KISIASA: Tanzania tuna chama kimoja tu, CCM!

KISIASA: Tanzania tuna chama kimoja tu, CCM!

SALOK

JF-Expert Member
Joined
Sep 20, 2011
Posts
3,364
Reaction score
2,001
Inasikitisha, Inahuzunisha ila uhalisia unabaki hivyo.

Nchi ya Tanzania kama yalivyo mataifa mengine Duniani inatamaduni zake na mifumo yake ya kiutawala! Democracy ndio mfumo unaotumika ktk kuendesha Nchi hususani mfumo wa vyama vingi vya siasa!

Tanzania kuna vyama vingi vya siasa vikubwa kwa vidogo! Ktk hivyo vipo vichache ambavyo ktk kipindi fulani kwa nyakati tofauti tofauti vipo vilivyokuja na sera na mikakati ya maana ktk kuonesha utayari wa kuchukua Nchi, hapa nazungumzia vyama pinzani. Lakini kwa kukosa pengine umadhubuti ktk sera na mikakati na ustahimilivu kwa sasa karibia vyote vimekumbwa na dhoruba kali la upinzani toka serikalini na chama kinachounda serikali na kisha kusambaratikia mbali huko, vimebaki majina tu, na hayo tunayashuhudia kwa NCCR-MAGEUZI, CIVIC UNITED FRONT (CUF) na CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA).

NINI KIMESABABISHA HALI HIYO?

Pamoja na ukweli kwamba vitimbi vya watawala na chama tawala ndio sababu kuu ya kutosimama imara kwa vyama vya upinzani, vile vilivyoonekana kuwa tishio kwa CCM, lakini pia kuna ukweli kwamba vyama vyenyewe vinaudhaifu mkubwa sana ambao ndio upenyo uliotumika kuvisambaratisha kwa urahisi.

Kukosekana umoja, Viongozi kuwa wabinafsi, kung'ang'ania madaraka, kukosekana ajenda zenye kuwaunga watu ktk misingi ya chama na mengineyo kibao! ni miongoni mwa sababu, sababu zilizopelekea kurubuniwa kirahisi, kugombanishwa na kununuliwa! na kisha kujifia kibudu. UROHO WA MADARAKA/UCHOYO NA KUENDEKEZA NJAA!

Kwa sasa hamna tena chama kilichokuwa imara dhidi ya CCM! Vyama vyote vimebaki kuwa Chawa wa CCM.
VIMETEPETA, LABDA ACT WAZALENDO AMBACHO BADO NI KICHANGA. NASEMA LABDA, TUSUBIRI TUONE!

CCM NDIO MWELEKEO WA NCHI
Hali ya sasa kisiasa ni kipimo tosha kuonesha uhalisia huu, kwamba ccm ndio mwelekeo wa Nchi, Genge lipi ndani CCM likitawala siasa za ndani ya chama basi Nchi itakuwa na mwelekeo huo na hakuna wa kubadili chochote. Makada wa vyama pinzani, wachambuzi wa mambo ya kisiasa, Mitandao ya kijamii na media zote kwa ujumla wote/vyote hivi vimekuwa chawa wa CCM.

Ni ccm ndio inaamua mijadala ktk kipindi hiki iwe nini kumuhusu nani. Nani ndani ya CCM ndiye tumaini la watu na nani hafai na kwa nini. CCM inaamua hayo! Wapinzani hawana tena ajenda, wamebaki kuparamia paramia matukio, hawana ujasiri tena wa kuanzisha ajenda za kitaifa.

Hawana tena Dira, wapinzani wamebaki kuwa machawa wa makada wa CCM. Watampamba leo Bashiru,
Kesho akizibwa mdomo watabaki kimya wakisubiri tukio jingine.

TANZANIA TUNACHAMA KIMOJA TU KILICHOSIRIASI
VINGINE HIVI NI VIKOBA TU
 
Wapinzani wa Tanzania wote wanapigania matumbo yao. Mwaka 2015 Lowasa katuthibitishia hilo baada ya kutumwa na CCM kupeleka pesa kwa viongozi wa chama fulan cha siasa ili apewe nafasi ya kugombea uraisi na kupata chance ya kuusambaratisha upinzani uchwara uliyokuwepo miaka hiyo.

Asilimia 90 ya vijana wa upinzani waliopo humu wanalijua hilo, lkn ndo hivyo wengi wao wanaishi kupitia mifuko ya viongozi wao, kwahiyo hawawezi kuwa na ujanja au ujasiri wa kulizungumzia hili zaidi ya kunungunikia moyoni tu kimya kimya.
 
