Kisiwa chenye hazina

Kisiwa chenye hazina

SURA YA THELATHINI NA TATU: MWISHO WA SAFARI.

Asubuhi tulipoamka tukaanza kazi ya kupakia hazina melini. Ilikuwa si kazi nyepesi maana tulikuwa watu wachache. Wale waasi watatu hatukuwaona tena, lakini tuliweka mtu mmoja kushika zamu, maana wasije wakatushambulia ghafla. Vipande viwili vya dhahabu vilitosha mzigo wa mtu mzima. Mimi kazi yangu ilikuwa kukaa pangoni na kufunga sarafu za dhahabu katika mifuko, tayari kwa kupakiwa melini.

Lo! Sarafu hizo zikikuwa ni za kila namna na kila nchi, na vidole vyangu viliuma sana kwa kuzihesabu kwa sababu zilikuwa nyingi sana. Basi kazi hii ikaendelea kila siku mpaka zikaisha zote.

Siku moja tulipokuwa tukitembea tulisikia sauti za watu wakiimba, na tukajua ni wale waasi watatu wamelewa. Yule John Fedha aliwekwa huru kabisa, akawa anatembea apendavyo, lakini hapana hata mmoja aliyemuamini wala kumpenda. Tukashauriana tuwafanye nini waasi wale, ikawa sote nia moja, kuwaacha kisiwani. Basi tulipokuwa tayari kujipakia tukawawekea akiba ya chakula na baruti kisha tukangoa nanga.

Wale watu watatu walipoona tunaenda zetu wakaja mbio pwani, wakapiga magoti kutusihi tusiwaache kisiwani, lakini wamechelewa! Hatukuweza kujitia katika hatari ya uasi tena.

Basi bwana Livesi akawaita na kuwaeleza tulipowawekea akiba ya chakula na baruti. Lakini wakazidi kusihi kwamba wahurumiwe. Basi meli ikaanza kutoka pwani. Nao walipoona kuwa hatuwachukui wakaelekeza bunduki zao kutupiga. Risasi zikipita juu juu hivyo ilitulazimu tulale chini mpaka tutoke katika upeo wa shabaha zao.

Basi tukaendelea hivi mpaka saa sita, kutazama nyuma nikaona kile kilima kirefu cha kisiwa kiko mbali kabisa, wala kisiwa chenyewe hakionekani. Sasa nikafurahi kuona mwisho wa kisiwa chenye hazina. Na kwa kuwa tulikuwa wachache sana, ilitupasa wote tushirikiane katika kazi kwa bidii sana. Tukaelekeza meli yetu kwenda kusini ya Amerika. Huko tulikusudia kupata mabaharia wengine wa kutusaidia. Tulipofika ilikuwa jioni, nikifurahi mno tulipoegesha meli bandarini, tuliona watu, tukaona watu weusi wa nchi zile, nikajua sasa hatari ya safari yetu imekwisha. Basi bwana Livesi na bwana Treloni wakashuka pwani, wakanichukuwa na mimi pamoja nao. Tukatembea pwani na kuzungumza na watu wa huko. Tuliporudi ilikuwa ni usiku, na mara tulipopanda melini Ben Gun akatujia na akasema kuwa John Fedha ametoroka na kuwa yeye alimsaidia kutoroka. Basi sisi hatukumlaumu, maana kusema kweli tulifurahi kuwa ametoroka kwa kuwa yeye alituletea kisirani katika safari yetu. Basi tukapata mabaharia wengine kutusaidia. Tukafanya safari njema kabisa, mpaka tukafika mji wa Uingereza, Bristol.

Tulipofika tukapata habari kuwa ile meli ya pili ndiyo kwanza inajitayarisha kusafiri.

Kweli ulevi na shetani umewamaliza wengine. Lakini hatukupata kisirani kama wale walioimba. 'Na mtu mmoja tu ndiye aliyesalia katika sabini na tano waliotoka.'

Sote tulipata mali nyingi tulipogawana ile hazina. Nahodha Smollet akaacha kazi yake ya kusafiri na kukaa raha mustarehe. Gray akaendelea na kazi yake na sasa yeye ni nahodha wa meli kubwa nzuri. Ben Gun alipata mali nyingi sana lakini katika muda wa siku kumi zilikwisha zote! Akaja kuomba. Tukamweka kuwa mlinzi wa nyumba yetu naye akaridhika. Hatukusikia tena habari za John Fedha, nadhani anaishi raha mustarehe.

Bunduki na fedha zingine tuliacha kulekule kisiwani, na labda ziko huko hata leo, wala nami sina nia ya kusafiri tena kwenda kuzichukua. Hata sasa nikilala naota safari na kisiwa, na pengine nasikia mawimbi yakipigapiga mchangani, na pengine nasikia sauti ya kasuku yule, Kapteni Flinti akilia, "vipande vya dhahabu! Vipande vya dhahabu!"

Mwisho.
 
SURA YA THELATHINI NA MBILI: UASI MIONGONI MWA WAASI.


Watu wote sita walisimama kama waliopagawa, lakini katika muda huo mchache, John Fedha akawa amepata akili yake, akanivuta karibu na kuninong'oneza, "Twaa bastola hii uwe tayari kwa matata." Akanipa bastola na akaanza kujongea polepole na kunivuta karibu naye mpaka tukawa tumejitenga na maharamia wale.

