanya kwa marehemu mkeo na ndoa yenu. Yaani ulikuwa na mkeo wa ndoa; ila hadi watoto ulikuwa unawatuma kwa mchepuko??? Huyo mkeo wa sasa hivi; hata awe mwema kiasi gani haibadili ukweli kwamba wakati mkeo yupo hai; wewe na huyo mchepuko wako ndiyo mlivunja ndoa yenu kwa uzinzi, na mlimsababishia marehemu mkeo mateso, maumivu na stress. Na usikute yeye ndiyo alichangia hata kumrudisha marehemu mkeo kwao. Mtubu, yasiye yakawarudi na ninyi

So na sasa hivi una faida nyingine pembeni (mchepuko?). UMENISHANGAZA, UMENISIKITISHA....... Anyway, to each his own.
MMH huyu amenisikitisha sana na kunishangaza sana, ila Mungu wa haki yupo
 
Kwenye Maisha tunajifunza kutokana na makosa na makosa yanaleta majuto kabla ya funzo.

Aidha ufanye kosa kwa siri au hadharani, ni lazima likugharimu kwa namna moja au nyingine na hivyo kupelekea majuto.

Kuna vitu huwezi kuzungumza na watu wanaokufahamu vizuri, kuna vitu vinabaki mioyoni mwetu kwa muda mrefu sana.

Lakini sehemu kama JamiiForums ambapo kila mtu ni kama mgeni tusiyemfahamu panafaa kabisa kutoa yale ambayo tunayabeba mioyoni mwetu kama majuto labda huenda yakamsaidia mtu mwingine kwa namna yake.

Unajutia vitu gani kwenye maisha yako?

Binafsi nina vitu fulani ambavyo niliwahi kujutia sana. Nitakuwa nashare kimoja kimoja kadiri navyopata muda.


FAKE BANK SLIPS

Kipindi fulani miaka kadhaa nyuma, wakati nasoma Chuo niliwahi kuingia katika harakati haramu za kuforge receipt za Malipo ya Ada. Ilinigharimu Sana!

Wakati huo maisha ya Chuo yamekuwa magumu sana, mambo ya ujana ni mengi halafu mpunga naotumiwa kutoka nyumbani hautoshi kabisa kumudu gharama zisizo rasmi.

Basi bhana, ilivyotokea hiyo story ya kuwa kuna namna unaweza kutoa pesa kidogo kama robo tu ya Ada unayolipa kisha ukapokea receipt halali ya Bank yenye malipo ya Ada kamili nikajikuta nimeingia mkenge kirahisi.

Tafuta connection mpaka nikakutana na jamaa mmoja ambaye ndio anaratibu huo mchongo. Kazi ikaanza. Wakati huo nipo mwaka wa mwisho ila Sem ya kwanza.

Nikaona maisha si ndio haya. Nakumbuka nilikua nalipa kama Mil 2 kasoro hivi ya Ada ya mwaka mzima. Kwahiyo nikawa nikitumiwa pesa ya Ada natoa kama jiwe 5 tu, receipt ya ada kamili hii hapa. Nikienda kwa mhasibu ni mhuri Twacha! Nishaingia kwenye kundi la walipa Ada naanza kupambana na Modules. Alikuwa wapi huyu Jamaa miaka yote hiyo nasota bure, Dah!

Sem ya kwanza ikaisha ki ulaini sana, Sem ya II ikaanza kama kawaida nikamcheck mzee wa michongo akanifanyia utaratibu chap maisha yakaendelea.

Kipindi hicho mpaka washkaji zangu wakawa kama hawanielewi elewi, si unajua tena zile umetoka na mwana kitaa kimoja anajua uchumi wenu vizuri halafu anashangaa mwana ghafla tu kila kitu huulizi bei na hukaukiwi Mchuzi! Duh, wangejua nilipojiingiza hata wasingekubali kupokea mia yangu.

Muda ukaenda, wiki zikakatika. UEs zikaanza. Kizaazaa kikaja!

Nakumbuka zilikua zimebaki kama paper 2 tu nimalize Chuo, katikati ya mtihani anaingia Dean of Student na maafande.

Heh! Moyo ukafanya Paah, Mkono ukaanza kutetemeka mpaka kalamu ikaanguka chini. Sijamalizia kuokota kalamu nasikia jina langu linaitwa, Mama yangu! Nimekwisha!

Nikasimama nikatoka nje wajomba wakaniambia kijana uko chini ya ulinzi. Kila mtu hapo ndani ya chumba cha mtihani wanashangaa. Laskaboza kafanya nini tena jamani? Mbona hanaga shida na mtu.

Unajua kuna kitu watu huwa hawajui kuhusu kukamatwa na mapolisi. Siku wanakuchukua huwa wanakuchukua kama utani vile, kama vile wanaenda kukuhoji tu kidogo kesho yake unatoka.

Aaah thubutu, nilikaa Central karibu wiki mbili, mpaka nikahamishiwa Magereza Bulalifuu. Naona kama ni Movie ya kihindi inanitokea lakini ni painful reality. Nimeshakuwa Mfungwa!

Wazee wakafunga safari kutoka mkoani wakaja Chuoni kujua kulikoni. Sitasahau aibu niliyoipata wakati namuona mzee wangu. Laskaboza? Imekuaje Mwanangu? Uliomba nini hukupewa? Pesa zote ulikuwa unapeleka wapi? Uchungu niliokuwa nao jumlisha na uchungu wa mzee, hali ikazidi kuwa Mbaya.

Story zikasambaa Chuo kizima, Laskaboza ni tapeli, ametapeli Chuo. Ubaya wa haya mambo, akikamatwa mwingine anasema wewe ndio ulimwambia kwahiyo mimi ndio nabanwa niseme mashine za kufyatulia Receipt ziko wapi. Niliteseka sana.

Kwa sababu hata yule jamaa aliyeniingiza huko alishamaliza Chuo mwaka mmoja kabla yangu. Kwaiyo alikua mtaani tayari. Alivyosikia nimedakwa, akapotea. Akawa hapatikani tena.

Aisee, hakuna rangi niliacha kuona. Hii story ni ndefu sana, ila ki ufupi nilikuja kuachiwa baada ya miezi 4.. walikuja kugundua hata mimi sijui mahali hizo receipt zinafyatuliwa.

Waliofanya mpango uvuje ni Auditors. Maana Chuo kilikuja kugundua pesa hazionekani Bank lakini zipo kwenye makaratasi.

Kwaiyo wakaguzi wa mahesabu wakishirikiana na Bank ndio wakagundua huo mchongo. Ki ukweli ulinigharimu sana. Nilijuta sana. Watu wa nyumbani kwetu walihisi nimelogwa ili nisimalize Chuo, Duh

Nilikuja kumaliza masomo yangu miaka miwili mbele, maana hapa katikati habari zangu zilikua zimeshasambaa sana.

Kwaiyo hata kurudi ikawa ngumu mnoo. Nilikuja kukubaliwa miaka miwili mbeleni baada ya mabadiliko katika uongozi wa Chuo kufanyika.

Hakika nilijutia sana

Kamwe usije ukaingia kwenye michongo meusi. Maana ina tabia ya kukolea kama sukari halafu ikishakolea unajisahau. Unajikuta umeharibu, maisha yanaanza kuwa Machungu!

Kisa kipi kilikufanya
Kisa kama hiki kilimgharimu shemeji yangu akawa amefukuzwa chuo mwaka wa mwisho, Ili bidi aende jeshi kwa mayokeo ya six

Nilikunywa sana bia zake bila kujua anapata wapi hela
 
Back
Top Bottom