Wapinzani wa Tanzania wote wanapigania matumbo yao. Mwaka 2015 Lowasa katuthibitishia hilo baada ya kutumwa na CCM kupeleka pesa kwa viongozi wa chama fulan cha siasa ili apewe nafasi ya kugombea uraisi na kupata chance ya kuusambaratisha upinzani uchwara uliyokuwepo miaka hiyo.
Na hawataki kukubali kama kuna tatizo...
 
Inasikitisha, Inahuzunisha ila uhalisia unabaki hivyo....

Nchi ya Tanzania kama yalivyo mataifa mengine Duniani inatamaduni zake na mifumo yake ya kiutawala! Democracy ndio mfumo unaotumika ktk kuendesha Nchi hususani mfumo wa vyama vingi vya siasa!

Tanzania kuna vyama vingi vya siasa vikubwa kwa vidogo!
Ktk hivyo vipo vichache ambavyo ktk kipindi fulani kwa nyakati tofauti tofauti vipo vilivyokuja na sera na mikakati ya maana ktk kuonesha utayari wa kuchukua Nchi, hapa nazungumzia vyama pinzani. Lakini kwa kukosa pengine umadhubuti ktk sera na mikakati na ustahimilivu kwa sasa karibia vyote vimekumbwa na dhoruba kali la upinzani toka serikalini na chama kinachounda serikali na kisha kusambaratikia mbali huko, vimebaki majina tu, na hayo tunayashuhudia kwa NCCR-MAGEUZI, CIVIC UNITED FRONT (CUF) na CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA).

NINI KIMESABABISHA HALI HIYO?

Pamoja na ukweli kwamba vitimbi vya watawala na chama tawala ndio sababu kuu ya kutosimama imara kwa vyama vya upinzani, vile vilivyoonekana kuwa tishio kwa CCM, lakini pia kuna ukweli kwamba vyama vyenyewe vinaudhaifu mkubwa sana ambao ndio upenyo uliotumika kuvisambaratisha kwa urahisi.
Kukosekana umoja, Viongozi kuwa wabinafsi, kung'ang'ania madaraka, kukosekana ajenda zenye kuwaunga watu ktk misingi ya chama na mengineyo kibao! ni miongoni mwa sababu, sababu zilizopelekea kurubuniwa kirahisi, kugombanishwa na kununuliwa! na kisha kujifia kibudu. UROHO WA MADARAKA/UCHOYO NA KUENDEKEZA NJAA!!

Kwa sasa hamna tena chama kilichokuwa imara dhidi ya CCM! Vyama vyote vimebaki kuwa Chawa wa CCM..!!!
VIMETEPETA, LABDA ACT WAZALENDO AMBACHO BADO NI KICHANGA....NASEMA LABDA, TUSUBIRI TUONE!!

CCM NDIO MWELEKEO WA NCHI
Hali ya sasa kisiasa ni kipimo tosha kuonesha uhalisia huu, kwamba ccm ndio mwelekeo wa Nchi, Genge lipi ndani ccm likitawala siasa za ndani ya chama basi Nchi itakuwa na mwelekeo huo na hakuna wa kubadili chochote...
Makada wa vyama pinzani, wachambuzi wa mambo ya kisiasa, Mitandao ya kijamii na media zote kwa ujumla wote/vyote hivi vimekuwa chawa wa CCM.
Ni ccm ndio inaamua mijadala ktk kipindi hiki iwe nini kumuhusu nani..!!
Nani ndani ya CCM ndiye tumaini la watu na nani hafai na kwa nini... Ccm inaamua hayo! Wapinzani hawana tena ajenda, wamebaki kuparamia paramia matukio, hawana ujasiri tena wa kuanzisha ajenda za kitaifa...
hawana tena Dira, wapinzani wamebaki kuwa machawa wa makada wa CCM..!!
Watampamba leo Bashiru,
Kesho akizibwa mdomo watabaki kimya wakisubiri tukio jingine..

TANZANIA TUNACHAMA KIMOJA TU KILICHOSIRIASI,
VINGINE HIVI NI VIKOBA TU..
Sijasoma ulicho andika ila uliposema ccm ni chama cha siasa nikajua moja kwa moja kuwa wewe ni ZUZU ....Kwakifupi tu CCM siyo chama cha siasa ni GENGE LA WAHUNI NA WAHALIFU
 
Inasikitisha, Inahuzunisha ila uhalisia unabaki hivyo....

Nchi ya Tanzania kama yalivyo mataifa mengine Duniani inatamaduni zake na mifumo yake ya kiutawala! Democracy ndio mfumo unaotumika ktk kuendesha Nchi hususani mfumo wa vyama vingi vya siasa!

