Kisarawe: Watu 8 wavunja nyumba saa nane usiku, wabaka, waiba na kujeruhi kwa mapanga

Kisarawe: Watu 8 wavunja nyumba saa nane usiku, wabaka, waiba na kujeruhi kwa mapanga

KATIBA MPYA NDIYO SULUHISHO LA HAYO YOTE.
Katiba mpya? Inaondoaje vibaka. Kinachotakiwa ni kuimarisha mifuko ya ulinzi kuanzia ngazi za jamii, kipindi cha nyuma polisi jamii ilitiliwa mkazo kukawa na ulinzi shirikishi vitendo vya uhalifu vikapungua. Wakati wa mwendazake akasimamia uwajibikaji wa viongozi kila ngazi kukawa hakuna uzembe, kwa sasa hakuna uwajibikaji wala ndo sababu haya yanarudi. Mlinda nchi ni mwananchi kwa kuwa wahalifu ni ndugu zetu, watoto nk, tusimame kwa pamoja.
 
Kundi la watu wanaokadiriwa kuwa 8 usiku wa kuamkia Juni 4, 2022 wamevunja nyumba moja iliyopo Mtaa wa Bomani Wilayani Kisarawe Mkoani Pwani na kufanya ukatili wa kubaka, kuiba vifaa vya ndani na kujeruhi kwa mapanga na kutokomea kusikojulikana

Wahalifu hao walifunga komeo kwa nyumba za majirani ili wasiweze kutoa msaada. Majeruhi, Estem Sevenia amelazwa Hospitali ya Wilaya ya Kisarawe baada ya kucharazwa mapanga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Pius Lutumo amekiri kutokea kwa tukio hilo na kusema msako unaendelea kuwatafuta waliohusika na tukio hilo.

Mganga wa Zamu, Dkt. Sadi Amri amesema Estem amejeruhiwa kichwani na kwenye vidole.

Source: ITV
Huko ndio kuna DC mlamba lips kazi kuuza sura mitandaoni
 
Back
Top Bottom