Mara wale maharamia wakaanza kutukana na kutoa maneno machafu na makali, na mmoja wao ambaye aliokota vipande viwili vya dhahabu, akavitupa akasema, "hivi ndivyo hazina zote? Wewe ndiye uliyetuongoza, wewe ndiye uliyeharibu mambo yote tangu mwanzo mpaka mwisho."

John Fedha akajibu, "chimbeni rafiki, chimbeni, huenda labda mkaona karanga."

"Jamani mwasikia asemavyo? Nakwambieni kuwa huyu alijua habari hizi tangu mwanzo."

Basi sasa wote wakageuka nia na mmoja wao akasema, "Jamani hawa ni watu wawili peke yao, mmoja ni kilema ambaye ndiye aliyetuleta kwenye shida hii, na mwingine ni kijana ambaye huyo nitamuua mimi. Haya sasa jamani." Akainua mkono kuanzisha vita. Mara ghafla tukasikia milio mitatu ya bunduki iliyopigwa msituni. Watu wawili wakaanguka palepale wakafa na wengine wakageuka na kuanza kukimbia kwa nguvu zao zote.

Basi nasi, John Fedha na mimi tukapiga bastola zetu. Na hapo bwana Livesi, Gray na Ben Gun wakatokea msituni na bwan Livesi akasema, "Haya wafuateni upesi, wasije wakafika kwenye meli." Loo! Tukaanza kuwafuata mbio sana, mpaka tulipojua kuwa sisi tupo katikati yao na meli ndipo tukapumzika.

John Fedha akasema, "ahsante sana bwana Livesi, umetuokoa, na kama ungalichelewa kidogo, mimi na Jim tungaliuwawa. Na wewe Ben Gun, je, habari gani?"

Sasa basi tukawa tunakwenda polepole tunashuka mlima, tukafika pwani tulipoweka mtumbwi wetu na bwana Livesi akawa anahadithia habari zote zilizotokea. Zile hazina zilikwisha vumbuliwa na mtu wa kisiwani, Ben Gun. Alipoachwa pale kisiwani kazi yake ilikuwa kutembea huku na huku kutafuta hazina mpaka akazivumbua, akazichukua na kuziweka katika pango lake. Basi alipomwambia bwana Livesi hayo, likifanywa shauri kutoka mule bomani na kuwaachia wale waasi, na sababu ya kupewa ile ramani ni kwasababu ilikuwa haina kazi tena! Na sababu ya kuwaachia kile chakula ni sababu Ben Gun alikuwa ameweka akiba ya nyama ya nbuzi mwitu.

Basi bwana Livesi alipojua kuwa mimi nimekamatwa na waasi, alifanya mpango wa kuniokoa watakapofika kwenye hazina, maana alitambua kuwa waasi wakijua kuwa hazina imekwisha vumbuliwa lazima kutakuwa utata, uasi katika waasi. Tena ndiye aliyetia fikra ya kumuambia Ben Gun aimbe kule msituni ili kusudi awatishe wale waasi.

Basi tukaingia mtumbwini na kuvuta makasia kwenda kutafuta meli yetu. Tukaiona imetoka uguoni inaelekea bandarini. Sasa tukapanda melini na kukuta kila kitu tayari. Basi tukatengeneza nanga ingine na kuifunga mahali pa kufaa, halafu tukashuka kwenda pwani kwenye lile pango, huko tukamkuta bwana Treloni ambaye alifurahi sana kuniona. Lakini akamwambia John Fedha, "wewe ni mtu mwovu kabisa, tena mwovu sana. Nimeambiwa kuwa sisi tumeahidi kutokushtaki, basi hata mimi nimekubali, lakini sina budi kukuambia kuwa damu za watu hawa zitakuwa kama mzigo juu yako mpaka mwisho wa maisha yako."

John Fedha akacheka na kusema, "asante sana bwana." Hatimaye tukaingia pangoni na kumkuta nahodha Somllet amelala mbele ya moto, na humo nikaona hazina zote zimepangwa. Kulikuwa na vyungu vikubwa vya fedha na dhahabu. Tena dhahabu zingine zilikuwa mfano wa mitalimbo mifupi, ndizo hizi zilikuwa hazina za Flinti tulizozijia. Nikafikiri sana nikaona kuwa, katika wote tuliosafiri na meli ya Hispaniola, wamekufa watu kumi na saba. Je, katika hao waliotangulia, wangapi wamekufa katika kazi hii ya kutafuta hazina?

Basi bwana nahodha akafurahi sana kuniona, akasema, "wewe ni kijana mwema Jim, lakini nadhani mimi na wewe hatutasafiri tena pamoja. Wewe una bahati sana. Oh! Na wewe John Fedha wataka nini?

John Fedha akajibu, "nimerudi kazini. " Nahodha akajibu, "vema" bila kuongeza neno jingine. Basi usiku ule tukafanya karamu, tukakaa usiku kucha tukihadithiana. Na John Fedha naye akakaa pale pale akicheka na kufurahi kama ambaye hakuwemo katika wale maharamia na wale walioasi!
Bonge moja la storiii
 
Niliisoma Kipindi nipo shule ya Msingi std5 Kwenye vitabu vyetu.. John Silver wanamwita Jan Fedha.
 
Back
Top Bottom