Tanzania kuna vyama vingi vya siasa vikubwa kwa vidogo!
Ktk hivyo vipo vichache ambavyo ktk kipindi fulani kwa nyakati tofauti tofauti vipo vilivyokuja na sera na mikakati ya maana ktk kuonesha utayari wa kuchukua Nchi, hapa nazungumzia vyama pinzani. Lakini kwa kukosa pengine umadhubuti ktk sera na mikakati na ustahimilivu kwa sasa karibia vyote vimekumbwa na dhoruba kali la upinzani toka serikalini na chama kinachounda serikali na kisha kusambaratikia mbali huko, vimebaki majina tu, na hayo tunayashuhudia kwa NCCR-MAGEUZI, CIVIC UNITED FRONT (CUF) na CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO (CHADEMA).

NINI KIMESABABISHA HALI HIYO?

Pamoja na ukweli kwamba vitimbi vya watawala na chama tawala ndio sababu kuu ya kutosimama imara kwa vyama vya upinzani, vile vilivyoonekana kuwa tishio kwa CCM, lakini pia kuna ukweli kwamba vyama vyenyewe vinaudhaifu mkubwa sana ambao ndio upenyo uliotumika kuvisambaratisha kwa urahisi.
Kukosekana umoja, Viongozi kuwa wabinafsi, kung'ang'ania madaraka, kukosekana ajenda zenye kuwaunga watu ktk misingi ya chama na mengineyo kibao! ni miongoni mwa sababu, sababu zilizopelekea kurubuniwa kirahisi, kugombanishwa na kununuliwa! na kisha kujifia kibudu. UROHO WA MADARAKA/UCHOYO NA KUENDEKEZA NJAA!!

Kwa sasa hamna tena chama kilichokuwa imara dhidi ya CCM! Vyama vyote vimebaki kuwa Chawa wa CCM..!!!
VIMETEPETA, LABDA ACT WAZALENDO AMBACHO BADO NI KICHANGA....NASEMA LABDA, TUSUBIRI TUONE!!

CCM NDIO MWELEKEO WA NCHI
Hali ya sasa kisiasa ni kipimo tosha kuonesha uhalisia huu, kwamba ccm ndio mwelekeo wa Nchi, Genge lipi ndani ccm likitawala siasa za ndani ya chama basi Nchi itakuwa na mwelekeo huo na hakuna wa kubadili chochote...
Makada wa vyama pinzani, wachambuzi wa mambo ya kisiasa, Mitandao ya kijamii na media zote kwa ujumla wote/vyote hivi vimekuwa chawa wa CCM.
Ni ccm ndio inaamua mijadala ktk kipindi hiki iwe nini kumuhusu nani..!!
Nani ndani ya CCM ndiye tumaini la watu na nani hafai na kwa nini... Ccm inaamua hayo! Wapinzani hawana tena ajenda, wamebaki kuparamia paramia matukio, hawana ujasiri tena wa kuanzisha ajenda za kitaifa...
hawana tena Dira, wapinzani wamebaki kuwa machawa wa makada wa CCM..!!
Watampamba leo Bashiru,
Kesho akizibwa mdomo watabaki kimya wakisubiri tukio jingine..

TANZANIA TUNACHAMA KIMOJA TU KILICHOSIRIASI,
VINGINE HIVI NI VIKOBA TU..
Kweli
 
Bila kujitathmini na kukubali mapungufu na kisha kuyafanyia kazi, hakuna kitu Mkuu..!!

CCM sio chama cha siasa acha upotoshaji usio na tija. CCM ni kikundi cha dola kilichovaa koti la chama cha siasa. CCM ikitoka madarakani hakichukui hata mwaka kitakufa kifo ilichokufa KANU ya Kenya.

Ni kweli CCM inajadiliwa huku mitandaoni, ila sio kwa mijadala positive bali kudhalilishwa zaidi. Uoga tu wa wananchi ndio pumzi pekee ya hilo genge liitwalo CCM. Siku watu wataingia mtaani hamtaamini.
 
Na hawataki kukubali kama kuna tatizo...

Kwahiyo tukubali kuwa CCM ni chama bora, ambacho ndani ya miaka 30 imetumia zaidi ya 10t+ bila kumaliza tatizo la umeme! Huo upinzani wenyewe mnaosema hauna nguvu, wizi wa kura na hujuma ndio zinawafanya muuwadhibiti. Kwa mantiki kuwa wapinzani wakiamua kushika silaha ndio itakuwa mwisho wa CCM.
 
Back
Top Bottom