Kisheria na kikanuni, Yanga pia hawatambuliki kama walikuwepo uwanjani siku ya 08 March, 2025

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Watu wanadai pwenti 3 za bure wakati hata wao hawajafuata taratibu zinazoweza kuwapa nguvu ya kudai hizo pwenti tatu.

Tuachilie mbali tukio la kuvunja kanuni kwa kuzuia mpinzani wake asifanye mazoezi na kumfanyia vurugu usiku wa kuamkia mechi husika.

Tuachilie mbali kuvunja kanuni kwa kuingia uwanjani kwa kutumia milango isiyo rasmi. Tuachilie mbali kutokuwepo kwa maafisa wa TFF, Bodi ya Ligi wala waamuzi wa mechi uwanjani ili kushuhudia uwepo wa timu mojawapo iliyotimiza taratibu za mechi.

Soma Pia: Bodi ya Ligi kuu yaahirisha Mechi ya Derby kati ya Yanga dhidi ya Simba

Embu twende kwenye fact kuwa hakuna picha wala video yoyote ya Yanga wakiwa uwanjani wakiwa wamevaa jezi rasmi zinazotambulika na TFF za msimu huu wakiwa tayari kwa mechi husika.

Kisheria na kikanuni, Yanga pia hawatambuliki kama walikuwepo uwanjani siku ya 08/03/2025.
 
Wewe uwezo wako wa kufikiri uko sawa na wanavyo fikiri wajumbe wa bodi ya Ligi ya Tanzania
 
Ulikuwepo uwanjani wakati Simba “inazuiliwa” kuingia uwanjani au umesoma taarifa Facebook tena za upande mmoja?

Kwamba wale wahuni wanaosemekana waliwazuia wachezaji wa Simba ndio Yanga wale? Kwamba wana misuli na mbinu za kuweza kulizidi jeshi la police?
 
Suala ni mechi imeahirishwa basi hamna pwenti 3 za bure subirini tarehe itangazwe sasa ole wenu msije.
 
Kama "Makolo" mnaowaimba katika nyimbo zenu zote ghafla mkawakana kwa kusema hakuna timu hiyo katika ligi ya NBC, tutashangaa vipi mkiwakana hao Janjaweed na M23 mliowatuma kufanya uhuni?
 
Kile kilichofanyija trh 8 ilikuwa planed, imeisha hiyo jilaumuni tu ninyi mashabiki wa hizo Tim za kariakoo
 
Suala ni mechi imeahirishwa basi hamna pwenti 3 za bure subirini tarehe itangazwe sasa ole wenu msije.
Mpira huongozwa kwa kanuni. Hii mbungi bado mbichi sana na ikibidi itafika CAS

Kila mtu (Simba, Yanga, Bodi ya Ligi) lazima apate adhabu stahiki kwa kuzua taharuki maana kanuni na miongozo ipo wazi kabisa. Tungekuwa na TFF imara, mechi ingebaki kama ilivyopangwa na Simba angekuwa forced kwenda uwanjani

Ila sasa, tuna viongozi wa mpira wa hovyo sana Nchini
 
Hamna cha CAS wala SAC, tutamalizana wenyewe kwa wenyewe hapa hapa.
 
Soka la bongo ni tamthilia kubwa na linafuatiliwa kuliko hata mchezo uwanjani. Safari ya kutwaa ubingwa wa Africa Bado ndefu sana
 
Pia mechi imeahirishwa kwa kanuni inayoipa nguvu na mamlaka bodi ya ligi kuahirisha mechi yoyote muda wowote.
Au hujui kama ipo hiyo kanuni
 
Hawana akili.
 
Tanzania watu wengi uwezo wao wa kutafsiri mambo ni mdogo,(lack of background knowledge)
Cha ajabu wanajua kubushana bila hoja
 
Hata kama wangekesha, ni sawa na hakuna.

Ila siri usimwambie mtu.....

Walifuata majini yao baada ya mechi kuahirishwa.
 

Mnahangaika na Yanga nyie si mmegomea mechi zilizobaki ? Mlitumia kanuni gani?

Endeleni kugoma, Yanga itaendelea na mechi zake zilizobaki. Kila mmoja na maamuzi yake,halafu tuone nani atashikilia msimamo wake........?
 
Mnahangaika na Yanga nyie si mmegomea mechi zilizobaki ? Mlitumia kanuni gani?

Endeleni kugoma, Yanga itaendelea na mechi zake zilizobaki. Kila mmoja na maamuzi yake.
Simba walichungulia kaburi, wakaona bora wakimbie tu wanao jua madhara ya kipigo hukimbia Kam mwizi

All in all, Simba SC on this issue failed to play the cards right, (not smart as an institution)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…